BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Thursday, November 10, 2011

NOLLYWOOD ACTOR,DANIEL IYAMU ALLEGEDLY MURDERED BY HIS WIFE

The Nigerian movie industry otherwise known as Nollywood again was thrown into mourning on Tuesday, as it lost one of its respected actor, Daniel Iyamu to the cold hands of death.

Sources revealed that the Benin based actor was allegedly murdered by his wife.

Family sources said that Iyamu was found dead in a pool of his blood on his bed after neighbours forcefully broke his door open.

It was learnt that injuries were found on his head which suggested that he might have been hit on the head while asleep.

The wife has reportedly made statements to the police amidst tears, saying that she hit her husband with a pestle which led to his death.

One of the children of the late actor, Faith, a student of Federal Polytechnic Auchi, told journalists that their mother has been suffering from suspected mental illness, which their father has been treating since last year

Tuesday, November 8, 2011

AKUTWA CHUMBANI KWA DBANJI....


AWALI alikanusha kwamba hana uhusiano wowote wa kimapenzi na msanii Fally Ipupa wa Congo, lakini sasa Nadia Buari amefumwa nyumbani kwa mwanamuziki Dbanj wa Nigeria.

Msanii huyo raia wa Ghana alifumwa ndani ya jumba la mwanamuziki huyo usiku hivikaribuni akiwa amejivinjari kwenye kigauni cha kulalia huku akigonga mvinyo.

Chanzo kingine kimethibitisha kwamba mastaa hao wamekuwa na uhusiano wa kimapenzi muda mrefu na hata Ghana wamekuwa wakionekana pamoja. Nadia anayekaribia miaka 30.

Kama ni kweli wawili hao wana mpango wa kuoana utakuwa ni mwisho wa uvumi uliokuwa umeenea kwamba D'banj alikuwa kwenye penzi zito la muigizaji Genevieve Nnaji.

VICHWA VYA MTITU...


MARA nyingi watayarishaji wa filamu za Bongo hupenda kuwatumia wasanii wenye majina maarufu, kuliko kutafuta vipaji vipya ili kuvina nafasi.
Lakini hali hiyo ni tofauti kidogo kwa mwongozaji na mtayarishaji wa filamu, William John, maarufu kwa jina la Mtitu, ambaye ni Mkurugenzi wa 5 Effect ya jijini Dar es Salaam.
Awali alianza na filamu iliyojulikana kwa jina la Sandra ambapo aliwashirikisha wasanii waliokuwa wakivuma na michezo ya kuigiza kama Single Mtambalike na Haji Adam.
Mtayarishaji huyo ambaye anaamini kuwa ukiwa na hadithi nzuri inaweza kuwakilishwa na msanii yeyote mwenye sifa na vigezo vya kuigiza.
Wasanii aliowaibua na kuwa nyota hadi leo ni Aunt Ezekiel, Yusuph Mlela, Irene Uwoya na Mariam Ismail. Wasanii hao kwa sasa ni nyota na wanatesa katika tasnia ya filamu.
Aunty Ezekiel
Msanii huyu kwa mara ya kwanza kabisa alishiriki filamu iliyojulikana kwa jina la Miss Bongo, Mtitu anasema kuwa baada ya kuandaa filamu hiyo, alifanya usahili kwa wasanii mbalimbali lakini nafasi ya Miss ilisumbua hadi alipompata
Yusuph Mlela
Ni kijana aliyekuwa katika fani ya mavazi, lakini Mtitu alimwibua na kumfanya kuwa mmoja kati ya wasanii wanaotesa katika tasnia ya filamu, alipomshirikisha katika filamu ya Diversion Of Love.
Humo aliigiza nafasi ya msanii chipukizi na kuibuka mshindi katika Tuzo za Vinara kupitia filamu hiyo.
Irene Uwoya
Hana tofauti na Mlela kwani naye akitokea katika mambo ya urembo kama alivyokuwa Aunty Ezekiel, alipewa uhusika katika filamu ya Diversion Of Love na kufanya vizuri.
Mariamu Ismail
Ni msanii ambaye tayari anatikisa anga hizi za tasnia ya filamu baada ya kuibuliwa na Mtitu kwa kumshirikisha katika filamu ya Best Man, ambayo ameiigiza kwa umahiri mkubwa na kuwafunika baadhi ya nyota.
Mariam alimudu kuigiza na nyota wakubwa kama Cloud, Mlela na Hemed.

Saturday, November 5, 2011

LOST HOPE INAKUJA..

BAADA ya kufanya vizuri katika filamu ya Blue Monday, muandaaji wa filamu hiyo, Abui Ahmed amewataka wapenzi wa filamu nchini kukaa tayari kwa ujio wa filamu mpya itakayokwenda kwa jina la  Lost Hope.

Ahmed ambaye pia  ni   Mkurugenzi wa Abui Production alisema kuwa filamu hiyo   iliyobeba ujumbe mzito wa familia na mapenzi kwa ujumla itakuwa sokoni mapema wiki ijayo.

“Filamu hii imebeba ujumbe mzito ambao nina uhakika utaelimisha jamii kwa ujumla na vilevile kumfanya kila mtu ajifunze kwa nafasi yake kutokana na kile kilichopo ndani ya filamu hii”alisema Ahmed.

Aliwataja wasanii walioshiriki katika filamu hiyo ni pamoja na Michael Philipo (Kojack) ,Nila Sultani (Jasmin) ambao ni wahusika wakuu na wengine ni Flora Mvungi,Mainda,Abdala Agosi, Badi pamoja na wengine wengi.

Abui Production  imehusika kuandaa filamu mbalimbali zikiwemo Zindiko,Tension of Love na Blue Monday ambayo inafanya vizuri katika soko la filamu nchini.

WAZEE WATATU VICHWA KATIKA TASNIA YA FILAMU KWA SASA...

KILA unapokutana na filamu yoyote ya Bongo, si rahisi kuzikosa sura hizi katika filamu hizo. Sura hizo ni za wasanii Hashim Kambi �Ramsey�, Charles Magali �Mzee Magali� na Ahmed Olotu �Mzee Chilo�.

Wakongwe hao hata kama watakuwa wameigiza japo kwa ufupi, lakini ndiyo wasanii wa kiume wanaoongoza katika kushiriki filamu nyingi za Bongo, ukiachilia Ray na Kanumba, ambayo hufanya kazi zao wenyewe. 

Uchunguzi unaonesha kuwa wasanii hao wamekuwa wakihusishwa katika filamu mbalimbali kutokana na uhusika wao, kwa maana watu wenye mwonekano wa kiutu uzima.

Pengine kama wangekuwa wanalipwa vizuri, ni wazi tungezungumza mambo mengine kwa sasa. Walistahili kuwa matajiri wa kutupwa. 

Lakini kwa bahati mbaya, Bongo, pamekuwa na mfumo usioeleweka. Hollywood, Bollywood na kwingineko wasanii kama hawa hutengeneza fedha nyingi kwa kila hatua, kuanzia mikataba ya ushiriki wa filamu husika, maonyesho ya filamu katika majumba ya sinema na uuzaji wa filamu katika DVD. 


Friday, November 4, 2011

TBC KUANZA KUONESHA CHINA-SWAHILI SOAP OPERA NOVEMBER HII...


Shirika la utangazaji la Tanzania TBC leo limetangaza uzinguzi rasmi wa tamthiliya ya kichina mbayo imetafsiriwa kwa Kiswahili na wantanzania waishio nchini humo na wafanyakazi wa kituo cha radio cha China radio International (CRI).
Tamthiliya hiyo ambayo itajulikana kwa jina la ‘Dou Dou na Visa vya Mama Wakwe zake’ itaanza kuonyeswa rasmi TBC 1 tarehe 23 mwezi huu wa kumi na moja.
Akizungumza na waandishi wa habari mkurugenzi mkuu wa TBC Mr Clemence Mshana alisema kuwa lengo kubwa la tamthiliya hiyo ni kuonyesha jinsi lugha adhimu ya Kiswahili inavyoweza kutumika moja kwa moja bila kuweka tafsiri za maandishi katika filamu au tamthiliya kuelezea utamaduni wa mataifa mengine.
Alisema kuwa kupita tamthiliya hii, ambayo inatarajiwa kuzinduliwa rasmi wiki ya mwisho wa mwezi huu wa November, itawasaidia wasanii wa Tanzania ninsi wanavyoweza kutengeneza tamthiliya nzuri zenye ubora na zikaweza kuuzwa nchi za nje na hivyo kukuza matumizi ya lugha ya Kiswahili nje ya Tanzania.
“ Vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kuitangaza lugha ya Kiswahili kwa kueleza jamii kuwa inatosheleza katika Nyanja mbali mbali za maisha ya binadamu bila kujali taifa lake,” alisema.






Friday, October 28, 2011

WASAMBAZAJI WANAZINGUA ASEMA ROSE...


MTAYARISHAJI na mwigizaji nyota wa filamu wa Bongo, Rose Ndauka, amesema kuwa filamu yake ya Diary imeshindwa kuingia sokoni mapema kwa sababu ya matatizo ya usambazaji.

Badala yake ameamua kuigiza filamu ya Ruben n� Angel wakati akijaribu kumtafuta msambazaji anayefaa.

Filamu ya Diary ilikuwa itoke mapema kabla ya filamu ya Ruben n� Angel, lakini kutokana na matatizo ya usambazaji ameamua kusitisha zoezi hilo. 


Mwanadada huyu ambaye anamiliki kampuni yake inayojulikana kwa jina la Rose Ndauka Entertainment, anatayarisha filamu zake mwenyewe pia na kushiriki filamu nyingine.

�Nilikuwa nimewaahidi wapenzi wa kazi zangu kuwa filamu ya Diary inatoka mwezi huu, na watu walikuwa wanasubiri kwa hamu itoke, lakini ratiba imebadilika badala yake nimetoa filamu nyingine ya Ruben n� Angel,� alisema Ndauka.

Filamu ya Ruben wameshiriki wasanii kama Khaleed Tajiri, Irene James, Ndauka na wasanii wengine filamu hiyo ipo mtaani ikiendelea kuuzwa.


Saturday, October 15, 2011

Aunt Ezekiel asema hajafungiwa...


BAADA ya uvumi wa kufungiwa kwa mwigizaji Aunty Ezekiel kuenea , mwenyewe amefunguka na kusema kuwa huo ni uvumi tu ambao hata yeye amekuwa akiusikia tu bila kujua chanzo chake.

“Sijui nani aliyeanzisha habari hizi, lakini mimi sijafungiwa na sasa ninapozungumza na wewe nipo mzigoni nikiandaa filamu yangu mpya ambayo nitaiingiza sokoni muda si mrefu,” alisema Aunty.

Aunty amesema filamu yake hiyo itaitwa House Boy and House Boy na itakuwa ikielezea maisha ya kila siku ya wafanyakazi wa ndani.

Mwenyekiti wa Bongo Movie, Jacob Steven amesema umoja wao huo haukumfungia kuigiza, bali asingeruhusiw akufanya kazi na msanii yoyote wa umoja huo.

Hata hivyo alisema Aunty ameshajirekebisha kwahiyo anaweza kuendelea na kazi kama kawaida.

Hata hivyo kufungiwa kwa Aunty kuna leta utata kutokana na waigizaji kuwa na vyama mbalimbali ambvyo mpaka sasa hakijukani kipi chenye nguvu ya kuweza kumfungia msanii.

Kipindi cha nyuma kulikuwa na shirikisho la wasanii wa filamu TAFF ambalo inasemekana liliundwa baada ya serikali kuamuru uundwe umoja utakaowawakilisha kwenye shughuli mbalimbali.

Baadae ukaundwa umoja huu uitwao Bongo Movie ambao wasanii wengine wanadai kutoutambua kutokana na mazingira yake nakusema kuwa umeundwa kwaajili ya maslahi ya wasanii wachache.

Saturday, October 1, 2011

Kitu Kipya kabisa kwenye game...

 
RATIFA MTOBI (TANITA)
Amezaliwa Tanga miaka kumi na tisa iliyopita. Mwigizaji wa Tuesday Entertainment. anapendelea kuogelea na riadha.
 
Ni Mwanadada Chipukizi ambaye yuko pamoja na actors wengine katika tamthiliya ya Millosis inayorushwa TBC1 kutoka kwa Director Tuesday Kihangala.

Shirley; Nyota anayetikisa kwenye tamthiliya ya Millosiss...


Jina halisi la chipukizi huyo ni Celina Victor, lakini mashabiki wa filamu wanamfahamu kwa 'Shirley', msanii ambaye aliweza kuonesha uwezo katika tamthilia ya 'Jumba la Dhahabu'.
Nyota huyo anajitahidi kusaka umaarufu lakini bado ana changamoto nyingi za kucheza filamu ambazo zitazidi kumweka juu kama ilivyo kwa The Sandy kazi ambayo inafanya vizuri.


Katika mawasiliano na mdada huyu na blog hii kupitia mtandao wa Facebook Shirley alifunguka na kutaja kazi mbali mbali ambazo aliwahi kufanya na bado zingine zinazotarajiwa kutoka hivi karibuni.


“Kazi nilizowahi kucheza ni jumba la dhahabu (series) + movies nilizoshiriki kuna mboni yang ya kina sajuki, zingine indecency, jasho la kifo, hostell na XXL ambayo haijatoka bado. Also nipo kwny drama inaitwa millosis inaruka Tbc kwa sasa,” alisema Shirley.