BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Saturday, December 29, 2012

Miaka 51 baada ya uhuru wawekezaji wanaongezeka tuu

 Hapa sio Mkoani Simiyu bali ni Dar wawekezaji kibao lakini maisha bado kitendawili... kwa kiasi mji unakua atiii!!!



Tuesday, December 18, 2012

Vodacom Family Day..

 Meneja wa  matangazo wa kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Bw Nicholas Machugu (Kushoto) akikabidhi kombe kwa nahodha wa timu ya wa mpira wa miguu kutoka idara ya biashara kwa nahodha wa timu ya idara ya biashara katika tamasha la Vodacom Family day lililofanyika katika viwanja vya kunduchi Beach Hotel lililofanyika Jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Waimbaji wa Skylight Band wakitumbuiza katika tamasha la Vodacom Family Day, tamasha lililo fanyika katika viwanja wa Kunduchi Beach Hotel mwishoni mwa wiki.

Monday, December 17, 2012

Wafanyakazi wa Vodacom watoa msaada kwa kituo cha yatima Friend of Don Bosco Kimara

 wafanyakazi wa mtandao wa simu ya mkononi Vodacom Tanzania kitengo cha Customer care wakitoa msaada wa vitu mbali mbali kama vyakula, vitanda, magodoro vyenye thamani ya Sh6 million.

Saturday, November 24, 2012

Msanii wa Filamu Tanzania John Maganga afariki

John Maganga
Marehemu John Maganga mwigizaji wa filamu enzi za uhai wake.
KATIKA Tasnia ya filamu Swahiliwood wiki hii imekubwa na simanzi baada ya wasanii wake kuaga Dunia siku ya jana msanii mahiri wa maigizo Halid Mohamed ‘Mlopelo’ alizikwa na leo hii tasnia hiyo imekubwa na msiba mwingine mkubwa baada ya John Maganga kufariki katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
John Maganga
Marehemu John Maganga akiwa na msanii mwenzake katika moja ya sene.
John Maganga
Marehemu John Maganga enzi za uhai wake.
Taarifa za awali zinasema kuwa marehemu John amefikwa na mauti baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa tumbo, ni huzuni kwa wasanii na wadau wa tasnia hiyo ya filamu kwani wengi wamedai kuwa msanii huyo ni jana tu walikuwa naye katika matembezi na leo hatunaye tena.
Taarifa zaidi kuhusu mazishi mtazipata hapa hapa bado timu ya FC inajaribu kufuatilia kwa karibu na kuwataarifu, Bwana Mungu alitoa na ametwaha jina lake lihimidiwe.

Friday, October 26, 2012

KITU KIPYA KUTOKA D PRODUCTION "MAGIC MONEY"


""zimebaki sikuchache kuingia sokoni noma...""
ni kauli ya msanii wa filamu Daudi Michael katika wall yake ya facebook akiongelea ujio wa fila mu yake mpya ijulikanayo kama Magic Money iliyoandaliwa na D Production na wasambazaji ni Pili Pili entertainment.... JIPATIE NAKALA YAKO COMING SOOOOON!!!!! BIGUP D PROD....

Sunday, September 2, 2012

TSJ Bash ilivyo wabamba wanafunzi...

 Hao ni washiriki mashindano ya kumtafuta Miss na Mr Tsj kwa mwaka 2012/2013 yaliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Mbalamwezi Beach na hapo wakiwa wanaingia katika steji.
 Wakiwa katika katika steji wakiwa burudisha wanafunzi wenzao kutoka chuo cha uandishi habari kiitwacho Tsj kilichopo Ilala-Sharifu shamba pamoja na Mkuu wao wa chuo cha TSJ akiwa bega kwabega akiongozana na mgeni Rasmi kutoka kitengo cha Haki za kibinaadamu{LHRC}
                                            Washiriki wa MISS na MR TSJ wakiwa katika picha ya pamoja hapo
 Picha ya pamoja wakiwepo washindi wa MISS na MR TSJ kwa mwaka huu, wakiwa pamoja  na mkuu wa chuo upande wa kulia aliyevaa nguo ya rangi nyeupe Bi Carolyne Setumbi kushoto Rais wa serikali ya wanafunzi ya TISJOSO Bi Frida Matinya.
 Picha ya pamoja wakiwepo washindi wa MISS na MR TSJ kwa mwaka huu, wakiwa pamoja  na mkuu wa chuo upande wa kulia aliyevaa nguo ya rangi nyeupe Bi Carolyne Setumbi kushoto Rais wa serikali ya wanafunzi ya TISJOSO Bi Frida Matinya.pamoja na Miss na Mr ambao wamewavalisha Taji washindi wa mwaka huu.

Sunday, August 12, 2012

TAMASHA LA DINI "LOVE TANZANIA" LILIVYOTIA FORA VIWANJA VYA JANGWANI JIJI DAR.


Pichani Juu na Chini ni Umati wa Watanzania uliofurika kwenye Tamasha la Dini lililopewa jina la LOVE TANZANIA linaloendelea katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam likiongozwa na Askofu Andrew Palau kutoka Marekani.
Vijana walioongoza na Askofu Andrew Palau wakitoa burudani na mafundisho ya dini kwa njia muziki.
Wana Dar es Salaam wakiendelea…

Saturday, August 11, 2012

MRITHI WA TAJI LA MISS &MR TSJ KUJULIKANA AUGUST 25 MWAKA HUU





SERIKALI  ya wanafunzi ya chuo cha uandishi wa habari cha Time School of Journalism (TSJ) inatarajia kuwapata wawakilishi wapya wa taji la Miss na Mr TSJ katika sherehe za ‘Bash’  ambazo zimelenga kuwakaribisha wanafunzi wapya wa mwaka wa kwanza katika chuo hicho.
Sherehe hizo ambazo zinatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi August tarehe 25 zitafanyika katika uwanja wa Mwalamwezi Beach, na itasindikizwa na wasanii mabli mbali wa muziki wa Bongo flava.
Akizungumza na gazeti hili, Rais wa chuo hicho Bi Frida Matinya alisema kuwa sherehe hizo ni moja ya utaratibu waliojiwekea katika kuwapokea wanafunzi wapya ambao ni wameingia chuoni hapo kuchukua kozi mabli mbali.
Alisema kuwa katika sherehe hizo ambazo zitashereheshwa na michezo mbali mbali ikiwa ni pamoja na maonyesho ya mavazi, Mr na Miss TSJ, Kuimba, kuvuta kamba, kuogelea na michezo mingine mingi ya baharini.
“Lengo la sherehe hizo ni kuwa kawaweka karibu wanafunzi wageni na pia kufahamiana pamoja na kujenga mazingira rafiki kwa wanafunzi wote pia kuwapa burudani pia kujijenga kisaikolojia kwani michezo hujenga, kujumuika pamoja katika hafla hii itatuwezesha kuwa na ushirikiano wa kutosha,” alisema.
MWISHO.


TAFF YATOA TAMKO JUU YA MAHARAMIA WA FILAMU TANZANIA

 
SHIRIKISHO la Filamu nchini(TAFF) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) pamoja Kampuni za usambazaji wa filamu na kazi za wasanii ‘wameapa’ kupambana na maharamia wote wa kazi hizo ili kulinda maslahi ya wasanii.
Wakizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam jana, umoja huo kwa pamoja ulisema umefika wakati tatizo la wizi wa kazi za wasanii lishughulikiwe kikamilifu ili kuzima mianya yote ambayo ni kero kwa muda mrefu.
Rais wa Shirikisho hilo Simon Mwakifwamba, mbali na mikakati hiyo pia aliiomba Serikali kutekeleza ahadi yake ya kuwasaidia wasanii kwa kupambana na maharamia hao aliodai kuwa wapo kila pembe ya nchi hii huku wakijiamini kwa kuendelea na kazi hiyo.
“Umefika wakati kwa Serikali kusikia kilio hiki cha wasanii na kuweka mbinu kali zitakazosaidia kuokoa maisha ya wasanii wanaoendelea kuwa masikini kila kukicha kutokana na uwepo wa watu wachache wanaoiba kazi zao”
“Tuna imani kuwa kama kazi za wasanii zitasimamiwa vizuri, tutaweza kuongeza pato la Taifa kwa kiwango kikubwa ikizingatiwa kuwa sanaa hii kwa sasa hapa nchini imeonyesha mafanikio isipokuwa kuna watu wachache ndiyo wananufaika nayo” alisema Mwakifwamba.
Naye Mwenyekiti wa Bongomuvi Jacobo Steven ‘JB’ alisema sanaa inaweza kuwa na nafasi ya tatu kwa kuchangia pato la Taifa ukiacha pato linalochangiwa na sekta za madini maliasili pamoja na utalii.
Alisema Serikali inapswa kuonyesha makali yake kwa kuwakamata wahusika wote wa wizi wa kazi hizo ili kuendeleza nguvu za wasanii wa hapa nchini walioamua kujitoa mughanga kufanya kazi zao.
Kwa upande wake Meneja usimamizi kutoka TRA Msafiri Ndimbo alisema Mamlaka hiyo imejipanga kudhibiti wizi wa kazi hizo kuanzia Januari Mwakani hasa baada ya Serikali kupitia Bunge lake kukubaliana kuweka mikakati ya kupamba na suala hilo. 
Ambapo wasanii na wasambazaji wa kazi zao wameungana pamoja kwa ajili ya kuhakikisha kazi zao zinakwenda kwa haki ili wasanii na kazi zao

Sunday, June 3, 2012

AMREF Wazindua kampeni haki ya fya ya uzazi kwa vijana

 Keisha aikuzungmza na mmoja wa waelimisha rika ktk viwanja vya  Sinza darajani
 meya wa kndoni yusuph Mwenda na Meshak toka amrefu wakifuatili kwa makini
 wana acrobatic wakifanya vitu vyao uwanjani.
 duh... unamfahamu huyu... nimemkubali sana kwa kazi hii
 jingine hilo
na hii...

Monday, May 28, 2012

Serikali yataka maombi ya uchunguzi wa umri wa Lulu yatupwe


UPANDE wa mashtaka katika kesi ya mauaji inayomkabili msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu ambaye anakabiliwa na kesi ya mauaji ya msanii mwenzake Steven Kanumba umepinga maombi yaliyowasilishwa Mahakama Kuu kuhusu umri wa mshtakiwa huyo na kuiomba mahakama hiyo iyatupilie mbali.

Pingamizi hilo la awali liliwasilishwa mahakamani hapo jana na mawakili wa upande wa mashtaka Elizabeth Kaganda na Shadrack Kimaro mbele ya Jaji Dk Fauz Twaib wakati wa kusikilizwa maombi hayo.
Akiwasilisha pingamizi hilo, wakili Kimaro alidai kuwa maombi hayo yamewasilishwa mahakamani hapo kinyume cha sheria.

Alidai kuwa hata vifungu vya sheria namba 120 (ii) na 113 (i) na (ii) vya sheria ya mtoto ya mwaka 2009 ambavyo upande wa utetezi umevitumia kuwasilisha maombi hayo haviipi mamlaka mahakama hiyo kuweza kusikiliza maombi hayo.

“Namna walivyowasilisha maombi yao na sababu walizozitaja hazitoshi kuiruhusu mahakama hii kusikiliza maombi yao,”alidai Kimaro na kuongeza kuwa:

“Ni kweli kwamba mahakama hii ina uwezo wa kusikiliza suala la umri, lakini namna upande wa utetezi walivyowasilisha maombi yao hakuiwezeshi mahakama hii kuyasikiliza,”alidai.

Kimaro alidai kuwa mojawapo ya kielelezo kilichowasilishwa na upande wa utetezi wakidai ni uamuzi uliotolewa na mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu si uamuzi bali ni amri ya mahakama.
Akijibu hoja hizo, wakili wa utetezi Kenedy Fungamtama ambaye alikuwa akisadiana na Fulgence Massawe na Peter Kibatala, alidai kuwa maombi yao ni ya msingi kwani wamefuata taratibu zote za kisheria na kuomba mahakama iyasikilize.

“Tulichofanya tumefanya kwa kufuata amri iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kilichoko hapa ni ubishi kuhusiana na umri wa mshtakiwa,”alidai Fungamtama na kuongeza kuwa:

“Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haikutoa uamuzi bali ilitoa amri kwa mawakili wa mshtakiwa kama wana maombi yoyote wafanye hivyo kupitia mahakama kuu na ndivyo tulivyofanya,”alidai.

Wakili huyo wa utetezi aliendelea kudai kuwa, hata katika sheria ya mtoto ya mwaka 2009 imetafsiri neno mahakama ikimaanisha kuwa ni ile ya mwanzo, wilaya, mkoa ama mahakama kuu hivyo ni sahihi maombi yao kuwapo mahakamani hapo.

“Upande wa mashtaka wameshindwa kuisaidia mahakama hii ni taratibu zipi ambazo hatukuzifuata katika kuwasilisha maombi haya hivyo pingamizi lao litupiliwe mbali,”alidai Fungamtama.

Upande wa utetezi pia ulinukuu kesi mbalimbali zikiwamo rufaa ya madai namba 86/2009 kati ya Samson Mwalida na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na  kati ya Farida na Kampuni ya Scania Tanzania Ltd.

Jaji Twaibu baada ya kusikiliza hoja zote, aliwauliza maswali.Jaji: Je mnadhani Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haikuwa na mamlaka ya kusikiliza maombi haya?
Jaji: Nikiangalia kumbukumbu katika jalada hili wakili Kaganda (upande wa mashtaka) alisema Mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza maombi haya kwasababu kesi iliyoko mbele yake ni ya mauaji ambayo husikilizwa na mahakama kuu.

Kaganda: Mtukufu Jaji mimi nilisema hivyo nikimaanisha kwamba bado tunaendelea na upelelezi na kati ya vitu tunavyochunguza ni pamoja na suala la umri wa mshtakiwa.
Baada ya kusikiliza hoja zote Jaji Twaib aliahirisha kesi hiyo hadi Juni 11 mwaka huu atakapotoa uamuzi kuhusiana na maombi hayo.

Upande wa utetezi umewasilisha maombi hayo ukiiomba mahakama kuu iangalie na kuona kama mahakama ya kisutu ina uwezo wa kuamua suala hilo.

Sunday, May 27, 2012

UPEPO WA RECHO NA SHILOLE NDANI YA MAISHA CLUB


MSANII WA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA H BABA AENDELEZA MASHAMBULIZI KANDA YA KASKAZINI.


 Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya H Baba akiwapa raha ya burudani ya muziki wake wakazi wa Tarakea Rombo kwenye akiwa kwenye ziara ya Promosheni mbalimbali za kampuni ya Simu za mkononi ya Tigo.
 H Baba akiwapa zawadi za T shirt watoto kabla nao hawajacheza pamoja nae.
 Akihamasisha mashabiki wake kucheza.
Hapa sasa anaonyesha uwezo wake mbele ya mashabiki.