BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Saturday, November 24, 2012

Msanii wa Filamu Tanzania John Maganga afariki

John Maganga
Marehemu John Maganga mwigizaji wa filamu enzi za uhai wake.
KATIKA Tasnia ya filamu Swahiliwood wiki hii imekubwa na simanzi baada ya wasanii wake kuaga Dunia siku ya jana msanii mahiri wa maigizo Halid Mohamed ‘Mlopelo’ alizikwa na leo hii tasnia hiyo imekubwa na msiba mwingine mkubwa baada ya John Maganga kufariki katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
John Maganga
Marehemu John Maganga akiwa na msanii mwenzake katika moja ya sene.
John Maganga
Marehemu John Maganga enzi za uhai wake.
Taarifa za awali zinasema kuwa marehemu John amefikwa na mauti baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa tumbo, ni huzuni kwa wasanii na wadau wa tasnia hiyo ya filamu kwani wengi wamedai kuwa msanii huyo ni jana tu walikuwa naye katika matembezi na leo hatunaye tena.
Taarifa zaidi kuhusu mazishi mtazipata hapa hapa bado timu ya FC inajaribu kufuatilia kwa karibu na kuwataarifu, Bwana Mungu alitoa na ametwaha jina lake lihimidiwe.