BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Monday, December 27, 2010

THIS BLOG IS UNDER CONSTRUCTION.


WADAU WANGU NIKO KATIKA MABORESHO YA BLOG HII HIVYO NINAOMBA RADHI KUWA SITAWAHABARISHA KWA MUDA KIDOGO KATIKA KUWEKA MAMBO SAWA KUPITIA BLOG HII LAKINI SOON JANUARY HALI ITAKUWA KAMA KAWAIDA..

nawatakia heri ya mwaka mpya 2011.


"NAITWA FRANK AMAN MAWENYA NI BLOGGER NAYEJIHUSISHA NA HABARI ZA BURUDANI KUPITIA BLOG ZANGU ZA filamutanzania.blogspot.com NA thazealottz.blogspot.com.NATOA SHUKRANI ZANGU ZA PEKEE ZIENDE KWAKO WEWE MDAU WANGU WA HABARI KUPITIA BLOG ZANGU AMBAZO NI MAHUSUSI KATIKA KUKUPASHA HABARI ZA KI-ENTERTAINMENT KWA HAPA BONGO NA NJE YA BONGO.NATANGULIZA SHUKRANI ZANGU KWA MUNGU MUUMBA WETU AMBAYE AMENIWEKA NA AMEKUWEKA HAI MPAKA SASA TUNAELEKEA KUHITIMISHA MWAKA HUU 2010 NA KUKARIBISHA MWAKA MPYA 2011.NAWAPA POLE WADAU WALIOPATWA NA MATATIZO MBALIMBALI YA KIJAMII KAMA MAGONJWA,MISIBA,AJALI NA MATUKIO MENGINE YOTE YA KUHUZUNISHA NA PIA MUNGU AZIWEKE MAHALI PEMA PEPONI ROHO ZA WENZETU WALIOTUTANGULIA MBELE ZA HAKI....

MWAKA 2010 UMEKUWA MWAKA WA MAFANIKIO KWANGU NAMSHUKURU MUNGU KWA HILO LAKINI PIA NAWASHUKURU WATU WALIO NISAPOTI MPAKA HAPA,NA WALIONISAIDIA KWA USHAURI NA MAMBO MENINE MENGI.NAKUAHIDI MAMBO MAKUBWA KWA MWAKA UJAO WA 2011 KWANI KWA SASA NAOMBA KUWAARIFU KUWA BLOG HII ITAKUWA UNDER CONSTRUCTION KWA MUDA ILI KUWEZA KUJA UPYA NA MAMBO MAZURI KABISA HIVYO NAOMBA LADHI KWA WADAU WANGU KWA UKIMYA UTAKAOKUWEPO MPAKA PALE NTAKAPO REJEA JANUARY 2011.NAKUSHUKURU KWA KUWA PAMOJA MWAKA HUU UNAOISHA NA PIA NAKUSIHI ENDELEA KUWA NA MIMI MWANZO MWISHO KWA HABARI KEM KEM ZA KI BURUDANI NDANI NA NJE" KUTAKUWA NA MABADILIKO MENGI SEGMENT MPYA MWONEKANO MPYA WA BLOG NA HABARI NZURI NA HOTTEST/LATEST KWAKO KUZIPATA.

WAWEZA KUWASILIANA NA MIMI KWA MAONI ZAIDI NA USHAURI KUPITIA E MAIL ADDRESS YANGU famanmawenya@yahoo.fr AMA WAWEZA KUTANA NA MIMI KATIKA FACEBOOK KWA JINA LA FRANK THA ZEALOT AMA ANDIKA fzealot/facebook UTANIPATA KWA STORY ZAIDI.

Monday, December 20, 2010

PERFECT ARTS GROUP WANAHITAJI WASANII

Kundi la Perfect Arts Group wanakutangazia kwamba kama una kipaji cha cha kuigiza unaweza mara moja kujiunga nao, piga simu namba 0716066078 ama 0787122976 .Atakayepokea ni muigizaji maarufu wa filamu anayeitwa Kishoka. Kundi hili huwa linafanya mazoezi katika Hotel ya Top Life, Kinondoni Mkwajuni jijini Dar es Salaam kila siku kuanzia saa kumi na moja jioni, wote mnakaribishwa. Baadhi ya filamu ambazo kacheza bingwa huyu ni Bad Night, Mbwembwe, Before Mid Night na nyingine kibao.

FRANK AJA NA FILAMU YA 'THE GIRL NEXT DOOR'.

MSANII nyota wa filamu Tanzania Mohamed Mwikongi (Frank) baada ya kimya cha muda anakuja na filamu kali na ya kusisimua ya The Girl Next Door filamu hii ambayo ipo katika hatua za mwisho katika kurekodiwa ni filamu ambayo inatarajiwa kumrudisha msanii huyu kwa nguvu katika tasnia hii ya filamu baada ya kufanya vizuri katika filamu ya Pretty Girl .
 
Nakuja na filamu ya ukweli, inayoshirikisha wasanii nyota na wenye uwezo katika game hili, najua wengi wamenimis sana kwa kutoandaa filamu yangu kama siku za nyuma, sasa narudi kwa nguvu na naibuka na kitu cha ukweli cha The Girl Next Door
alisema Frank.

Monday, December 13, 2010

TAFF KUWEKA BEI MOJA YA FILAMU KWA WASAMBAZAJI MWAKA 2011.


KATIKA kubororesha soko la filamu kuanzia mwakani mwezi wa kwanza bei ya filamu itapanda na kuletwa bei mpya ya filamu, lakini si kupanda tu bali vile vile kutakuwa na bei moja kwa wasambazaji wote tofauti na ilivyo sasa, ambapo kila msambazaji anakuwa na bei yake kiasi cha kuwachanganya wanunuzi wa filamu kwa hapa nchini.
Haya yanafanyika kwa kufuata utaratibu uliopangwa na TAFF kwa wanachama wake.

Bei ya sasa sokoni ni tata kwani wakati kauli ya pamoja ya wasambazaji baada ya kushusha bei ilipangwa wauze filamu kwa bei ya Tshs. 2,000/= hadi 2,500/=, kwa sasa kuna kampuni ambayo wanaamini kuwa ni kubwa wao wanauza Dvd moja kwa Tshs. 1,600/= hadi 1,000/= wadau wanaamini kuwa kukiwa na chombo cha kusimamia bei na wasambazaji kwa ujumla soko litaenda mbele.

Wasambazaji kwa sasa tayari kupitia Shirikisho la vyama vya filamu Tanzania (TAFF) wameunda chama chao kinachojulikana kama Tanzania Film Distributors Association (TFDA).
Bei mpya ambayo imependekezwa na TFDA ni Tshs. 3,000/= kwa Dvd moja hii ni bei ya jumla, hata hivyo tumegundua kuwa pamoja na misuguano kuhusu punguzo la bei za filamu inayoletwa na wasambazaji haina faida kwa mnunuzi wa mwisho kwani Mmachinga akinunu kwa bei yoyote yeye atauza kwa bei kubwa tu, na Wamachinga ndio wenye kupanga bei huku wakiangalia maslahi zaidi kwao.

FILAMU YA REASON TO DIE SASA INAPATIKANA SOKONI.


FILAMU ya A Reason to die iliyoshirikisha mastaa wakali imeingia jana sokoni na inapatikana nchi zima, filamu hii iliyofanikiwa katika kuonyesha uhalisia hasa sehemu za mapigano ni hadithi inayomwelezea binti Nyika anayeingi mikononi mwa jambazi hatari Dr. Cheni na kujikuta anamtia baba yake katika matatizo makubwa bila ya kujua, akiongea na mtandao huu mmoja wa washiriki.

Filamu hiyo inasambazwa na Gibs Media Pro ya jijini Dar es Salaam, A Reason to die imeshirikisha wasanii nyota kama Elizabeth Michael (Lulu), Christina Mhina, Mahsein Awadh ( Dr. Cheni), Peter Mhina, Abdul Bendera ( Mr. India), Teacher John na wasanii wengine wakali katika masuala ya filamu hapa nchini.

Wednesday, December 8, 2010

Esther Flavian Mwanadada nyota chipukizi kutoka D production

Huyu ni mwanadada chipukizi katika tasnia ya filamu na amezidi kuwa kinara katika filamu tofauti tofauti hasa filamu iliyotoka hivi karibuni kutoka katika kampuni ya D production ijulikanayo kama AUNT SUZZY na nyingine nyingi. Pia Esther ni moja ya Video Queen wa nyimbo mbali mbali kama wimbo wa Sam ujulikanao kama Sina Raha, pia wimbo wa Dullayo uitwao Naumia roho.

Akizungumza na blog hii Esther ametoa mawazo yake kuhusiana na tasnia hii kuwa "ubovu wa filamu unaolalamikiwa hivi sasa na mashabiki wa sanaa hiyo nchini unatokana na tamaa ya waandaji wa ‘filamu’ hizo kutaka kupata ‘fedha ’ za haraka haraka." Aliongeza kwa kusema malalamiko ya mashabiki juu ya kutoeleweka kwa hadithi za filamu za Kibongo wanayopata hivi sasa unatokana na utayarishaji wa kukurupuka unaofanywa na waandaaji kwa lengo la kuingiza mkwaja haraka haraka jambo ambalo linafanya kazi hizo kukosa ubora.. asema Esther.
Kati ya filamu alizocheza kupitia D production ni pamoja na hiyo ya Aunty Suzzy, Fake pregnant, Where is Love na nyingine kibao chini ya mtayarishaji na muigizaji daudi michael..
 

Monday, December 6, 2010

GAME 1st QUALITY kuja na MORNING ALARM.

Wakati akiendelea kutesa hivi sasa na Uncle JJ, mkali wa filamu Bongo Steve Kanumba anatarajiwa kuiteka tena tasnia ya filamu Bongo na muvi yake nyingine iliyopewa jina la Morning Alarm. Katika filamu hiyo, Kanumba anashirikiana na 'mchizi' Benny, kijana ambaye anasifika kwa kuigiza filamu za comedy na ujambazi.

Katika muvi hiyo kuna mastaa wengine kibao kama vile Hashim Kambi, Maya, Flora Mvungi, mwanamuziki Patcho Mwamba na wengine wengi Ikiwa ni kazi nyingine makini kutoka chini ya Kampuni ya Game1st Quality, filamu hii inatarajiwa kuliteka soko la muvi itakapoingia mtaani hivi karibuni.

Sunday, December 5, 2010

Kutoka Udereva teksi hadi msanii na mwandaaji wa filamu


*Anatingisha na filamu za ‘Fake Pregnant’ Where Is Love, na sasa ‘Aunt Suzzy’.

WASANII nchini wataneemeka na kufaidi matunda ya kazi zao za filamu nchini ni pale tu watakapoamua kutoa kazi zilizo na ubora, utashi kwa jamii ikiwemo kufikisha ujumbe wa haraka na mpangilio sahihi wa filamu yenyewe.
Hayo ni maneno yake msanii na mwandaaji wa filamu anayekuja kwa kasi kubwa hapa nchini, Daud Michael, anayetamba na filamu za ‘ Upside Down’, ‘Where Is Love’, ‘Fake Pregnant’ na filamu ambayo tayari iko madukani, iliyojaa mastaa kibao ya ‘Aunt Suzzy’.
Emmed Hamis ‘Ramsey wa bongo’, Ester Flavian,Daud Tairo Michael, na Raulant Anthon ‘makala’
Hivi sasa msanii Daud Michael anamiliki studio yake ya kisasa ijushughulishayo na uandaaji wa filamu mbalimbali hapa nchini inayofahamika kama ‘D Production, iliyopo maskani ya Mabibo Makutano jijini Dar es Salaam.
Daud anasema kuwa mpaka alipofikia ni safari ndefu katika tasnia hiyo ya sanaa kwani aliweza kupita milima na mabonde kama wasemavyo waswahili mpaka kufika hapo alipo na kuwa na kampuni yake hiyo sambamba na kutoa filamu zake ambazo jamii wamezikubali.