BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Tuesday, December 6, 2011

Ramsey awaasa wasanii wa muvi bongo..


VIPAJI vina nafasi kubwa katika ulimwengu wa sanaa, lakini kuna wakati lazima mhusika atafute elimu kwa ajili ya kulinda na kuendeleza kipaji chake.

Hayo ni maneno ya mwigizaji mahiri wa filamu Bongo, Hashim Kambi Ramsey aliyoyatoa hivi karibuni katika mazungumzo yake na Mwanaspoti.

Wakati naanza kuigiza nilikuwa najua ni kitu cha kujifurahisha tu, nilifanya hivi huku nikiendelea na shughuli nyingine, anasema Ramsey.

Lakini nimebaini uigizaji ni kazi. Inakuhitaji mtu uwe na taaluma hiyo ili uweze kudumu nayo katika kiwango bora.

Kinachosikitisha tu ni kuwa kuna hili tatizo la gharama kuwa kubwa kwa masomo ya filamu.

Akielezea zaidi, anasema kwamba wasanii wanaweza kujiendeleza kwa njia ya mitandao ya filamu, kama anavyofanya yeye.

MAGIC MONEY SOKONI HIVI KARIBUNI.


'PESA SHETANI ASIYE EPUKIKA KATIKA DUNIA HII YA SASA NA USIOMBE ABISHE HODI NDANI YA FAMILIA KABISA'' ...KUMKANYWA NA KUPEWA TAHADHALI KWA MTU NDIYO KUMTIA HAMASA NA MUWASHAWASHA KUITIKIA KIU YA NAFSI YAKE YA TAMAA YA PESA NA HAPO MAISHA YA KUKIMBIA DAIMA HUANZA NA NDIYO MATOKEO YAKE KAMA SIO KUKOSANA NA NDUGU AU MPENZI/MUME/MKE WAKO...MTIZAME BINTI HUYU NAMNA NDOA YAKE INAVYO TIBULIWA NA SHETANI (PESA)


CAST
Daudi Michael (DAUDI)
Hemed Suleiman (ERICK)
Halima Yahaya (SANTANA)
Msafili Njechele (BUGO)
Ibrahim Lipili(NYANGO)
Ratifa Idabu (BADRA)


STORY
Daudi Michael
SCRIPT
Daudi Michael
EXCTIVE PRODUCER
D.Production
(A DAUDI MICHAEL FILM PROMO)

Sunday, December 4, 2011

SAJUKI AFUNGUKA KUGAWANYIKA KWA WASANII...

MWIGIZAJI na mwongozaji wa filamu Bongo, Juma Kilowoko Sajuki, amesema watayarishaji wa filamu wamegawanyika katika makundi, ingawa ni vugumu mwingine kulibaini hilo.

Akizungumza na jukwaa hili nyumbani kwake Tabata Bima, jijini Dar es Salaam, msanii huyo ambaye kwa sasa anasumbuliwa na tumbo, anasema kuwa mara nyingi wale ulio karibu nao ndiyo hukuzunguka.

Sisi wasanii tayari tuna makundi japo tunafanya kazi moja, kwa mfano mimi rafiki zangu labda Frank au Dino, basi watakuwa ni hao tu, hata linapotokea jambo kama la msaada wao ndiyo watawajibika, alisema.

Hata kama mtu akiongea na mwingine atasema kuwa huyu jamaa hajichanganyi na watu, lakini ukweli tunajuana kuwa kila mtu na mtu wake. Msanii huyo alisema japo jambo hilo lipo, lakini si rahisi kuyataja makundi hayo. Kutokana na hali hiyo, anawataka wasanii kujilazimisha kujenga umoja wa kweli kuliko ilivyo sasa.

MABINTI WANAOTETEMESHA VIDUME NOLLYWOOD..

MERCY Johnson ameshaolewa. Nani anafuata? Ndiyo swali wanalojiuliza mashabiki wa filamu za Nollywood, asilimia kubwa ya wasanii wa kike hawajaolewa na wengine hawana hata mpango na hayo mambo.
Wengine walishaolewa wakaachika kutokana na kuendekeza starehe na kushindwa kutulia kwenye ndoa zao. Hii ni orodha ya mabinti ambao hawajaolewa na wanaotetemesha wanaume Nollywood. 

Funke Akindele
Huyu binti ana mafanikio makubwa kikazi na ni miongoni mwa wasanii wanaolipwa sana. Ana umri wa miaka 35, hana skendo nyingi za mapenzi kama walivyo mastaa wengine wa Nollywood.
Yuko kwenye uhusiano wa kudumu na huenda muda wowote akatamka jambo kwa marafiki zake.
Amesomea sheria kwenye Chuo Kikuu cha Lagos. Baadhi ya filamu alizowahi kufanya ni kama Jenifa, Omo Ghetto na Return of Jenifa Part 2. 

Rita Dominic
Sura na umbo lake vinadanganya watu wengi sana, ukimwangalia kwa haraka unaweza kudhani ana umri wa miaka 25, lakini kwa taarifa yako ana miaka 37 sasa na bado pia yumo kwenye kundi hilo la mabachela.
Mambo yake ya uhusiano wa zamani hayajafunuliwa sana lakini aliwahi kuwa na uhusiano na msanii mwenzie, Jim Iyke, hususani alipokuwa anaishi maeneo ya Wemabod Estates, Ikeja. 

Genevieve Nnaji
Miaka yake ni 32 na anatafsiriwa kama nembo ya filamu za Nollywood Afrika na Dunia nzima. Ni miongoni mwa mabinti matajiri Nigeria, lakini bado hajabahatika kufanya maamuzi magumu ya kuachana na ubachela.
Ana mtoto mmoja wa kike na awali alishavumishwa kuwa na uhusiano na Makamu wa Rais wa zamani wa Nigeria, Abubakar Atiku. 

Chika Ike
Ni mzuri na ana mvuto. Aliolewa lakini baada ya muda akaachika kwa sababu ambazo marafiki zake wa karibu waliziita za kitoto na ni binti wa kuendekeza sana starehe. Amenunua Range Rover ya kisasa na amefungua saluni za kisasa jijini Abuja, kama ni fedha anayo. 

Uche Jombo
Anawatoa udenda wengi. Lakini rafiki yake wa karibu amedokeza kwamba huyu binti hana mpango wa kuolewa sasa hivi, akili yake imekaa kibiashara zaidi. Anatengeneza fedha sana na anajua kuzitumia.
Anaishi maeneo ya Lekki jijini Lagos. Ametamba na filamu kama Secret Fantasy, Endless Lies, Kiss and Tell, Silent Scandal na Home in Exile. Miaka yake ni 32 na ni msomi wa Chuo Kikuu cha Calabar, Nigeria. Aliwahi kuwa na uhusiano na Ikechukwu Uche ambaye ni mchezaji. 

Monalisa Chinda
Ni bachela mzoefu. Aliolewa akazaa mtoto mmoja maisha yakamshinda akaamua kurudi kwao na sasa maisha yanaendelea kwa staili ya kujirusha kwa wingi.
Mwanaume waliyeachana naye ameshaoa lakini Monalisa bado yupo yupo ingawa inaelezwa wanaume wengi sana wanamnyemelea. Amesomea sanaa kwenye Chuo Kikuu cha Port Harcourt kwao Nigeria. 

Stephanie Okereke
Kila kukicha ana skendo na sura yake haikosekani kwenye kurasa za mbele za magazeti ya udaku. Kwenye masuala ya urefu na uzuri kote amesheheni.
Alishawahi kuolewa pia akaachika sasa hivi yuko kwenye penzi zito na jamaa mmoja anaitwa Linus Idahosa. Hakuna anayejua ni lini wana mpango wa kuoana.

MATANGAZO YA BIASHARA HAYA LIPI.... Ray

NYOTA katika tasnia ya filamu Bongo, Vincent Kigosi (Ray), amesema matangazo ya biashara hayalipi na ndiyo maana hashiriki katika kutengeneza matangazo hayo kwa sababu hayana faida kwake.

Si kama sipati matangazo ya biashara kwa ajili ya kutangaza bidhaa, fedha wanayotoa wahusika ni ndogo sana kiasi cha kukatisha tamaa, siwezi kutumika katika matangazo kwa pesa ndogo wakati nikitengeneza filamu naipata zaidi ya hiyo, alisema Ray.

Kwa wale wanaopenda sifa za kuonekana bila faida waache tu wafanye, lakini mimi msimamo wangu upo kimaslahi zaidi.

Msanii huyo alisema kuwa tatizo la matangazo hayo pamoja na kuwa malipo ni kidogo, lakini hayana ukomo wa muda wa kutumika. 

Mwenye bidhaa husika ana uwezo wa kulitumia hata milele bila kuendelea na malipo mengine, sasa hii si halali kabisa, aliongeza.

Mara nyingi makampuni hunifuata, lakini kila linapofika suala la malipo na ukomo wa tangazo wanakimbia, kuna tangazo ilitakiwa nilifanye, lakini baada kuambiwa kuwa nitalipwa dola 2,500 (Sh 223,864 za Kenya) na litatumika milele bila malipo ya ziada nilikataa.

Msanii huyo alisema kama kuna kampuni inataka kufanya kazi naye anaikaribisha, lakini ikubali kutimiza masharti yake kwa kuwa na mkataba unaoeleweka na si wa kuuza sura.

Monday, November 21, 2011

Nicki Samonas kusaidia shule za msingi zote nchini kwake


Muigizaji Nikki Samonas wa Ghana ambaye ni mzaliwa wa Ghana ameamua kusaidia shule zote msingi kwenye wilaya za nchi hiyo.

Nikki ameweka bayana kwamba atagawa vitabu na vifaa mbalimbali vya elimu kwenye shule za wilaya zote za Ghana utakapoanza msimu mpya mwezi Januari mwakani.

Msanii huyo amepanga kugawa vitabu 10,000 kwa kila wilaya kupitia Shirika lake aliloanzisha linaloitwa 'Help Them Learn'. Alisema kuwa;

Nimepanga kufanya huu mradi kusaidia wanafunzi wasiojiweza, wapate elimu na maarifa. Elimu inaleta heshima na maisha bora,"alisisitiza huku akipanga kuchangisha zaidi kutoka kwa mashirika ya kimataifa.

MWIGIZAJI wa filamu za Bongo, Haji Adam Baba Haji anajuta kupoteza muda wake kwa kuchelewa kusomea sanaa na masuala ya filamu.

Masomo hayo anayosoma kwa sasa katika Chuo cha Sanaa Bagamoyo yatamgharimu miaka mitatu.
Ninaamini kuwa baada ya kumaliza masomo yangu nitakuwa ni msanii wa kimataifa kweli kwa vitendo siyo kwa maneno tu, aliiambia Mwanaspoti.

Nimekuwapo hapa na nimejifunza mambo mengi sana kuhusu sanaa tunayoifanya hususani filamu, wasanii pamoja na watayarishaji tumeshindwa kabisa kuifanya tasnia hii ilete maslahi kwetu.

Nilichogundua ni ukosefu wa elimu hali inayopoteza umakini katika katika kazi zetu.

Msanii huyo amewashauri wasanii wengine kujiendeleza kielimu badala ya kutegemea vipaji tu, kwani anaamini kuwa mambo hayo yana mwisho wake hasa katika karne hii.

Anasema kuwa jambo ambalo analiona kwa sasa ni wasanii kufurahia maslahi kidogo yanayopatikana tena bila kuwa ya uhakika nayo.

Haji hivi karibuni alichaguliwa kuwa Rais wa Wanafunzi chuoni hapo

Wema amdondokea Linex

MWIGIZAJI na mrembo aliyewahi kushikilia taji la Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu, wiki hii amegeuka na kuamua kumwangukia msanii, Sunday Mangu Linex baada ya kumkashifu wiki kadhaa zilizopita kupitia ukurasa wake wa Facebook.

Wema sasa amemwomba msamaha Linex kutokana na kitendo cha kumwingiza katika ugomvi aliokuwa nao na msichana mwenzake.

Amekiri na kusema kuwa ilikuwa ni hasira tu na alijikuta ameandika ujumbe uliomhusisha Linex kimakosa.

Ni hali ya kawaida na si mpango wangu kumkosea Linex, ila nilikuwa nikitolea mfano tu na sikumaanisha vile, ameandika Wema. 

Wakati huohuo, Linex wiki hii ameandika kupitia ukurasa wake wa Facebook kwamba amemsamehe mwigizaji huyo.

Linex alipokuwa Kigoma kwenye msiba wa babu yake aliyemlea, anasema alipata simu kutoka kwa watu wakimtaka kuingia katika ukurasa wa Blackberry Messenger maarufu kama BBM wa Wema Sepetu ili asome nini mlimbwende huyo amekiandika kuhusu yeye.

Kwa kweli nilijisikia vibaya sana baada ya kusoma ujumbe aliokua ameuandika,alisema Linex.

Umekosa watu mpaka unatembea na mtu wa ajabu kama Linex,ni ujumbe ambao Linex anadai uliandikwa na Wema na kusomwa na watu wengi.
Lakini sasa wameshasameheana.


Tuesday, November 15, 2011

STAR ACTOR,BABA SUWE FINALLY RELEASED


The embattled Yoruba actor/comedian, Babatunde Omidina, popularly known as Baba Suwe, was finally released today.

This followed the order of the Ikeja High Court that the comedian be released on bail on Friday, the 4th of November (today) if no drug was found on him.

The comedian was arrested by officers of National Drug Law Enforcement Agency (NDLEA) on his way to France on October 12, 2011 on the suspicions of ingesting substance suspected to be cocaine.

Welcome to freedom Baba Suwe! 

STAR ACTOR JIM IYKE IN COURT OVER N15 MILLION FRAUD


Controversial actor, Jim Iyke was on Thursday arraigned before an Abuja court for allegedly fleecing one Habiba Abubakar of the sum of N15 Millon.

Abubarkar was said to have petitioned the Inspector general of Police on August 8, to investigate the fraud.

In the petition, Abubakar accused Jim of deceiving her into acquiring 15% equity from his company, Untamed Records Ltd and as soon as the money was paid into his account, the actor converted the money to his personal use and went on shopping spree all around the world.

The petitioner further said the accused resorted to beating her and threatened to kill her when she requested for her money.

Jim pleaded not guilty to all the charges and was granted bail on N500,000 with two sureties in like sum. Case has been adjourned till December 9, 2011 for further hearing.

Thursday, November 10, 2011

Nollywood actress Mary Remmy loses sister to Boko Haram

Eucharia Remmy, the sister of fast rising Nollywood actress Mary Remmy is dead, Nollywoodgossip can confirm.
Eucharia, who graduated from the University of Nigeria Nsukka in 2010, was undergoing her youth service at Damaturu in Yobe state when she was attacked and killed by Boko Haram.  The bomb attack that killed her was said to have so far left 150 people dead.
Her actress sister Mary is famous for her roles in hit movies Beyonce and Rihanna and Blackberry Babes.
May her soul rest in peace.

NOLLYWOOD ACTOR,DANIEL IYAMU ALLEGEDLY MURDERED BY HIS WIFE

The Nigerian movie industry otherwise known as Nollywood again was thrown into mourning on Tuesday, as it lost one of its respected actor, Daniel Iyamu to the cold hands of death.

Sources revealed that the Benin based actor was allegedly murdered by his wife.

Family sources said that Iyamu was found dead in a pool of his blood on his bed after neighbours forcefully broke his door open.

It was learnt that injuries were found on his head which suggested that he might have been hit on the head while asleep.

The wife has reportedly made statements to the police amidst tears, saying that she hit her husband with a pestle which led to his death.

One of the children of the late actor, Faith, a student of Federal Polytechnic Auchi, told journalists that their mother has been suffering from suspected mental illness, which their father has been treating since last year

Tuesday, November 8, 2011

AKUTWA CHUMBANI KWA DBANJI....


AWALI alikanusha kwamba hana uhusiano wowote wa kimapenzi na msanii Fally Ipupa wa Congo, lakini sasa Nadia Buari amefumwa nyumbani kwa mwanamuziki Dbanj wa Nigeria.

Msanii huyo raia wa Ghana alifumwa ndani ya jumba la mwanamuziki huyo usiku hivikaribuni akiwa amejivinjari kwenye kigauni cha kulalia huku akigonga mvinyo.

Chanzo kingine kimethibitisha kwamba mastaa hao wamekuwa na uhusiano wa kimapenzi muda mrefu na hata Ghana wamekuwa wakionekana pamoja. Nadia anayekaribia miaka 30.

Kama ni kweli wawili hao wana mpango wa kuoana utakuwa ni mwisho wa uvumi uliokuwa umeenea kwamba D'banj alikuwa kwenye penzi zito la muigizaji Genevieve Nnaji.

VICHWA VYA MTITU...


MARA nyingi watayarishaji wa filamu za Bongo hupenda kuwatumia wasanii wenye majina maarufu, kuliko kutafuta vipaji vipya ili kuvina nafasi.
Lakini hali hiyo ni tofauti kidogo kwa mwongozaji na mtayarishaji wa filamu, William John, maarufu kwa jina la Mtitu, ambaye ni Mkurugenzi wa 5 Effect ya jijini Dar es Salaam.
Awali alianza na filamu iliyojulikana kwa jina la Sandra ambapo aliwashirikisha wasanii waliokuwa wakivuma na michezo ya kuigiza kama Single Mtambalike na Haji Adam.
Mtayarishaji huyo ambaye anaamini kuwa ukiwa na hadithi nzuri inaweza kuwakilishwa na msanii yeyote mwenye sifa na vigezo vya kuigiza.
Wasanii aliowaibua na kuwa nyota hadi leo ni Aunt Ezekiel, Yusuph Mlela, Irene Uwoya na Mariam Ismail. Wasanii hao kwa sasa ni nyota na wanatesa katika tasnia ya filamu.
Aunty Ezekiel
Msanii huyu kwa mara ya kwanza kabisa alishiriki filamu iliyojulikana kwa jina la Miss Bongo, Mtitu anasema kuwa baada ya kuandaa filamu hiyo, alifanya usahili kwa wasanii mbalimbali lakini nafasi ya Miss ilisumbua hadi alipompata
Yusuph Mlela
Ni kijana aliyekuwa katika fani ya mavazi, lakini Mtitu alimwibua na kumfanya kuwa mmoja kati ya wasanii wanaotesa katika tasnia ya filamu, alipomshirikisha katika filamu ya Diversion Of Love.
Humo aliigiza nafasi ya msanii chipukizi na kuibuka mshindi katika Tuzo za Vinara kupitia filamu hiyo.
Irene Uwoya
Hana tofauti na Mlela kwani naye akitokea katika mambo ya urembo kama alivyokuwa Aunty Ezekiel, alipewa uhusika katika filamu ya Diversion Of Love na kufanya vizuri.
Mariamu Ismail
Ni msanii ambaye tayari anatikisa anga hizi za tasnia ya filamu baada ya kuibuliwa na Mtitu kwa kumshirikisha katika filamu ya Best Man, ambayo ameiigiza kwa umahiri mkubwa na kuwafunika baadhi ya nyota.
Mariam alimudu kuigiza na nyota wakubwa kama Cloud, Mlela na Hemed.

Saturday, November 5, 2011

LOST HOPE INAKUJA..

BAADA ya kufanya vizuri katika filamu ya Blue Monday, muandaaji wa filamu hiyo, Abui Ahmed amewataka wapenzi wa filamu nchini kukaa tayari kwa ujio wa filamu mpya itakayokwenda kwa jina la  Lost Hope.

Ahmed ambaye pia  ni   Mkurugenzi wa Abui Production alisema kuwa filamu hiyo   iliyobeba ujumbe mzito wa familia na mapenzi kwa ujumla itakuwa sokoni mapema wiki ijayo.

“Filamu hii imebeba ujumbe mzito ambao nina uhakika utaelimisha jamii kwa ujumla na vilevile kumfanya kila mtu ajifunze kwa nafasi yake kutokana na kile kilichopo ndani ya filamu hii”alisema Ahmed.

Aliwataja wasanii walioshiriki katika filamu hiyo ni pamoja na Michael Philipo (Kojack) ,Nila Sultani (Jasmin) ambao ni wahusika wakuu na wengine ni Flora Mvungi,Mainda,Abdala Agosi, Badi pamoja na wengine wengi.

Abui Production  imehusika kuandaa filamu mbalimbali zikiwemo Zindiko,Tension of Love na Blue Monday ambayo inafanya vizuri katika soko la filamu nchini.

WAZEE WATATU VICHWA KATIKA TASNIA YA FILAMU KWA SASA...

KILA unapokutana na filamu yoyote ya Bongo, si rahisi kuzikosa sura hizi katika filamu hizo. Sura hizo ni za wasanii Hashim Kambi �Ramsey�, Charles Magali �Mzee Magali� na Ahmed Olotu �Mzee Chilo�.

Wakongwe hao hata kama watakuwa wameigiza japo kwa ufupi, lakini ndiyo wasanii wa kiume wanaoongoza katika kushiriki filamu nyingi za Bongo, ukiachilia Ray na Kanumba, ambayo hufanya kazi zao wenyewe. 

Uchunguzi unaonesha kuwa wasanii hao wamekuwa wakihusishwa katika filamu mbalimbali kutokana na uhusika wao, kwa maana watu wenye mwonekano wa kiutu uzima.

Pengine kama wangekuwa wanalipwa vizuri, ni wazi tungezungumza mambo mengine kwa sasa. Walistahili kuwa matajiri wa kutupwa. 

Lakini kwa bahati mbaya, Bongo, pamekuwa na mfumo usioeleweka. Hollywood, Bollywood na kwingineko wasanii kama hawa hutengeneza fedha nyingi kwa kila hatua, kuanzia mikataba ya ushiriki wa filamu husika, maonyesho ya filamu katika majumba ya sinema na uuzaji wa filamu katika DVD. 


Friday, November 4, 2011

TBC KUANZA KUONESHA CHINA-SWAHILI SOAP OPERA NOVEMBER HII...


Shirika la utangazaji la Tanzania TBC leo limetangaza uzinguzi rasmi wa tamthiliya ya kichina mbayo imetafsiriwa kwa Kiswahili na wantanzania waishio nchini humo na wafanyakazi wa kituo cha radio cha China radio International (CRI).
Tamthiliya hiyo ambayo itajulikana kwa jina la ‘Dou Dou na Visa vya Mama Wakwe zake’ itaanza kuonyeswa rasmi TBC 1 tarehe 23 mwezi huu wa kumi na moja.
Akizungumza na waandishi wa habari mkurugenzi mkuu wa TBC Mr Clemence Mshana alisema kuwa lengo kubwa la tamthiliya hiyo ni kuonyesha jinsi lugha adhimu ya Kiswahili inavyoweza kutumika moja kwa moja bila kuweka tafsiri za maandishi katika filamu au tamthiliya kuelezea utamaduni wa mataifa mengine.
Alisema kuwa kupita tamthiliya hii, ambayo inatarajiwa kuzinduliwa rasmi wiki ya mwisho wa mwezi huu wa November, itawasaidia wasanii wa Tanzania ninsi wanavyoweza kutengeneza tamthiliya nzuri zenye ubora na zikaweza kuuzwa nchi za nje na hivyo kukuza matumizi ya lugha ya Kiswahili nje ya Tanzania.
“ Vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kuitangaza lugha ya Kiswahili kwa kueleza jamii kuwa inatosheleza katika Nyanja mbali mbali za maisha ya binadamu bila kujali taifa lake,” alisema.






Friday, October 28, 2011

WASAMBAZAJI WANAZINGUA ASEMA ROSE...


MTAYARISHAJI na mwigizaji nyota wa filamu wa Bongo, Rose Ndauka, amesema kuwa filamu yake ya Diary imeshindwa kuingia sokoni mapema kwa sababu ya matatizo ya usambazaji.

Badala yake ameamua kuigiza filamu ya Ruben n� Angel wakati akijaribu kumtafuta msambazaji anayefaa.

Filamu ya Diary ilikuwa itoke mapema kabla ya filamu ya Ruben n� Angel, lakini kutokana na matatizo ya usambazaji ameamua kusitisha zoezi hilo. 


Mwanadada huyu ambaye anamiliki kampuni yake inayojulikana kwa jina la Rose Ndauka Entertainment, anatayarisha filamu zake mwenyewe pia na kushiriki filamu nyingine.

�Nilikuwa nimewaahidi wapenzi wa kazi zangu kuwa filamu ya Diary inatoka mwezi huu, na watu walikuwa wanasubiri kwa hamu itoke, lakini ratiba imebadilika badala yake nimetoa filamu nyingine ya Ruben n� Angel,� alisema Ndauka.

Filamu ya Ruben wameshiriki wasanii kama Khaleed Tajiri, Irene James, Ndauka na wasanii wengine filamu hiyo ipo mtaani ikiendelea kuuzwa.