BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Sunday, May 6, 2012

Jamani msaidieni huyu muigizaji

   MUIGIZAJI maarufu wa filamu nchini Tanzania, Wastara Juma, amesema kuwa alikataa kuwekwa mapumziko (bed rest) kwa wakati wote wa ujauzito wake kutokana na kumuuguza mume wake Juma Kilowoko maarufu Sajuki ambaye anasumbuliwa na matatizo ya uvimbe tumboni.

Wastara, ambaye hivi sasa ana mtoto mwenye umri wa miezi miwili, anasema matatizo ya afya yake kwa wakati huo ndiyo yaliyosababisha madaktari kutaka alazwe hospitalini.

"Tangu mume wangu alipokuwa anaumwa nilikuwa nahangaika naye huku na kule kumtibia, lakini baadaye nilikuja kugundua kuwa nilikuwa mjamzito. Vipimo vya hospitalini vikaonyesha nina matatizo ya sukari ya mimba, presha pamoja na mguu wangu ulikuwa mbovu," anasema.

Anasema kutokana na ugonjwa wa mume wake, hakutaka kukubaliana na madaktari kuhusu kulazwa kwa kipindi chote atakachokuwa mjamzito na badala yake aliendelea kumuuguza mumewe.

"Nilikataa kulazwa, kwa kweli, japokuwa nilihatarisha maisha yangu, niliendelea kumuuguza na kuhangaika huku na kule, wakati huo mimba nayo ilizidi kukua. Kwa bahati mbaya ilipofikia miezi nane na wiki moja madaktari waliniamuru nifanyiwe oparesheni kwani nisingeweza kuzaa kwa njia ya kawaida, na Machi 5 mwaka huu ndipo nilipompata mtoto wangu," anasema.

Hata hivyo, anabainisha kuwa ilimlazimu kusimama kazi zake zote ili aweze kumuuguza Sajuki.

"Kutokana na ugonjwa wa mume wangu, ilinilazimu kuacha kazi, kuacha kuigiza pamoja na kusimama kwa kazi zangu binafsi ili niweze kupata wasaa wa kumuuguza mume wangu.

"Nilifunga ofisi na vitu vyangu vyote zikiwemo mashine tunazozitumia katika kazi, nilihamishia nyumbani, vitu ambavyo viliibiwa siku moja baada ya mimi kujifungua," anasema.

Changamoto anazokutana nazo Wastara ni kubwa. Anasema kuwa anahitaji zaidi ya Sh 25 milioni pesa za Kitanzania ili kuweza kuokoa maisha ya Sajuki ambaye kwa sasa anatumia dawa zenye thamani ya Dola 1,000 kwa wiki moja alizozinunua nchini India.

"Nahitaji Sh 25 milioni ili Sajuki aweze kupona, kwani kwa sasa anatumia dawa ambazo alizipata nchini India tulizonunua dola 8,000, lakini zikiisha anatakiwa kurudi tena ili akapewe nyingine na matibabu zaidi, sina pesa na vifaa vyangu vyote niliibiwa.�

Anasema na kuongeza: "Tuna maisha ya kawaida kama watu wengine, lakini ninavyoomba msaada watu wananishangaa, kwa kuwa wanatuona tunacheza filamu katika majumba ya kifahari wanadhani ndiyo maisha yetu, siyo hivyo, mimi nafanya hivi ili mume wangu apone.�

Wastara aliweka bayana nambari za akaunti yake ya benki kwa wale wenye mapenzi mema wanaotaka kumsaidia kuwa ni Wastara Juma, Akaunti Namba 050000003047 iliyopo Akiba Commercial Bank.

�Tatizo kubwa zaidi linalomsumbua Sajuki lilikuwa ni kukauka kwa damu ambapo ilifikia hatua anakuwa na damu 5 mpaka 4, hali ambayo ni hatari, lakini nashkuru Mungu kwani ameanza kutumia dawa na kwa sasa ana damu 9,� anaeleza Wastara.

Anasema kuwa, katika maisha yao wamekutana na mitihani mingi ikiwemo yeye kukatwa mguu siku chache kabla ya ndoa yake na kwa sasa kuugua kwa wote wawili kwa wakati mmoja.


Ramsey yuko juu sana


RAMSEY Nouah ametamka hadharani kwamba hakuna jinsi utakavyoitaja fani ya filamu Nigeria uache kumgusa, lakini anafikiria kukaa pembeni kabla hajachuja.

Msanii huyo alisema; "Najua mashabiki wangu watataka kuniona siku zote kwenye runinga, lakini kama ilivyo kawaida, lazima ung'atuke ukiwa bado unapendwa.

Najua nimefanya mambo makubwa sana kwenye hii tasnia, hakuna jinsi utakavyotaja jina Nollywood uache kunitaja."

"Nitakuwa naigiza hapa na pale lakini kidogo sana, nitakuwa nafanya sana mambo ya uongozaji, kuna kipindi kirefu sasa sijaonekana kwenye runinga kwa sababu sitaki kufanya kazi ambazo hazina viwango.

"Sitaki kufanya kazi ilimradi, nataka kuhusishwa na filamu zenye viwango na heshima kwenye hii fani."

Baba azuia mali za Kanumba mahakamani

MZEE Charles Kanumba ambaye ni baba mzazi wa marehemu Steven Kanumba, amezuia kuuzwa kwa mali zilizoachwa na mkali huyo wa filamu nchini.

Mzee Kanumba anataka kitu chochote kisiuzwe mpaka mahakama itakapoamua mrithi wa mali hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini hapa, mzazi huyo alisema kuwa ameamua kutoa tamko hilo baada ya kusikia mzazi mwenzake, Flora Mutegoa, ameanza kuuza mali zilizoachwa na marehemu Kanumba kabla ya mahakama kutoa uamuzi.

Mali hizo ni pamoja na gari la kifahari lenye thamani ya Sh 75 milioni.

�Nimesikitishwa na kitendo cha kusikia mama wa Kanumba ameanza kuuza mali za marehemu, nimeamua kutoa tamko kwa Watanzania wote kuwa wasinunue mali yoyote ya marehemu mpaka mahakama itakapotoa uamuzi," Mzee Kanumba alisema.

"Sisi wazazi wote tuna haki kwa sababu ndiyo tuliomzaa, mtu yeyote atakayenunua mali hiyo atakuwa ametenda kosa la jinai."

Pia alisema ametoa kauli hiyo kufuatia kupata taarifa kuwa kuna wasanii ndiyo madalali wa kuuza mali hizo za Kanumba.

Mzee huyo pia ametoa wito kwa mzazi mwenzake kuacha kusikiliza watu wanaopotosha kuwa kifo cha mtoto wao kilitokana na imani za ushirikina.

�Kuna kijana mmoja ambaye ni mtoto wa dada yangu (anamtaja jina) nimesikia anamdanganya kuwa mtoto wetu karogwa, mara amechukuliwa msukule asimsikilize huyo," aliongeza Mzee Kanumba.
"Tuliwahi kumwita ili kumhoji lakini hakutokea."

Kanumba alfariki dunia Aprili 7 mwaka huu katika kifo kilichozua utata. Msanii Lulu yuko rumande akiendelea na kesi inayomtuhumu kuhusika na kifo hicho.

Wednesday, May 2, 2012

KENYELA AMESEMA ANAFUATILIA BASTOLA ILIYOKUWA IKIMILIKIWA NA KANUMBA

Bastola ambayo inadaiwa ilikuwa ikitumiwa kihalali na staa wa filamu barani Afrika, Steven Charles Kanumba, inasakwa na Jeshi la Polisi Tanzania.Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, Dar es Salaam, ACP Charles Kenyela amesema kuwa anafuatilia kumbukumbu za silaha hiyo, kwani haijarejeshwa kwenye jeshi lake.Kenyela alisema juzi kuwa anafuatilia umiliki wa Kanumba juu ya umiliki huo na baada ya hapo, jeshi la polisi litawahoji ndugu“Bastola ni mali ya serikali. Kuna hatua ambazo hufuata mpaka mtu aruhusiwe kumiliki bastola,” alisema Kenyela na kuongeza:Endapo mmiliki halali wa silaha hiyo atafariki dunia, ndugu zake lazima waikabidhi kwa jeshi la polisi na baada ya hapo, kama kuna ndugu anataka aimiliki, inabidi afanye maombi upya na atakapokidhi vigezo ndiyo anaruhusiwa.“Kutokana na hali hiyo, bastola ya Kanumba lazima irudi kwetu haraka na kama kuna ndugu yake yeyote anataka kuimiliki, itabidi awasilishe maombi.”Kenyela aliongeza kuwa hivi sasa anafuatilia kumbukumbu za jeshi la polisi ili awe na uhakika kama kweli msanii huyo alikuwa anamiliki silaha hiyo.“Tukithibitisha tutawahoji ndugu zake pamoja na wengine wanaohusika ili tuwe na taarifa za hiyo silaha. Ila kwa sasa tunafanyia kazi taarifa hizi kwa kupitia kumbukumbu za jeshi,” alisema.Kenyela alitoa ufafanuzi huo baada ya kuulizwa na ripota wetu kama jeshi lake limeshapokea bastola ambayo alikuwa anaitumia Kanumba enzi za uhai wake.
NDUGU WANASEMAJE?
Mama mzazi wa Kanumba, Flora Mtegoa, aliulizwa na paparazi wetu kuhusu bastola inayodaiwa kutumiwa na mwanaye alipokuwa hai, na haya ni majibu yake:“Sijaiona hiyo bastola humu ndani tangu nimefika hapa. Sijui ipo wapi na sijui kama kweli Kanumba alikuwa anamiliki hiyo silaha.“Najua sheria za silaha hiyo, kwa hiyo ingekuwepo ningeiwasilisha polisi haraka. Baba yangu alikuwa na silaha hiyo, alipofariki dunia tuliikabidhi kwa jeshi la polisi.”
NANI ANAJUA ILIPO?
Taarifa zinaonesha kuwa mdogo wa Kanumba, Seth Bosco alikuwa karibu zaidi na marehemu lakini kwa sababu umiliki wa silaha hiyo ni siri, siyo rahisi kujua ilipo.Mtu mwingine ambaye alikuwa karibu na marehemu mpaka nyakati za mwisho za uhai wake, kama ripoti zinavyoonesha ni muigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’, ingawa naye inawezekana akawa hajui kutokana na unyeti wa silaha yenyewe.
BASTOLA NA KANUMBA
Akiwa hai, Kanumba aliwahi kuripotiwa mara kadhaa kumiliki silaha hiyo, japo haikufafanuliwa kama ni kihalali au batili.Kanumba aliripotiwa kwa mara ya kwanza kumiliki bastola miaka minne iliyopita, akidaiwa kuichomoa baada ya kuvamiwa na kundi la watu aliohisi wanataka kumteka.Licha ya stori hiyo kuandikwa gazetini na nyingine ambazo zilimhusisha na umiliki wa bastola, bado Kanumba hakuwahi kufafanua chochote kuhusu silaha hiyo.
IPO WAPI?
1. Je, aliiacha sehemu ambayo hakuna mtu ameweza kupafikia?
2. Aliirejesha kabla mauti hayajamkuta ndiyo maana haionekani?
3. Je, Kuna mtu aliiwahi baada ya kifo chake akiona ni dili?
Kanumba alifariki dunia Aprili 7 na kuzikwa Aprili 10, 2012 kwenye Makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam. wa msanii huyo kuhusu kurejesha bastola hiyo jeshini.
Martin Lukanga
Tin White.
MCHEKESHAJI mahiri wa vichekesho Swahiliwood Martin Lukanga ‘ Tin White’ ameamua kuachana na komedi za kushirikishwa bali ni kuandaa komedi zake mwenyewe kama ambavyo ufanya wasanii wenzake na kuuza kwa wasambazaji, akiongea na Jukwaa la filamu Tin White amesema ameshiriki Komedi nyingi lakini hapati nafasi nzuri ya kuwakilisha mawazo yake.
“Nimetumwa sana na mimi zamu yangu kuwatuma vijana wangu nimetayarisha Komedi yangu kali inayokwenda kwa jina la Mr. Lover ni hadthi nzuri ina mtiririko mzuri kama zilivyo filamu, ni komedi ya kipekee mtu anacheka humo kwa ajili ya hadithi na si vinginevyo, nimeanza na spidi yangu haina mwisho,”anasema Tin White.
Kama ilivyo tabia ya wachekeshaji ya kujikusanya na kushiriki kwa wingi katika filamu moja na humu namo wapo wachekeshaji kama Bambo, Kingwendu, Ringo, Tin White mwenyewe, Mtanga, alipoulizwa kwani nini wachekeshaji wengi ujazana katika filamu moja alisema kuwa si wao bali ni fikra finyu za wasambazaji wanaamini
kuwa wachekeshaji wengi ndio kuuza, lakini yeye anaamini kuwa hata msanii mmoja tu anatosha.

CLOUD KATIKA HARAKATI ZA UZINDUZI WA TOBA

 Cloud.
MWIGIZAJI na Mtayarishaji wa filamu Swahiliwood Issa Mussa ‘Cloud 112’ yupo katika maandalizi ya kuzindua filamu yake mpya inayokwenda kwa jina la Toba uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Salama uliopo Zanzibar tarehe 18/05/2012 siku ya Ijumaa.
Cloud anakuwa ni msanii wa kwanza kwa mwaka huu kufanya tamasha kwa ajili ya uzinduzi wa filamu yake hiyo ya Toba baada ya utaratibu huo kusimama kwa muda mrefu kidogo, kwani siku hizi filamu zikitengenezwa zinaingizwa sokoni moja kwa moja bila kufanyiwa uzinduzi.
Filamu ya Toba imeshirikisha wasanii nyota kama Suleiman Barafu, chiki, Sandra, Eshe, Bi. Hindu na wasanii wengine wakali katika tasnia ya filamu Swahiliwood hongera kwa Cloud 112 kwa kufanya uzinduzi wa filamu yake

Tuesday, April 24, 2012

JE WASANII WA FILAMU TZ WANATENGENEZA FILAMU AMBAZO WATU WANAZIHITAJI?.

''The most important quality in a filmmaker is… having a balance between creativity, understanding the tools of the trade, and having a keen business sense.''
Whereas many filmmakers have an unbridled creative passion for telling stories and know the tools of their trade, few understand how to create and package content that distributors and audiences want to see. 
Pastor Myamba

TINO AMSHUKIA STEVE NYERERE...

 MWIGIZAJI Nyota wa filamu na mtayarishaji wa filamu Swahiliwood, Hisani Muya Tino, amemshukia mchekeshaji na mwigizaji wa filamu Steven Mangere Steve Nyerere kwa kusema kuwa ni tatizo na mgombanishi wa wasanii wakubwa.

�Huyu Steve Nyerere ni mtu mbaya sana kwa sasa katika tasnia ya filamu, siku za nyuma wasanii walikuwa na ushirikiano wa kweli bila kuwa na makundi ambayo yapo sasa, na kila tatizo ukifuatilia utaambiwa Steve.

"Nimeshangaa sana hata msiba wa Kanumba haujakwisha tayari ameshatengeneza zengwe akidai kuwa mimi nimekaa na mama wa marehemu eti kumponda mdogo wake Seth asipewe kampuni ya Kanumba, hawezi kuongoza nipewe mimi,� anasema Tino.

Tino alisema kuwa Steve Nyerere alimpigia simu kwa kumlaumu kuwa Bongo Movie wapo Leaders wakiwa katika kikao cha kumjadili yeye kwa kuingilia suala la marehemu wakati wao walikuwa wanataka kuisimamia kampuni hiyo kwa kumtumia Seth, lakini Tino anakuwa kikwazo jambo ambalo linawakera, lakini pia alisema anashangaa Steve kujiweka mbele wakati marehemu alijitoa katika kundi hilo.

�Huyu anatakiwa kujua kuwa mimi sijajuana na marehemu juzi, nimekuwa nikifanya naye kazi mbalimbali hata kabla ya kufariki aliniita akaniambia anahitaji tuendeleze mradi wa kuinua vipaji vya wasanii wachanga na kusema nizifuate (tape) mikanda tuliyorekodi kwa ajili ya usaili wa wasanii tuliowafanyia siku za nyuma,� alisema Tino.

Mwanaspoti ilimpigia simu Steve Nyerere ambaye alisema kuwa mambo hayo yalishapita na Tino waliongea naye yakaisha, sasa anashangaa kuyasikia tena yakiendelea bila sababu za msingi wakati yeye anaamini kuwa hayana faida yoyote.

�Jamani hayo mambo yamepita, tumwache marehemu apumzike kwa amani hakuna sababu ya kuendelea na malumbano yasiyotuingizia fedha na tusitafute umaarufu kupitia marehemu, tufanye kazi maisha yaendelee, kama kuna kosa kila mtu kajifunza kwa wakati wake,� alisema Steve.

Kufuatia kifo cha Steven Kanumba kumekuwa na maneno yanayoashiria shari na kuibuka makundi kwa wasanii na kuzua vikao kila kukicha, huku wakishindwa kupanga mikakati imara ya maendeleo yao.

Mawakili wanne kumtetea Lulu


JOPO la mawakili wanne maarufu nchini akiwamo Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHRAGG), Joaquine De Mello, wamejitokeza kumtetea msanii wa filamu, Elizabeth Michael Kimemeta Lulu anayetuhumiwa kuhusika na mauaji ya aliyekuwa msanii maarufu Steven Kanumba.

De-Mello ambaye pia aliwahi kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) na mshindi wa tuzo ya Mwanamke Jasiri Tanzania ya Martin Luther King, anaungana na wanasheria wengine ambao ni Kennedy Fungamtama, Peter Kibatala na Fulgence Massawe katika kumtetea Lulu mwenye umri wa miaka 17.

Fungamtama ambaye ndiye kiongozi wa jopo lao anakumbukwa kwa kuitetea kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans katika kesi dhidi ya Shirika la Umeme la Tanzania (Tanesco).
Katika kesi hiyo Dowans ilishinda na Tanesco iliamuliwa kuilipa Dowans zaidi ya Sh 94 bilioni kwa kuvunja mkataba kinyume cha sheria.

Kwa upande wake, Kibatala ambaye pia anamtetea kada wa Chadema, Fred Mpendazoe, katika kesi ya uchaguzi Jimbo la Segerea, pia ni Makamu wa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), wakati Massawe anatoka Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki za Binadamu (LHRC). 


Mawakili hao walijitokeza jana Jumatatu, mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Ritha Tarimo, kwa ajili ya kumtetea Lulu anayekabiliwa na kesi ya hiyo ya mauaji. Kesi hiyo ilikuja mahakamani hapo jana kwa ajili ya kutajwa.

Baada ya mawakili hao kujitambulisha kumtetea msanii huyo, Wakili Mwandamizi wa Serikali, Elizabeth Kaganda, alidai kuwa upelelezi wa kesi bado haujakamilika na kuiomba mahakama ipange tarehe nyingine.

Hakimu Tarimo aliiahirisha kesi hiyo hadi Mei 7, mwaka huu itakapokuja kwa ajili ya kutajwa.

Lulu alifikishwa mahakamani hapo saa 3:06 asubuhi kwa kutumia gari la Magereza lenye namba za usajili STK 4310 ambalo lilisindikizwa na gari mbili zenye usajili namba STK 4253 na STK 8901.

Alikuwa chini ya ulinzi mkali wa askari sita wa kike wa Jeshi la Magereza pamoja na askari mmoja wa kike wa Jeshi la Polisi.
Askari hao kwa kushirikiana na askari wa kiume wa Jeshi la Magereza zaidi ya sita walimwingiza msanii huyo mahakamani kwa ulinzi mkali kiasi kilichowafanya baadhi ya wapiga picha kushindwa kumwona.

Lulu ambaye alikuwa amevalia vazi la aina ya dira la rangi nyekundu, kutokana na kubanwa katikati ya askari hao wakati akiingizwa mahakamani, alianza kulia kitu ambacho kilimfanya Hakimu Tarimo kumpa pole na baadhi ya askari kumnyamazisha.

Kutokana na kujaa kwa watu mahakamani humo na wengine wakitaka kuzidi kuingia askari wa jeshi la Magereza walitumia nguvu kufunga mlango wa chumba cha mahakama hiyo na kuwezesha kesi hiyo kusikilizwa.

Baada ya kesi hiyo kumalizika, wakili Kaganda, aliiomba mahakama iamuru watu wote watoke nje ili mtuhumiwa aweze kupitishwa kwa sababu walikuwa wamefunga njia.

Kufuatia ombi hilo, hakimu Tarimo aliwaamuru askari kusafisha njia ili waweze kumpitisha msanii huyo kwa kile alichosema kuwa Lulu bado ni mtuhumiwa na anaweza kuumizwa.

"Askari safisheni njia ili mtuhumiwa aweze kupita kwa sababu yeye bado ni mtuhumiwa anaweza kuumizwa,"alisisitiza Hakimu Tarimo.

Baada ya kutolewa kwa amri hiyo askari walitimiza wajibu wao na muda mfupi njia ilipatikana na msanii huyo kutolewa mahakamani hapo chini ya ulinzi mkali.

Hiyo ilikuwa mara ya pili kwa Lulu kufikishwa mahakamani hapo. Mara ya kwanza ilikuwa Aprili 10 mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi, Augustina Mmbando.

Wakati akifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza, polisi walitumia mbinu za kikachero kuwapiga chenga waandishi ambao wengi walikwenda mahakama ya Kinondoni wakidhani mtuhumiwa huyo angefikishwa hapo, lakini akapandishwa Kisutu na kusomewa mashtaka katika kipindi kisichozidi dakika kumi kisha kupelekwa rumande.

Pia tofauti na matarajio, siku hiyo polisi hawakuwa wametumia magari yenye ving'ora na ulinzi wa kutisha kama ilivyotarajiwa bali walitumia magari mawili madogo na alipofika mahakamani hapo, alisomewa shitaka hilo na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Elizabeth Kaganda.

Kaganda akimsomea hati ya mashtaka Lulu, alidai kuwa Aprili 7, mwaka huu, maeneo ya Sinza Vatican katika wilaya ya Kinondoni, Lulu alimuua, Steven Kanumba.

Baada ya kumaliza kusoma shtaka hilo, Kaganda alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika hata hivyo, Lulu hakuruhusiwa kujibu chochote kwa sababu Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina uwezo wa kuisikiliza kesi hiyo hadi Mahakama Kuu.

Hakimu Mmbando aliamuru Lulu apelekwe rumande katika Gereza la Segerea kwa sababu shtaka linalomkabili ni moja kati ya mashtaka yasiyo na dhamana.

Kanumba alifariki dunia usiku wa Aprili 7 kwa kile kilichodaiwa kuwa ni baada ya ugomvi baina yake na Lulu. Alizikwa kwenye makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Wednesday, April 18, 2012

SHIRIKISHO LA FILAMU LAMSHUKURU RAIS JK

Rais wa TAFF, Simon Mwakifwamba, akitoa shukrani wakati akiongea na vyombo vya habari.