BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Sunday, November 27, 2011

'Mbayuwayu' NGO NGO NGO ... my favourite song of the day...

  


  

Yalaiti''' My song of the day...

Monday, November 21, 2011

Nicki Samonas kusaidia shule za msingi zote nchini kwake


Muigizaji Nikki Samonas wa Ghana ambaye ni mzaliwa wa Ghana ameamua kusaidia shule zote msingi kwenye wilaya za nchi hiyo.

Nikki ameweka bayana kwamba atagawa vitabu na vifaa mbalimbali vya elimu kwenye shule za wilaya zote za Ghana utakapoanza msimu mpya mwezi Januari mwakani.

Msanii huyo amepanga kugawa vitabu 10,000 kwa kila wilaya kupitia Shirika lake aliloanzisha linaloitwa 'Help Them Learn'. Alisema kuwa;

Nimepanga kufanya huu mradi kusaidia wanafunzi wasiojiweza, wapate elimu na maarifa. Elimu inaleta heshima na maisha bora,"alisisitiza huku akipanga kuchangisha zaidi kutoka kwa mashirika ya kimataifa.

MWIGIZAJI wa filamu za Bongo, Haji Adam Baba Haji anajuta kupoteza muda wake kwa kuchelewa kusomea sanaa na masuala ya filamu.

Masomo hayo anayosoma kwa sasa katika Chuo cha Sanaa Bagamoyo yatamgharimu miaka mitatu.
Ninaamini kuwa baada ya kumaliza masomo yangu nitakuwa ni msanii wa kimataifa kweli kwa vitendo siyo kwa maneno tu, aliiambia Mwanaspoti.

Nimekuwapo hapa na nimejifunza mambo mengi sana kuhusu sanaa tunayoifanya hususani filamu, wasanii pamoja na watayarishaji tumeshindwa kabisa kuifanya tasnia hii ilete maslahi kwetu.

Nilichogundua ni ukosefu wa elimu hali inayopoteza umakini katika katika kazi zetu.

Msanii huyo amewashauri wasanii wengine kujiendeleza kielimu badala ya kutegemea vipaji tu, kwani anaamini kuwa mambo hayo yana mwisho wake hasa katika karne hii.

Anasema kuwa jambo ambalo analiona kwa sasa ni wasanii kufurahia maslahi kidogo yanayopatikana tena bila kuwa ya uhakika nayo.

Haji hivi karibuni alichaguliwa kuwa Rais wa Wanafunzi chuoni hapo

Wema amdondokea Linex

MWIGIZAJI na mrembo aliyewahi kushikilia taji la Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu, wiki hii amegeuka na kuamua kumwangukia msanii, Sunday Mangu Linex baada ya kumkashifu wiki kadhaa zilizopita kupitia ukurasa wake wa Facebook.

Wema sasa amemwomba msamaha Linex kutokana na kitendo cha kumwingiza katika ugomvi aliokuwa nao na msichana mwenzake.

Amekiri na kusema kuwa ilikuwa ni hasira tu na alijikuta ameandika ujumbe uliomhusisha Linex kimakosa.

Ni hali ya kawaida na si mpango wangu kumkosea Linex, ila nilikuwa nikitolea mfano tu na sikumaanisha vile, ameandika Wema. 

Wakati huohuo, Linex wiki hii ameandika kupitia ukurasa wake wa Facebook kwamba amemsamehe mwigizaji huyo.

Linex alipokuwa Kigoma kwenye msiba wa babu yake aliyemlea, anasema alipata simu kutoka kwa watu wakimtaka kuingia katika ukurasa wa Blackberry Messenger maarufu kama BBM wa Wema Sepetu ili asome nini mlimbwende huyo amekiandika kuhusu yeye.

Kwa kweli nilijisikia vibaya sana baada ya kusoma ujumbe aliokua ameuandika,alisema Linex.

Umekosa watu mpaka unatembea na mtu wa ajabu kama Linex,ni ujumbe ambao Linex anadai uliandikwa na Wema na kusomwa na watu wengi.
Lakini sasa wameshasameheana.


Tuesday, November 15, 2011

STAR ACTOR,BABA SUWE FINALLY RELEASED


The embattled Yoruba actor/comedian, Babatunde Omidina, popularly known as Baba Suwe, was finally released today.

This followed the order of the Ikeja High Court that the comedian be released on bail on Friday, the 4th of November (today) if no drug was found on him.

The comedian was arrested by officers of National Drug Law Enforcement Agency (NDLEA) on his way to France on October 12, 2011 on the suspicions of ingesting substance suspected to be cocaine.

Welcome to freedom Baba Suwe! 

STAR ACTOR JIM IYKE IN COURT OVER N15 MILLION FRAUD


Controversial actor, Jim Iyke was on Thursday arraigned before an Abuja court for allegedly fleecing one Habiba Abubakar of the sum of N15 Millon.

Abubarkar was said to have petitioned the Inspector general of Police on August 8, to investigate the fraud.

In the petition, Abubakar accused Jim of deceiving her into acquiring 15% equity from his company, Untamed Records Ltd and as soon as the money was paid into his account, the actor converted the money to his personal use and went on shopping spree all around the world.

The petitioner further said the accused resorted to beating her and threatened to kill her when she requested for her money.

Jim pleaded not guilty to all the charges and was granted bail on N500,000 with two sureties in like sum. Case has been adjourned till December 9, 2011 for further hearing.

Thursday, November 10, 2011

Nollywood actress Mary Remmy loses sister to Boko Haram

Eucharia Remmy, the sister of fast rising Nollywood actress Mary Remmy is dead, Nollywoodgossip can confirm.
Eucharia, who graduated from the University of Nigeria Nsukka in 2010, was undergoing her youth service at Damaturu in Yobe state when she was attacked and killed by Boko Haram.  The bomb attack that killed her was said to have so far left 150 people dead.
Her actress sister Mary is famous for her roles in hit movies Beyonce and Rihanna and Blackberry Babes.
May her soul rest in peace.

NOLLYWOOD ACTOR,DANIEL IYAMU ALLEGEDLY MURDERED BY HIS WIFE

The Nigerian movie industry otherwise known as Nollywood again was thrown into mourning on Tuesday, as it lost one of its respected actor, Daniel Iyamu to the cold hands of death.

Sources revealed that the Benin based actor was allegedly murdered by his wife.

Family sources said that Iyamu was found dead in a pool of his blood on his bed after neighbours forcefully broke his door open.

It was learnt that injuries were found on his head which suggested that he might have been hit on the head while asleep.

The wife has reportedly made statements to the police amidst tears, saying that she hit her husband with a pestle which led to his death.

One of the children of the late actor, Faith, a student of Federal Polytechnic Auchi, told journalists that their mother has been suffering from suspected mental illness, which their father has been treating since last year

Tuesday, November 8, 2011

AKUTWA CHUMBANI KWA DBANJI....


AWALI alikanusha kwamba hana uhusiano wowote wa kimapenzi na msanii Fally Ipupa wa Congo, lakini sasa Nadia Buari amefumwa nyumbani kwa mwanamuziki Dbanj wa Nigeria.

Msanii huyo raia wa Ghana alifumwa ndani ya jumba la mwanamuziki huyo usiku hivikaribuni akiwa amejivinjari kwenye kigauni cha kulalia huku akigonga mvinyo.

Chanzo kingine kimethibitisha kwamba mastaa hao wamekuwa na uhusiano wa kimapenzi muda mrefu na hata Ghana wamekuwa wakionekana pamoja. Nadia anayekaribia miaka 30.

Kama ni kweli wawili hao wana mpango wa kuoana utakuwa ni mwisho wa uvumi uliokuwa umeenea kwamba D'banj alikuwa kwenye penzi zito la muigizaji Genevieve Nnaji.

VICHWA VYA MTITU...


MARA nyingi watayarishaji wa filamu za Bongo hupenda kuwatumia wasanii wenye majina maarufu, kuliko kutafuta vipaji vipya ili kuvina nafasi.
Lakini hali hiyo ni tofauti kidogo kwa mwongozaji na mtayarishaji wa filamu, William John, maarufu kwa jina la Mtitu, ambaye ni Mkurugenzi wa 5 Effect ya jijini Dar es Salaam.
Awali alianza na filamu iliyojulikana kwa jina la Sandra ambapo aliwashirikisha wasanii waliokuwa wakivuma na michezo ya kuigiza kama Single Mtambalike na Haji Adam.
Mtayarishaji huyo ambaye anaamini kuwa ukiwa na hadithi nzuri inaweza kuwakilishwa na msanii yeyote mwenye sifa na vigezo vya kuigiza.
Wasanii aliowaibua na kuwa nyota hadi leo ni Aunt Ezekiel, Yusuph Mlela, Irene Uwoya na Mariam Ismail. Wasanii hao kwa sasa ni nyota na wanatesa katika tasnia ya filamu.
Aunty Ezekiel
Msanii huyu kwa mara ya kwanza kabisa alishiriki filamu iliyojulikana kwa jina la Miss Bongo, Mtitu anasema kuwa baada ya kuandaa filamu hiyo, alifanya usahili kwa wasanii mbalimbali lakini nafasi ya Miss ilisumbua hadi alipompata
Yusuph Mlela
Ni kijana aliyekuwa katika fani ya mavazi, lakini Mtitu alimwibua na kumfanya kuwa mmoja kati ya wasanii wanaotesa katika tasnia ya filamu, alipomshirikisha katika filamu ya Diversion Of Love.
Humo aliigiza nafasi ya msanii chipukizi na kuibuka mshindi katika Tuzo za Vinara kupitia filamu hiyo.
Irene Uwoya
Hana tofauti na Mlela kwani naye akitokea katika mambo ya urembo kama alivyokuwa Aunty Ezekiel, alipewa uhusika katika filamu ya Diversion Of Love na kufanya vizuri.
Mariamu Ismail
Ni msanii ambaye tayari anatikisa anga hizi za tasnia ya filamu baada ya kuibuliwa na Mtitu kwa kumshirikisha katika filamu ya Best Man, ambayo ameiigiza kwa umahiri mkubwa na kuwafunika baadhi ya nyota.
Mariam alimudu kuigiza na nyota wakubwa kama Cloud, Mlela na Hemed.

Saturday, November 5, 2011

LOST HOPE INAKUJA..

BAADA ya kufanya vizuri katika filamu ya Blue Monday, muandaaji wa filamu hiyo, Abui Ahmed amewataka wapenzi wa filamu nchini kukaa tayari kwa ujio wa filamu mpya itakayokwenda kwa jina la  Lost Hope.

Ahmed ambaye pia  ni   Mkurugenzi wa Abui Production alisema kuwa filamu hiyo   iliyobeba ujumbe mzito wa familia na mapenzi kwa ujumla itakuwa sokoni mapema wiki ijayo.

“Filamu hii imebeba ujumbe mzito ambao nina uhakika utaelimisha jamii kwa ujumla na vilevile kumfanya kila mtu ajifunze kwa nafasi yake kutokana na kile kilichopo ndani ya filamu hii”alisema Ahmed.

Aliwataja wasanii walioshiriki katika filamu hiyo ni pamoja na Michael Philipo (Kojack) ,Nila Sultani (Jasmin) ambao ni wahusika wakuu na wengine ni Flora Mvungi,Mainda,Abdala Agosi, Badi pamoja na wengine wengi.

Abui Production  imehusika kuandaa filamu mbalimbali zikiwemo Zindiko,Tension of Love na Blue Monday ambayo inafanya vizuri katika soko la filamu nchini.

WAZEE WATATU VICHWA KATIKA TASNIA YA FILAMU KWA SASA...

KILA unapokutana na filamu yoyote ya Bongo, si rahisi kuzikosa sura hizi katika filamu hizo. Sura hizo ni za wasanii Hashim Kambi �Ramsey�, Charles Magali �Mzee Magali� na Ahmed Olotu �Mzee Chilo�.

Wakongwe hao hata kama watakuwa wameigiza japo kwa ufupi, lakini ndiyo wasanii wa kiume wanaoongoza katika kushiriki filamu nyingi za Bongo, ukiachilia Ray na Kanumba, ambayo hufanya kazi zao wenyewe. 

Uchunguzi unaonesha kuwa wasanii hao wamekuwa wakihusishwa katika filamu mbalimbali kutokana na uhusika wao, kwa maana watu wenye mwonekano wa kiutu uzima.

Pengine kama wangekuwa wanalipwa vizuri, ni wazi tungezungumza mambo mengine kwa sasa. Walistahili kuwa matajiri wa kutupwa. 

Lakini kwa bahati mbaya, Bongo, pamekuwa na mfumo usioeleweka. Hollywood, Bollywood na kwingineko wasanii kama hawa hutengeneza fedha nyingi kwa kila hatua, kuanzia mikataba ya ushiriki wa filamu husika, maonyesho ya filamu katika majumba ya sinema na uuzaji wa filamu katika DVD. 


Friday, November 4, 2011

TBC KUANZA KUONESHA CHINA-SWAHILI SOAP OPERA NOVEMBER HII...


Shirika la utangazaji la Tanzania TBC leo limetangaza uzinguzi rasmi wa tamthiliya ya kichina mbayo imetafsiriwa kwa Kiswahili na wantanzania waishio nchini humo na wafanyakazi wa kituo cha radio cha China radio International (CRI).
Tamthiliya hiyo ambayo itajulikana kwa jina la ‘Dou Dou na Visa vya Mama Wakwe zake’ itaanza kuonyeswa rasmi TBC 1 tarehe 23 mwezi huu wa kumi na moja.
Akizungumza na waandishi wa habari mkurugenzi mkuu wa TBC Mr Clemence Mshana alisema kuwa lengo kubwa la tamthiliya hiyo ni kuonyesha jinsi lugha adhimu ya Kiswahili inavyoweza kutumika moja kwa moja bila kuweka tafsiri za maandishi katika filamu au tamthiliya kuelezea utamaduni wa mataifa mengine.
Alisema kuwa kupita tamthiliya hii, ambayo inatarajiwa kuzinduliwa rasmi wiki ya mwisho wa mwezi huu wa November, itawasaidia wasanii wa Tanzania ninsi wanavyoweza kutengeneza tamthiliya nzuri zenye ubora na zikaweza kuuzwa nchi za nje na hivyo kukuza matumizi ya lugha ya Kiswahili nje ya Tanzania.
“ Vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kuitangaza lugha ya Kiswahili kwa kueleza jamii kuwa inatosheleza katika Nyanja mbali mbali za maisha ya binadamu bila kujali taifa lake,” alisema.