BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Tuesday, April 24, 2012

JE WASANII WA FILAMU TZ WANATENGENEZA FILAMU AMBAZO WATU WANAZIHITAJI?.

''The most important quality in a filmmaker is… having a balance between creativity, understanding the tools of the trade, and having a keen business sense.''
Whereas many filmmakers have an unbridled creative passion for telling stories and know the tools of their trade, few understand how to create and package content that distributors and audiences want to see. 
Pastor Myamba

TINO AMSHUKIA STEVE NYERERE...

 MWIGIZAJI Nyota wa filamu na mtayarishaji wa filamu Swahiliwood, Hisani Muya Tino, amemshukia mchekeshaji na mwigizaji wa filamu Steven Mangere Steve Nyerere kwa kusema kuwa ni tatizo na mgombanishi wa wasanii wakubwa.

�Huyu Steve Nyerere ni mtu mbaya sana kwa sasa katika tasnia ya filamu, siku za nyuma wasanii walikuwa na ushirikiano wa kweli bila kuwa na makundi ambayo yapo sasa, na kila tatizo ukifuatilia utaambiwa Steve.

"Nimeshangaa sana hata msiba wa Kanumba haujakwisha tayari ameshatengeneza zengwe akidai kuwa mimi nimekaa na mama wa marehemu eti kumponda mdogo wake Seth asipewe kampuni ya Kanumba, hawezi kuongoza nipewe mimi,� anasema Tino.

Tino alisema kuwa Steve Nyerere alimpigia simu kwa kumlaumu kuwa Bongo Movie wapo Leaders wakiwa katika kikao cha kumjadili yeye kwa kuingilia suala la marehemu wakati wao walikuwa wanataka kuisimamia kampuni hiyo kwa kumtumia Seth, lakini Tino anakuwa kikwazo jambo ambalo linawakera, lakini pia alisema anashangaa Steve kujiweka mbele wakati marehemu alijitoa katika kundi hilo.

�Huyu anatakiwa kujua kuwa mimi sijajuana na marehemu juzi, nimekuwa nikifanya naye kazi mbalimbali hata kabla ya kufariki aliniita akaniambia anahitaji tuendeleze mradi wa kuinua vipaji vya wasanii wachanga na kusema nizifuate (tape) mikanda tuliyorekodi kwa ajili ya usaili wa wasanii tuliowafanyia siku za nyuma,� alisema Tino.

Mwanaspoti ilimpigia simu Steve Nyerere ambaye alisema kuwa mambo hayo yalishapita na Tino waliongea naye yakaisha, sasa anashangaa kuyasikia tena yakiendelea bila sababu za msingi wakati yeye anaamini kuwa hayana faida yoyote.

�Jamani hayo mambo yamepita, tumwache marehemu apumzike kwa amani hakuna sababu ya kuendelea na malumbano yasiyotuingizia fedha na tusitafute umaarufu kupitia marehemu, tufanye kazi maisha yaendelee, kama kuna kosa kila mtu kajifunza kwa wakati wake,� alisema Steve.

Kufuatia kifo cha Steven Kanumba kumekuwa na maneno yanayoashiria shari na kuibuka makundi kwa wasanii na kuzua vikao kila kukicha, huku wakishindwa kupanga mikakati imara ya maendeleo yao.

Mawakili wanne kumtetea Lulu


JOPO la mawakili wanne maarufu nchini akiwamo Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHRAGG), Joaquine De Mello, wamejitokeza kumtetea msanii wa filamu, Elizabeth Michael Kimemeta Lulu anayetuhumiwa kuhusika na mauaji ya aliyekuwa msanii maarufu Steven Kanumba.

De-Mello ambaye pia aliwahi kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) na mshindi wa tuzo ya Mwanamke Jasiri Tanzania ya Martin Luther King, anaungana na wanasheria wengine ambao ni Kennedy Fungamtama, Peter Kibatala na Fulgence Massawe katika kumtetea Lulu mwenye umri wa miaka 17.

Fungamtama ambaye ndiye kiongozi wa jopo lao anakumbukwa kwa kuitetea kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans katika kesi dhidi ya Shirika la Umeme la Tanzania (Tanesco).
Katika kesi hiyo Dowans ilishinda na Tanesco iliamuliwa kuilipa Dowans zaidi ya Sh 94 bilioni kwa kuvunja mkataba kinyume cha sheria.

Kwa upande wake, Kibatala ambaye pia anamtetea kada wa Chadema, Fred Mpendazoe, katika kesi ya uchaguzi Jimbo la Segerea, pia ni Makamu wa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), wakati Massawe anatoka Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki za Binadamu (LHRC). 


Mawakili hao walijitokeza jana Jumatatu, mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Ritha Tarimo, kwa ajili ya kumtetea Lulu anayekabiliwa na kesi ya hiyo ya mauaji. Kesi hiyo ilikuja mahakamani hapo jana kwa ajili ya kutajwa.

Baada ya mawakili hao kujitambulisha kumtetea msanii huyo, Wakili Mwandamizi wa Serikali, Elizabeth Kaganda, alidai kuwa upelelezi wa kesi bado haujakamilika na kuiomba mahakama ipange tarehe nyingine.

Hakimu Tarimo aliiahirisha kesi hiyo hadi Mei 7, mwaka huu itakapokuja kwa ajili ya kutajwa.

Lulu alifikishwa mahakamani hapo saa 3:06 asubuhi kwa kutumia gari la Magereza lenye namba za usajili STK 4310 ambalo lilisindikizwa na gari mbili zenye usajili namba STK 4253 na STK 8901.

Alikuwa chini ya ulinzi mkali wa askari sita wa kike wa Jeshi la Magereza pamoja na askari mmoja wa kike wa Jeshi la Polisi.
Askari hao kwa kushirikiana na askari wa kiume wa Jeshi la Magereza zaidi ya sita walimwingiza msanii huyo mahakamani kwa ulinzi mkali kiasi kilichowafanya baadhi ya wapiga picha kushindwa kumwona.

Lulu ambaye alikuwa amevalia vazi la aina ya dira la rangi nyekundu, kutokana na kubanwa katikati ya askari hao wakati akiingizwa mahakamani, alianza kulia kitu ambacho kilimfanya Hakimu Tarimo kumpa pole na baadhi ya askari kumnyamazisha.

Kutokana na kujaa kwa watu mahakamani humo na wengine wakitaka kuzidi kuingia askari wa jeshi la Magereza walitumia nguvu kufunga mlango wa chumba cha mahakama hiyo na kuwezesha kesi hiyo kusikilizwa.

Baada ya kesi hiyo kumalizika, wakili Kaganda, aliiomba mahakama iamuru watu wote watoke nje ili mtuhumiwa aweze kupitishwa kwa sababu walikuwa wamefunga njia.

Kufuatia ombi hilo, hakimu Tarimo aliwaamuru askari kusafisha njia ili waweze kumpitisha msanii huyo kwa kile alichosema kuwa Lulu bado ni mtuhumiwa na anaweza kuumizwa.

"Askari safisheni njia ili mtuhumiwa aweze kupita kwa sababu yeye bado ni mtuhumiwa anaweza kuumizwa,"alisisitiza Hakimu Tarimo.

Baada ya kutolewa kwa amri hiyo askari walitimiza wajibu wao na muda mfupi njia ilipatikana na msanii huyo kutolewa mahakamani hapo chini ya ulinzi mkali.

Hiyo ilikuwa mara ya pili kwa Lulu kufikishwa mahakamani hapo. Mara ya kwanza ilikuwa Aprili 10 mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi, Augustina Mmbando.

Wakati akifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza, polisi walitumia mbinu za kikachero kuwapiga chenga waandishi ambao wengi walikwenda mahakama ya Kinondoni wakidhani mtuhumiwa huyo angefikishwa hapo, lakini akapandishwa Kisutu na kusomewa mashtaka katika kipindi kisichozidi dakika kumi kisha kupelekwa rumande.

Pia tofauti na matarajio, siku hiyo polisi hawakuwa wametumia magari yenye ving'ora na ulinzi wa kutisha kama ilivyotarajiwa bali walitumia magari mawili madogo na alipofika mahakamani hapo, alisomewa shitaka hilo na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Elizabeth Kaganda.

Kaganda akimsomea hati ya mashtaka Lulu, alidai kuwa Aprili 7, mwaka huu, maeneo ya Sinza Vatican katika wilaya ya Kinondoni, Lulu alimuua, Steven Kanumba.

Baada ya kumaliza kusoma shtaka hilo, Kaganda alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika hata hivyo, Lulu hakuruhusiwa kujibu chochote kwa sababu Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina uwezo wa kuisikiliza kesi hiyo hadi Mahakama Kuu.

Hakimu Mmbando aliamuru Lulu apelekwe rumande katika Gereza la Segerea kwa sababu shtaka linalomkabili ni moja kati ya mashtaka yasiyo na dhamana.

Kanumba alifariki dunia usiku wa Aprili 7 kwa kile kilichodaiwa kuwa ni baada ya ugomvi baina yake na Lulu. Alizikwa kwenye makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Wednesday, April 18, 2012

SHIRIKISHO LA FILAMU LAMSHUKURU RAIS JK

Rais wa TAFF, Simon Mwakifwamba, akitoa shukrani wakati akiongea na vyombo vya habari.

Tuesday, April 17, 2012

WASHINDI WA KILIMANJARO MUSIC AWARD KUFANYA ZIARA MIKOANI


Meneja wa kinywaji cha bia cha Kilimanaro Lager akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Savannah Lounge jijini Dar es salaam kuhusua ziara ya washindi wa tuzo za Kilimanjaro Music Award, Katikati ni mwanamuziki Diamond na kushoto ni Mwakilishi wa EATV Olympia Franteu.
 
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake cha Kilimanaro Premium Lager ambao ni wadhamini wakuu wa Kilimanjaro Music Awards leo wamezindua rasmi ziara ya washindi wa tuzo hizi kwa mwaka 2012.
 
Ziara hizi zitakazofanyika katika mikoa 6 ya Tanzânia zitahusisha uvumbuzi wa vipaji vichanga vya wasanii wa muziki wa kizazi kipya. Mikoa itakayohusishwa ni Dodoma, Mwanza, Kilimanjaro, Mbeya, Mtwara na kilele kuwa Dar es Salaam.
Ziara hii ya aina yae itajumuisha wasanii walioshinda tuzo za muziki za Kili, na hão watakaozinduliwa kwenye mikoa husika na kuwapa nafasi wasanii hão chipukizi kushiriki kikamilifu na kuonyesha vipaji vyao kama mpango wa bia ya Kilimanjaro wa kuzindua vipaji.
 
“Tunataka kuondoa mawazo hasi yaliyopo kwamba Tuzo za muziki za Kili ni za Dar es Salaam tu. Mwaka huu bali na kuwapeleka washindi wa tuzo mikoani tumeamua pia kuzindua vipaji vipya kweye mikoa hiyo kwani tunaamini kuwa vipaji vya muziki vinapatikana Tanzânia nzima. Vilevile tutawapa nafasi wasaniii watakaovumbuliwa kuimba na washindi vinara wa tuzo za Kili ambapo mshindi mmoja wa kila mkoa ataletwa Dar es Salaam kushiriki kwenye tamasha la mwisho la ziara, na pia kurekodiwa nyimbo moja ya kumwezesha kuanza safari yake ya muziki.” Alisema George Kavishe meneja masoko wa bia ya Kilimanjaro.
 
Kati ya wasanii watakaoshiriki kwenye ziara hizi za washindi wa tuzo za Kili ni pamoja na Diamond, Khadija Kopa, Suma Lee, Warriours from the East, Ali Kiba, AT, Aisha Msharuzi, Twanga Pepeta, Ben Pol, Roma, Ommy Dimples, Kalijo Kitokololo, Jaguar na Barnaba. Msanii mahiri Diamond ambaye amejinyakulia tuzo 3 kwenye tuzo za Kili wiki iliyopita alisema “Nina furaha kubwa kuwa kati ya washiriki wa ziara hizi, ni nafasi ya kipekee kwa mimi kukutana na mashabiki wangu walioko mikoani na kuwaonyesha shukurani zangu kwa upendo wao kwangu” Mbali na ziara hii kutegemea kuongeza mshikamano wa watanzania kwenye kushabikia muziki wa ndani pia itaongeza msisimko wa watanzania kushabikia wasanii wetu mahiri.
Ziara za tamasha zitaaza mkoani Dodoma tarehe 28 Aprili (Jamuhuri Stadium), - Mwanza tarehe 5 Mei (CCM Kirumba), Kilimanjaro tarehe 12 Mei(Ushirika Stadium), Mbeya tarehe 19 Mei (Sokoine Stadium), Mtwara tarehe 26 mei (Mtwara Stadium) na Dar es Salaam tarehe 2 June (leaders club).
 
Uvumbuzi wa vipaji utafanyika kwenye mikoa mitano kila mwisho wa juma, wiki moja kabla ya tarehe ya tamasha, ikianza na Dodoma tarehe 22 April (Club 84), Mwanza tarehe 29 April(Villa Park), Kilimanjaro tarehe 6 Mei (Mr. Price- Moshi), Mbeya tarehe 13 Mei (Vibes) na Mtwara tarehe 20 Mei (Maisha club).
Majaji wa kuamua mchakato wa uvumbuzi wa vipaji ni pamoja na Juma Nature, Proffessor Jay na Queen Darleen. “ Nikiwa kama mdau wa siku nyingi wa muziki wa kizazi kipya nchini natumaini nitatoa mchango mkubwa kwenye zoezi hili la kuzindua wasanii chipukizi mikoani. Nategemea kuona washiriki wa ike wakijitokeza kwa wingi kwani kuna pengo kubwa sana la uchache wa wasanii wa kike nchini” alisema msanii Professor Jay..
“Tunawaasa wenye vipaji vya musiki kujitokeza kwa wingi na kushiriki kwenye mchakato huu wa kuzindua vipaji ili wapate nafasi ya kuendeleza vipaji vyao” alimalizia bwana Kavishe.
Ziara nzima itarekodiwa na kuonyeswa kwenye kwenye televisheni ya EATV ambapo watanzania watapata nafasi ya kujionea jinsi mchakato mzima wa kuvumbua vipaji na matamasha yalivyoenda.

Monday, April 16, 2012

ALIKIBA AKANUSHA KUHUSIKA NA KUMTOROSHA LULU


Kutokana rumors zilizoenea kitaani na kwenye baadhi ya Vyombo vya habari kuwa Eti msanii Ali Kiba amehojiwa na Polisi baada ya Kushukiwa kuwa eti ni yeye ndiye aliye enda kumtorosha Mwanadada Lulu Nyumbani kwa Kanumba (Siku ile ambayo inadaiwa kuwa Lulu eti alisababisha Kifo cha Steven Kanumba kwa kumskuma na Mwigizaji huyo kujigonga Kisogoni na Kufa papo hapo)
Then baada ya tukio hilo Lulu si alipotea nyumbani kwa Kanumba, basi ndo rumorz zikaenea Ali Kiba ndie aliyemfata na Gari Lulu maeneo ya Sinza vatican na kufanikiwa kuondoka nae eneo la tukio.
Sasa Ali Kiba anasema siku hiyo ya Tukio yeye alikua ufukweni Coco Beach anakula bata, ndo akaskia watu wanaongea kwamba Kanumba kafaa, ndipo yeye akaamua kumvutia wire Lulu na kumuuliza ukweli wa taarifa hizo, lakini Lulu alimjibu sio kweli ila Steven Kanumba ana umwa, basi baada ya Muda akapata simu kutoka kwa Mama mtoto wake flani hivi anayeishi maeneo ya Sinza, akamwambia Kanumba amekufa na mwili wake ameuona ukiingizwa Mochwari.
Kuhusu ishu ya kutokuwepo Dar asubuhi ya siku hiyo Ali Kiba amejibu kuwa Alfajiri ya siku hiyo alisafiri kikazi na kuelekea Malindi Mombasa/Kenya  na taarifa kuwa aliwakimbia polisi si kweli.

HAPPY BIRTHDAY LULU


HAPPY BIRTHDAY LULU Leo ni siku aliyozaliwa lulu lakini UTATA wa umri wa Elizabeth Michael ‘Lulu’ anayekabiliwa na kesi inayomhusisha na kifo cha Steven Charles Kanumba ‘The Great’ unazidi kugubika katika ishu hiyo baada ya baba yake mzazi, Michael Edward Kimemeta kuibuka na kutofautiana na watu wengine akiwemo mama ...mzazi wa Lulu, Lucresia Karugila hivyo kushindwa kung’amua nani muongo na nani mkweli. Uchunguzi umebaini kuwa katika ishu hiyo, kuna mambo mengi yanayosemwa ya uongo na mengine ya ukweli. BABA LULU Mwishoni mwa wiki iliyopita, baba huyo wa Lulu anayeishi Moshi mkoani Kilimanjaro ambaye hakuwahi kusikika kwenye vyombovya habari, alijitokeza kwa mara ya kwanza na kudai kuwa binti yake ana umri wa miaka 16. Baba Lulu alikaririwa: “Mwanangu alizaliwa mwaka 1995, atatimiza umri wa miaka 17 ifikapo Aprili , mwaka huu (leo). Kwa sasa ana umri wa miaka 16.” LULU Kabla ya Kimemeta kugusia hoja hiyo alipokuwa akiwataka Watanzania kutomhukumu bintiye na kuacha haki itendeke, tayari Lulualishaiomba mahakama kurekebisha umri wake kuwa siyo miaka 18 kama ilivyokuwa ikielezwa bali ni 17. “Mheshimiwa hakimu, naomba kurekebisha umri wangu, nina miaka 17 na siyo 18,” Lulu aliiambiaMahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu alipofikishwa mahakamani hapo Aprili 11, mwaka huu. MAMA LULU Kwa upande wake, mama Lulu alisisitiza kuwa yeye ndiye aliyemzaa Lulu hivyo anajua vyema umri wa bintiye. “Mimi ndiye niliyemzaa Lulu, ana miaka 17,” alisema bila kutaja tarehe aliyozaliwa mwanaye kama alivyofanya baba. HALIMA MDEE Naye Mbunge wa Kawe kwa tiketi ya Chadema, Mhe. Halima Mdee alipokwenda Kituo cha Polisi Oysterbay kumuona Lulu, alidai kuwa aliona cheti cha kuzaliwa cha Lulu kikiwa kinaonesha ana umri wa miaka 17. “Niliona cheti cha kuzaliwa, Lulu ana miaka 17,” ....yoyte kwa yote happybirthdy lulu

Mwenyekiti wa vijana CCM ajiengua

Mwenyekiti wa Umoja wa vijana Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Arusha (UVCCM ), James Ole Milya ametangaza kujiengua katika chama chake.
Kwa habari zaidi ungana nasi baadaye.

NORA KURUDI KWA NGUVU NA I CAN’T FORGIVE.

Nuru Nassor
Nora msanii wa filamu Swahiliwood.

MWANADADA Nyota katika tasnia ya filamu Swahiliwood Nuru Nassor ‘Nora’ baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu katika mambo ya uigizaji wa filamu amerudi tena kwa nguvu zote kwa kuingia na filamu inayojulikana kwa jina la I Can’t Forgive, filamu hiyo ipo sokoni na inakimbiza filamu za wakongwe wanaofanya vizuri.
Akiongea na FC mmoja wa watayarishaji ambaye hakutaka jina lake litajwe katika habari amesema kuwa msanii huyo kuwa ni msanii mwenye uwezo wa hali ya juu sana na kwa upande mwingine ndiye kabeba sehemu kubwa ya filamu hiyo na kuifanya iwe ni ya kipekee zaidi.
“Msanii kama Nora ni wa kiwango cha juu sana iwapo anatumika vizuri katika filamu ya I Can’t Forgive kaitendea haki ameigiza kwa kiwango kikubwa sana ni vema tu wadau wasubiri kazi hiyo nakujionea wenyewe jinsi wasanii walioshiriki katika filamu hiyo walivyoonyesha uwezo wao katika kuigiza,”anasema mtayarishaji huyo

RUGE, SHIGONGO, ASHA BARAKA WAKABILIWA NA KASHFA YA KUCHAKACHUA FEDHA ZA MICHANGO MSIBA WA KANUMBA

MAJINA ya watu mashuhuri nchi hii, Erick James Shigongo na Rugemarila ‘Ruge’ Mutahaba- wote wakiwa ni wadau wa tasniya ya Habari yako hatarini kuingia doa.
Kwa nini? Hiyo inatokana na kuwamo kwao kwenye Kamati ya mazishi ya mwigizaji Steven Charles Kanumba, ambayo imeingia kwenye kashfa ya kuchakachua michango ya msiba.
Baadhi ya vyombo vya habari nchini leo vimeripoti kuwa, habari kutoka ndani ya familia ya Kanumba, imeituhumu Kamati hiyo kufanya uchakachuaji wa michango hiyo inayokadiriwa kuwa mamilioni ya fedha, achilia mbali vitu kadhaa, yakiwemo magunia 32 ya mchele.
Kamati ya Mazishi ilikuwa inaundwa  na Mwenyekiti Gabriel Mtitu, Makamu Mwenyekiti, Jacob Steven ‘JB’, Katibu, William Mtitu na Wajumbe Issa Mussa ‘Cloud’ (Mweka Hazina), Kimosa, Vincent Kigosi ‘Ray’, Single Mtambalike ‘Richie’, Dilesh Solanki, Millenne Happiness Magesse, Adele Kanumba (dada wa marehemu), Hartman Mblinyi, Ruge, Ally Choky, Simon Mwakifamba, Eric Shigongo, Steve Nyerere, Mahsein Awadh ‘Dk Cheni’ na Mama Nassor, mmiliki wa nyumba aliyokuwa akiishi Kanumba.
Je, ukweli ni upi. Ni matarajio sasa wahusika wataibuka kujibu tuhuma hizi, hasa ikizingatiwa Kamati iliundwa na watu watu wazito kama Eric Shigongo, mmiliki wa Global Publisher, Ruge Mutahaba, Mkurugenzi wa Clouds Media Group.

Chanzo cha habari hii ni:http://bongostaz.blogspot.com/

Ni kweli kero za wasanii kumalizwa Agosti?


Herieth Makwetta
KUNA msemo unasema: "Kitanda usicholalia hujui hila yake". Kwa tafsiri, msemo huu una maana pana zaidi, na nimeamua kuutumia kama sehemu ya taswira ya uchambuzi wangu wa leo.
Kupitia msemo huu, maana yangu ni kwamba tuepuke utamaduni wa kutoa majibu mepesi kwa maswali magumu, lakini pia sawa na kusema tuepuke kutarajia makubwa bila kuwa na malengo.
Wakati wa mazishi ya msanii maarufu wa filamu, Steven Kanumba, Aprili 10 mwaka huu, akitoa salamu kwa niaba ya serikali, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Emmanuel Nchimbi alisema, namnukuu: "Mwaka huu ni mwisho wasanii kuibiwa kazi zao".
Kama haitoshi, Waziri Nchimbi aliutaja Agosti kuwa ndiyo mwisho wa wizi huo uliodumu miaka chungu mzima.
Napata mashaka kidogo kama vita ya kupambana na wezi wa kazi za wasanii imeweza kudumu kwa miaka mingi kiasi hicho bila mafanikio, halafu leo ije imalizwe katika muda wa miezi mitatu tu.
Ikumbukwe kwamba, wasanii wamekuwa na kilio cha kuibiwa kazi zao kwa muda mrefu na mikakati mingi ilitangazwa kukabiliana na hali hiyo, lakini mpaka sasa hakuna la kujivunia.
Sasa tunapokuja na mikakati mipya ya kupambana na hali hii, ni lazima pia tuangalia nyuma ni kwa kiasi gani tuliweza kufainikiwa tulipoingia kwenye vita hiyo.
Bila kwanza kufanya tathmini ya kweli, ni vigumu kupata majibu ya kweli katika vita hii ambayo naamini kama dhumuni la dhati linawekwa mbele na wadau wakasapoti, bila shaka hakuna litakaloshindikana.
Sina nia ya kupaka rangi nyeusi juhudi za serikali katika kupambana na wizi huo, kwa maneno mengine niseme tu, naungana mkono jitihada zote zitakazochukuliwa kukomesha wizi huu.

Tatizo nilionalo mimi ni kwamba, tuna utamaduni wa kuingiza mambo ya siasa maeneo ambayo kimsingi hayastahili kabisa. Tusijenge porojo kwenye eneo linalohitaji utekelezaji wa vitendo.
Kama mdau wa burudani na wasanii, nafahamu kazi ni ngumu tena inayohitaji nguvu ya ziada katika kutetea kila jasho linalomvuja msanii. Usimamizi wa hali ya juu unahitajika.
Vita hii haitakuwa na mafanikio kwa serikali bila kuwapo na uwekezaji wa msikamano na umoja toka kwa wadau na wapenzi wa sanaa nchini wenye kiu ya kuona wasanii wanakombolewa.
Katika salamu zake, Nchimbi alisema Wizara yake ikishirikiana na Wizara ya Fedha, Wizara ya Kazi na Ajira na Shirikisho la Filamu nchini (TAFF), wameshakutana na kujadiliana namna ya kuzuia wizi huo.
Ifahamike kwamba siyo wa kuzuia wizi pekee yake, kwa vile katika hilo kuna sekta nyingi zinahusika kumkandamiza msanii na mojawapo ni media mbalimbali zinapokea kazi za wasanii na kuzitambulisha kwa jamii.
Kuna matamasha mengi yanafanyika nchini, lakini ukweli ni kwamba hakuna anayefuatilia na kubaini kama wasanii wanalipwa haki zao kama inavyostahili.
Waziri Nchimbi ajisumbue kidogo kwa kuwauliza wasanii wa muziki wa kizazi kipya wanalipwa kulingana na ukubwa wa maonyesho wanayofanya. Atapata jiwabu.
Lakini pia, wasanii wamekuwa wakitumika kutangaza matangazo mbalimbali, je wanapata kulinangana wanachotoa? Hakuna wizi katika hili? Haya ni mambo ya msingi kujiuliza.
Wanaotumia kompyuta kwa kusambaza na kuuza kazi za wasanii wanatoa malipo kwa wasanii? Wasambazaji wanafanya wanavyotaka katika kuuza kazi za wasanii, wanawasainisha mikata isiyokuwa na tija kwao.
Huu nao wizi wa kazi za wasanii, tena ni vigumu kuudhibiti. Kana kwamba haitoshi, wapo baadhi wanatengeneza kazi feki za wasanii na kuziuza bei rahisi.
Sheria iliyopo dhidi ya watu wanaokamatwa wakirudufu kazi za wasanii na kuziuza, haina meno na kwa muonekana wake imekuwa kama kichocheo cha kuendelea kuwapo kwa hali hiyo.
Eneo hili ni lazima lifanyiwe marekebisho, kwa maana ya nyongeza ya adhabu dhidi ya wezi hao ambao baadhi yao jamii imekuwa ikiwakumbatia na kuwafanya kama watu wema.
COSOTA chombo kilichobeba dhamana ya kusimamia ulinzi wa haki za wasanii nchini, kimeshindwa kufikia malengo yake. Hili halina ubishi, kwani hali ya kuibiwa wasanii imeendelea kuwapo.
Ukichunguza kwa makini ni takribani miaka mitano sasa COSOTA haina bodi, ilikuwa inapataje ruzuku? Audited reports zilikuwa zinapitishwa na nani?
COSOTA hukusanya fedha kwa niaba ya wasanii bila kuwa na Bodi, sasa ushahidi gani unaweza kuwekwa mbele ya jamii juu ya matumizi ya fedha hizo.
Utafiti wa hivi karibuni unaonyesha kuwa pato la sekta ya sanaa ya muziki peke yake linafika Sh78 Bilioni. Je, itakuwaje na sekta ya filamu ikijumuishwa hasa ukizingatia kuwa filamu za Tanzania zinauzwa sana ndani na nje ya nchi?
Nina hakika kama serikika ingekuwa makini katika hili, bila shaka ingekusanya mapato mengi ambayo yangeweza kutumika katika shughuli mbalimbali za ustawi wa jamii.
Lakini pia wasanii wangeweza kupata stahili zao ya malipo kutokana na kazi zao. Tumeona viongozi wakishiriki katika uzinduzi wa albamu mbalimbali za wasanii, hapa ukweli ni kwamba anayetangazwa siyo msanii ila msambazaji wa kazi ambaye hata kodi halipi?
Ni wajibu wa viongozi na watendaji wa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo kuanza kupitia suala moja baada ya jingine ili kujiridhisha kwa kupata taaarifa kamilifu kuhusu sekta ya sanaa kabla ya kuanza kutekeleza kazi hii.

Habari hii ni kwa hisani ya gazeti la Mwananchi.

Sunday, April 15, 2012

KILIMANJARO TANZANIA MUSIC AWARDS (KTMA) ILIVYOFANA MLIMANI CITY JANA..

MWANAMUZIKI nyota wa muziki wa Kizazi kipya, Naseeb Abdul maarufu kwa jina la Diamond ameibuka tena kinara wa Tuzo za Muziki za Kilimanjaro (KTMA) baada ya kujishindia tuzo tatu tofauti kwa mwaka 2012.
Diamond ameshinda tuzo hizo usiku huu katika Mkumbi wa Mlimani City baada ya kuibuka na tuzo ya Mtumbuizaji Bora wa Kiume, Mtunzi Bora wa Nyimbo na msanii ambaye ametoa Video Bora ya Muziki kwa mwaka huu.
Wimbo wa mwanamuziki huyo nyota ulioshinda katika tuzo hizo ni ‘Moyo Wangu. Hii ni mara ya pili ambapo Diamond anaibuka kinara wa mashindano ya KTMA, kwani mwaka juzi pia alikuwa msanii wa kwanza aliyejinyakulia tuzo nyingi zaidi.
Mwanamuziki Diamond akipiga picha na mama yake wa pili kutoka kushoto na Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka kutoka kulia pamona na wanenguaji wake mara baada ya kupokea tuzo yake ya Mtunzi Bora wa Nyimbo.

Katika tuzo hizo wanamuziki walioshika nafasi ya pili kwa kujinyakulia tuzo mbili ni watatu wote kutoka muziki wa kizazi kipya, ambao ni Suma Lee, Ommy Dimpoz na Roma. Suma Lee ameshinda tuzo ya Afro pop (akunaga) na wimbo bora wa mwaka, Ommy Dimpoz ameshinda tuzo ya msanii bora anayechipukia na wimbo bora wa kushirikiana, huku Roma akijinyakulia tuzo ya mwanamuziki bora wa Hip Hop na wimbo bora wa Hip Hop.
Wasanii wengine ambao wamejinyakulia tuzo moja moja katika KTMA na tuzo zao kwenye mabano ni pamoja na Hadija Kopa (Mtumbuizaji Bora wa Kike), Janguar (Wimbo Bora wa Afrika Mashariki), Judith Wambura-Jay Dee (Muimbaji Bora wa Kike), Barnabas (Muimbaji Bora wa Kiume), Ben Paul (Mwanamuziki Bora wa R & B), Isha Ramadhan (Wimbo Bora wa Taarab), A.T (Wimbo Bora wenye vionjo vya Asili) na rapa Kanjo Kitokololo (aliyeshinda tuzo ya Rapa Bora wa Bendi).
Wengine walioshinda katika tuzo hizo ni pamoja Bendi ya Twanga Pepeta (Wimbo Bora wa Kiswahili), Manek kutoka A.M Records (tuzo ya Mtayarishaji Bora wa mwaka). Wanamuziki King Kiki na Marehemu Dk. Remmy Ongala pamoja na Taasisi ya JKT wameshinda tuzo ya kutoa mchango mkubwa katika tasnia ya muziki. 



















WAIGIZAJI NINAOKUBALI KAZI ZAO KATIKA TASNIA YA MAIGIZO


Haya ni majina ya wacheza filamu ambao kwa mujibu wa blog hii inatambua ubora wa kazi zao na wanafanya vizuri katika soko la tasnia ya uigizaji nchini na nje ya nchi. Na hii ni maoni yangu binasfi  kama una maoni tofauti si mbaya ukinandikia…


The late Steven Kanumba


Jb


Ray


Cheni


Johari
Richie


Sajuki


Mlela


Hemed





Natasha and Monarisa

Lulu





Cloud

Tino




Uwoya




Haya ni majina ya comedian ambao kwa mujibu wa blog hii inatambua ubora wa kazi zao na wanafanya vizuri katika soko la tasnia ya uigizaji nchini na nje ya nchi. Na hii ni maoni yangu binasfi  kama una maoni tofauti si mbaya ukinandikia…


Majuto


Masanja


Mpoki


Joti




Wakuvanga


gamac legani wa pili toka kulia.


mtanga
Evans Bukuku


Masele chapombe