BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Saturday, October 16, 2010

Tuzo za ZAFAA kufanyika London october hii.


ZAFAA 2010
          
  African Film Festival & Academy Awards

LONDON

21st to 23rd October 2010


Closing Date for Entries is Monday 31st MAY 2010


Important Notice:

1)      Films Submitted with a VCD copy WILL NOT BE SCREENED at the Festival and may not qualify for nominations.
2)      Films in Native languages should be subtitled in English. Those without subtitles will not be accepted.
3)      Fully complete and return this forms with 3 DVD  copies of the film/s in a securely sealed mailing pack to:
Nollywood Entertainment Ltd.
291 New Cross Road
London
SE14 6AS
United Kingdom

  *** Please indicate if you do not wish your film/s to be screened at the Festival by marking the box ‘For Nomination Only’ ( ) ***
*Note: Films are charged @ £100. Per hour by the council for classification; should you wish your film/s to be screened?  

Tuesday, October 12, 2010

European Film Festival kufanyika october 14 mwaka huu.


TAMASHA la European Film Festival linatarajiwa kufanyika mwaka huu tarehe 14 october katika maeneo ya New World Cinema hapa jijini Dar es salaam,kwa muda wa wiki tatu mpaka tarehe 7 november.


Filamu kutoka nchi za ulaya na Tanzania zitaonesha kila siku. Pia kutakuwa na screen kubwa litakalo wekwa mnazi mmoja kwa siku za jumamosi na jumapili kasoro siku ya tarehe 31 october siku ya uchaguzi mkuu hapa Tanzania.


Sunday, October 10, 2010

Wazungu walioshiriki filamu Bongo waaga


Wanafunzi watatu wa Chuo Kikuu cha Mainz cha Ujerumani, waliopata kushiriki katika filamu na vichekesho nchini, wanajiandaa kuondoka baada ya kumaliza utafiti wao kuhusu masuala mbalimbali ya sanaa za maigizo, utamaduni, mila na uandishi wa habari katika jamii ya Tanzania.
Katika utafiti wao ulioanza mapema Agosti, wanafunzi hao ambao wanazungumza Kiswahili bila ya shida, wameamua kuishi na watu wa kawaida, jambo ambalo linaonekana ni tofauti na wageni wengine ambao mara nyingi huishi kwenye mahoteli ya kifahari.
Tunaishi na watu wa kawaida katika sehemu za uswahilini. Hatukai katika mahoteli ya kifahari kama wazungu wengine,” alisema mmoja wa wanafunzi hao, aliyejitambulisha kwa jina moja la Jorn, alipofanyiwa mahojiano.
Alisema yeye anafanya utafiti kuhusu Watanzania wanavyopokea mambo mbalimbali wanayoyaona kwenye tamthilia mbalimbali za kutoka nje ya nchi na za ndani kama 'Ze Comedy' — zinazorushwa kwenye runinga.
Lengo langu hasa ni kujua, ni kitu gani kinawafanya Watanzania kuangalia vipindi hivi, na jinsi wanavyoishi kulingana na maisha wanayoyaona kwenye vipindi kama hivi,” alisema mtafiti huyo mwanafunzi.
Kama sehemu ya utafiti, alisema, mtafiti unalazimika kukaa pamoja na watu wa kawaida na kuangalia vipindi hivyo ili kujua ni masuala gani yanawafurahisha Watanzania katika vipindi hivvyo.
Mwanafunzi mwingine, aitwaye Marie, alisema anafurahishwa na ujuzi na utaalamu wa waigizaji wa Kitanzania katika vipindi mbalimbali vya maigizo vinavyorushwa kwenye televisheni ya ITV na EATV.
Ni utaalamu wa viwango vya juu unaofanywa na waigizaji wa tamthilia hizi. Nimeshaongea na baadhi ya waigizaji hawa, na bado naendelea kuwahoji kama sehemu ya utafiti wangu,” alisema Marie.
Mwanafunzi mwengine, Jan, alisema wanachukua muda mwingi kuishi na watu wa kawaida uswahilini, kula vyakula vya watu wa kawaida, kupanda madaladala -- ili kujifunza kwa urahisi mila, tabia, utamaduni wa Watanzania na watu wa Afrika Mashariki kwa ujumla.
Jorn ameshiriki katika filamu mbalimbali za nchini zikiwemo za 'Zaidi ya Rafiki' na Tears on Valentine's Day', ambazo tayari ziko sokoni zikipatikana katika DVD na CD.
Baada ya utafiti wao, unaotarajia kumalizika mwezi huu, wanafunzi hao wanatarajia kuandika kitabu chenye kichwa “Utafiti wa Vyombo vya Habari Afrika Mashariki (Media Studies in Africa). Vijana hao wamewaomba Watanzania na watu wa Afrika Mashari kuwapa maoni yao kuhusu thamthilia za nje na za ndani, na masuala mengine kupitia.
CHANZO: NIPASHE

MZEE CHILO miongoni mwa wazee wachache, wanaofanya vizuri kwenye maigizo na filamu.


MZEE CHILO ama Ahmed Ulotu, ni msanii mahiri wa filamu nchini,.
                           
Huyu ni miongoni mwa wazee wachache, wanaofanya vizuri kwenye maigizo na filamu za kisasa nchini. Umaarufu wake umepaa maradufu tangu alipoibuka katika tamthiliya ya JUMBA LADHAHABU.

Ni kweli Jumba la Dhahabu, ndilo lililomtangaza zaidi, lakini Mzee Chilo ni mwigizaji kwa zaidi ya miaka 40.
Ndani ya tamthiliya hiyo, Mzee Chilo aliigiza kama mzee tajiri, mpole na mkimya, lakini `mafia’, mwenye kutumia fedha zake kufanya
maovu katika jamii na kulipa changamoto Jeshi la Polisi.

Kwa hakika, alifanikiwa kuwavuta watu wa rika zote, kutokana na umahiri wa kuigiza kama baba, anayewajali watoto wake, licha ya kuishi maisha ya anasa yanayoambatana na vitendo
vya uhalifu.

Amewahi kuigiza kama Mzee wa Kanisa anayekumbatia makasisi wenye kufanya maasi mengi, kwa kutumia nafasi zao hizo, ilhali yeye ni Mwislamu kwa dini.

Lakini, pia amewahi kuigiza kama muumini mwenye imani kali ya Kikristo, ambaye alifanyiwa ukatili wa kuibiwa mtoto na kulazimika kusamehe katika filamu ya 'Lost Twins'.

Enzi zake akiwa Azania Ni umahiri wake wa kuuvaa vyema uhusika, ndio uliomfanya, si tu
akubalike ndani ya jamii, bali hata miongoni mwa waigizaji na wachezaji filamu nyota nchini,
wanaopigana vikumbo kumshirikisha katika kazi zao.

Katika mazungumzo ya hivi karibuni yaliyozaa makala haya, Mzee Chilo anasema kwamba, fani hiyo iko katika damu yake. Anasema aliianza miaka mingi, tangu akiwa mwanafunzi katika Shule ya Sekondari Azania, jijini Dar es Salaam mwaka 1966, yaani miaka 44 iliyopita.

Nilipokuwa kidato cha tatu niliteuliwa kuwa miongoni mwa wanafunzi ambao waliwakilisha Shule ya Azania katika mashindano ya sanaa ya maonesho ya jukwaani, maarufu kwa jina la Shakespeare, hapo ndipo nilifanikiwa kuvuta watu wengi ambao walisifu kipaji changu,” anasema.

Anasema kwamba baada ya kuibuka nyota katika mashindano hayo, aliteuliwa kushiriki Tamasha la Mackbeth, mchezo ambao ulikuwa miongoni mwa sanaa za maonesho ya majukwaani, iliyoandikwa na Shakespeare.

Tamasha hilo lilisafisha zaidi nyota yake, kwa kuwa alipata umaarufu mkubwa.

Katika mashindano nilifanikiwa kuibuka mshindi wa pili, ambapo nafasi ya kwanza ilichukuliwa na mtoto wa Balozi wa Nigeria nchini Tanzania….Mtoto huyo alinishinda, kwa sababu ya Kiingereza ilikuwa lugha yake ya kwanza”, anasema.

Hata hivyo, ushindi huo ulimpa changamoto ya kujifunza lugha ya Kiingereza kwa bidii zaidi.

Pia, mashindano hayo yalimwongezea ujasiri wa kusimama mbele ya hadhara na kuigiza.

Kiu yake ya kusaka elimu Katika kuthibitisha kuwa alikuwa na kiu ya elimu, mwaka 1970 alijiunga na Chuo cha Utumishi wa Umma, kilichopo Magogoni jijini Dar es Salaam, ambapo alichukua kozi ya Utawala Bora na kutunukiwa cheti mwaka 1972.

Baada ya kuhitimu masomo, aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Kisarawe katika kitengo cha kilimo.

Alifanya kazi hiyo kwa muda mfupi, kisha akajiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT). Akiwa jeshini, alitumia taaluma yake kufanya kazi za uongozi, jambo lililomwezesha kujenga uzoefu.

Baada ya kuhitimu mafunzo ya jeshi hilo, aliajiriwa katika Kampuni ya viatu ya Bora na baadaye aliamua kusoma, ambapo mwaka 1978 alijiunga na Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Madina, Saudi Arabia na kuhitimu Shahada ya Dini mwaka 1986.

Aliporejea nchini, alifanya kazi ya ualimu na kufundisha vipindi vya dini katika sekondari mbalimbali mkoani Kilimanjaro, ikiwemo Masama, Old Moshi, Weruweru, Kibosho, Umbwe na Mawenzi.

Mwaka 1995 aliajiriwa na Ubalozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania, ambapo alifanya kazi mbalimbali katika kitengo cha utawala, ikiwa ni pamoja na kutafsiri nyaraka mbalimbali.

Alifanya kazi hiyo hadi mwaka 2002. Pia, alifanya kazi ya kuwaongoza mahujaji katika safari za Saudi Arabia, akiwa na Taasisi ya Haji Trust.

Juhudi za kutimiza ndoto ya uigizaji Mwaka 2002 aliamua kutimiza ndoto zake, kwa kujikita zaidi katika sanaa. Alianzia Taasisi ya Dunia Inc, iliyojishughulisha na utengenezaji wa matangazo na filamu na baadaye alitua Bahari Sanaa Group, ambako alikutana na walimu
wapya, ambao walimfundisha sanaa na miiko yake.

Nilijifunza mengi na kwa mara ya kwanza nikaibuka ndani ya filamu inayoitwa 'Sumu ya Mapenzi' nikitumia jina la Ahmed,” anasema.

Kwa kuwa alijituma na kutumia vyema kipaji chake katika filamu ya kwanza, alianza kupata
umaarufu ; na mwaka 2006 akaanza kupata mikataba ya kufanya filamu mbalimbali, kama vile Filamu ya Utata, Tanzia na Simu ya kifo.

Umahiri katika filamu hizo, ulimkuna mmiliki wa kundi la Fukuto, Tuesday Kihangala, aliyemwalika na kumshirikisha katika tamthiliya ya Jumba la Dhahabu, jukumu lake kubwa kucheza nafasi ya mtu `mafia’.

Ili kuimudu nafasi hiyo, alipewa mafunzo mapya ya kujenga ujasiri, kuvaa uhusika pasipo kutetereka na kutumia kipaji chake kuonesha jamii, jinsi dunia inavyoweza kubadilika, ambapo hata baadhi ya matajiri huweza kujihusisha na vitendo vya uhalifu.

Mzee Chilo anasema kuwa baada vya kufanikiwa kuigiza vyema katika tamthiliya hiyo, aliamua kujikita katika filamu na maonesho ya jukwaani, ambapo alisaini mikataba
mbalimbali ya kushiriki katika filamu.

Katika uigizaji wake, amefanikiwa kushirikiana na wasanii mbalimbali, wakiwamo kina Vincent Kigosi `Ray’, Steven Kanumba `Kanumba’, Yvonne Cheyl `Monalisa’, Yusuph Mlela `Mlela’ na Charles Magali `Mzee Magali’.

Anasema tofauti na miaka ya nyuma, ambapo sanaa ya maonesho ya majukwaani ilipuuzwa,
hivi sasa imekuwa sehemu ya ajira ; na kwamba Watanzania wameanza kuvutiwa na sanaa za
nyumbani.

Na baada ya kuonja faida za filamu nchini, Mzee Chilo anakiri kuwa fani hiyo imemsaidia
kubadilisha kwa kiasi kikubwa maisha yake, kuanzia kipato hata umaarufu. Anasema kiu yake ni kuwa mwigizaji wa kimataifa, akilenga kushirikiana na wakali kutoka nchi zilizopiga hatua katika filamu duniani, kama India (Bollywood) na Marekani (Hollywood).

Anasema mikakati ya kutimiza ndoto yake, kwa kuanzia na India, mikakati inafanywa na mmiliki wa Kampuni ya Pilipili Entertainment, Sameer Srtvastiva

Saturday, October 9, 2010

European Union na tamasha kubwa la filamu la European Film Festival ‘EFF' hapa Bongo.


Kampuni ya 1plus Communication kwa kushirikiana na European Union watateremsha Bongo tamasha kubwa la filamu litakalokwenda kwa jina la European Film Festival ‘EFF’ ambalo limekuwa likichukua nafasi barani Ulaya.

Akiongea na Ijumaa juzi msemaji wa ‘event’ hiyo, Tayana Amri (pichani) alisema kuwa, jumla ya mataifa 15 ya bara la Ulaya yatashiriki huku Bongo ikiwa mwenyeji wao.

Ni tamasha litakaloanza tarehe 14 mwezi huu mpaka Novemba 7 ndani ya New World Cinema, kwa siku za kawaida na litachukua nafasi kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja siku za wikiendi kupitia ‘Screen’ kubwa zitakazofungwa hapo,” alisema Tayana.

Katika hatua nyingine afisa huyo wa Kampuni ya 1plus, alianika kuwa, kwa kila siku katika maonesho ya filamu hizo kila taifa shiriki litakuwa na nafasi ya kuonesha filamu tatu tofauti.
Aidha, Tayana aliweka wazi kuwa kwa Jiji la Bongo tamasha hilo litaruka kwa wiki tatu kabla ya kuhamia Arusha ambako litang’aa kwa wiki moja.

Miongoni mwa mataifa yanayotarajiwa kushiriki na kuleta filamu zao katika tamasha hilo ni wahusika wakuu kutoka nchi zote za European Commission, Tanzania, Ubelgiji, Denmark, Finland, Ufaransa, Ujerumani, Ireland, Italia, Norway, Urusi, Sweden, Uswisi Uingereza,Uholanzi na Hispania