BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Tuesday, November 23, 2010

FILAMU MPYA YA DON'T CRY KUTOKA KWA BABA HAJI

       
MUIGIZAJI mahiri na nyota wa filamu hapa nchini Haji Adam almaarufu kama Baba Haji amerudi kwa kishindo na filamu yake ya Don’t Cry, Baba Haji ambaye kwa sasa yupo chuo cha Sanaa Bagamoyo akiongeza ujuzi zaidi, kwa muda kidogo msanii huyu alikuwa ametoweka kwa kutoonekana katika filamu akishiriki kwa sehemu kubwa ya filamu zaidi kushiriki scene chache tu.
       Safari hii katika filamu hii ameshirika kama Steringi na pia akiongoza filamu hii filamu ya Don’t Cry inasambazwa na kampuni ya Al Riyamy Production Limited ya jijini Dar es Salaam..
       Don’t Cry imetoka hivi karibuni na kusambazwa nchi nzima katika filamu hii unakutana na wasanii wakali wa filamu walioshiriki katika filamu hii ni kama mwanadada ambaye kwa sasa ni tishio kwa wasanii wa kike mwenye mvuto wa kufa mtu, muigizaji mahiri Rose Ndauka, Diana Nsumba na wengine wengi.

No comments:

Post a Comment