BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Tuesday, September 27, 2011

Loveness afunguka kuhus mahusiano...


MUIGIZAJI wa filamu za Bongo, Loveness Watson amebainisha kuwa yeye katika maisha yake hapendi kabisa kuolewa kwani hawezi kuwa huru kama alivyo sasa.
Amesema kulingana na kazi yake ya utayarishaji wa filamu anaamini akiwa mke wa mtu hatapata fursa ya kufanya kazi zake zinamfanya akose muda wa kuwepo sehemu tofauti.
�sipendi kuolewa kabisa kutokana na ndoa za watu ninazoziona, lakini mimi kazi zangu za kushinda sana sehemu ambazo tunarekodi na kurudi muda wa usiku, mume gani atakubali kusubiri mke mwenye kazi nyingi hivyo? "Najikuta nashindwa kujigawa katika ya mume na kazi, sanaa naipenda ipo katika damu,� alisema msanii huyo.
Loveness aliwahi kudaiwa mara nyingi hujifanananisha na Rose Ndauka na hata kutumia jina la mwanadada huyo kwa ajili ya kujipatia sifa, lakini yeye anakataa jambo hilo na kusema kuwa hawezi kufanya hivyo, kwani kazi anazofanya Rose naye anafanya.
Msanii huyo ameigiza filamu kama Sheria Mkononi, Impossible Promise, Fake Love, Penzi la Utata, Blood in the City na Doctor Thomas.

Sunday, September 18, 2011

MSISIMKO WA FILAMU YA CPU UMEFIKA.

 Mmoja kati wasanii waliofika katika usahili wa filamu ya CPU.
ULE msimu wa mapinduzi ya tasnia ya filamu Tanzania unakuja, tunasema kuwa Msisimko wa CPU umefika, na tayari watu kila kona wanasubiri ili waone filamu ya kwanza Tanzania kurekodiwa kwa teknorojia ya kisasa kabisa, kama umepata kusikia habari hizi basi si filamu nyingine ni CPU.
Wasanii wakisubiri kuingia chumba cha usahili.
Timu ya wataalamu kutoka sehemu mbalimbali, wiki hii walikuwa na kazi kubwa kwa ajili ya kufanya usahili wa wasanii wenye sifa na muonekano wa kuigiza filamu ya CPU, timu hiyo tayari imeshawapata wasanii kadhaa na zoezi linaendelea chini ya usimamizi wa kampuni ya Haak Neel Production.
Akiongea na vyombo vya habari meneja masoko wa kampuni hiyo God Mahendeka amsema kuwa
“Wasanii wanaohitajika ni wengi na kuna wasanii ambao tayari wamepita katika usahili na kuanzia sasa timu iliyofanya kazi hiyo itaanza kutangaza majina ya wasanii waliopita katika usahili, na kuhusu vifaa kwa ajili ya urekodiji wa filamu hiyo vipo tayari, watalaamu wanasubiri tu kazi ianze, ” anasema God.
Filamu ya CPU ni filamu ya kwanza ambayo inatarajia kuonyeshwa katika majumba ya sinema Afrika Mashariki, filamu hiyo inashirikisha kampuni mbili kubwa za utayarishaji wa filamu yaani Haak Neel Production na Wegos works ltd, kuanzia sasa kila mara tembelea mtandao huu kupata habari za kusisimua kuhusu filamu ya CPU. USIKOSE!!

Habari hii ni kwa hisani ya filamucenteral.co.tz

Wednesday, September 14, 2011

WASANII WAONYWA KUHUSU MAKUNDI WANAYOFANYA YA KUPONDANA...

MSANII mwenye fani lukuki sokoni, Mshindo Jumanne amebainisha kuwa katika sakata linaloendelea sasa kuhusu maslahi ya wasanii tatizo lipo kwa Wasanii na si kwa Wasambazaji.
Mshindo ambaye pia husambaza filamu ambazo anazitengeneza mwenyewe na baadhi ya filamu za watayarishaji wengine alibainisha hayo kuwa mara nyingi wasanii wanajitenga na kutengeneza makundi ambayo yanapingana yenyewe kwa yenyewe badala ya kuwa na kauli ya pamoja.
Tatizo kubwa ni sisi wenyewe wasanii kwa sababu hatuna umoja ambao unaweza kutuongoza katika kuzalisha filamu zenye ubora huku tukipata maslahi kwa kila mhusika, kwa sasa hali ni mbaya kuliko awali maana unafanya kazi hata hauna uhakika wa kuuza filamu yenyewe.
"Kuna msambazaji mmoja tu mwenyewe nguvu ambaye analalamikiwa lakini watu wanasahau kuwa yeye ni mfanyabiashara na hakuna mtu anayefanya biashara kwa ajili ya mtu mwingine,alisema na kuongeza kuwa wasanii ambao ni nyota ndiyo kikwazo cha ukuaji wa tasnia ya filamu Bongo.
Anasema mara nyingi mtu akiandaa filamu na kuwashirikisha kwa sehemu chache hawataki bali huhitaji kucheza kila filamu kama ni waigizaji wakuu, jambo ambalo yeye anapingana nalo kwani haiwezekani muswada (script) umfuate msanii.

Wabongo wanammendea Funke Akindele...

INAWEZEKANA wabongo wamo pia. Mamia ya wanaume mabachela wamefumuka kutoka kila kona ya Nigeria na Afrika wakiomba kuwa na uhusiano wa kimapenzi na staa wa Nollywood, Funke Akindele.
Msanii huyo aliliambia gazeti moja maarufu jijini Lagos wiki iliyopita kwamba anahitaji mwanaume wa kumuoa na yuko tayari kwa yoyote atayejitokeza mwenye msimamo na anayeeleweka, ila akatoa angalizo kuwa awe anamuogopa Mungu. Habari hiyo ilichapishwa pia na kwenye ukurasa huu Jumanne iliyopita.
Kwa mujibu wa gazeti hilo, mabachela zaidi ya 200 kutoka nchi mbalimbali za Afrika wamepiga simu, kutuma barua pepe na ujumbe wa simu wakimuwania msanii huyo.
Katika orodha ya wanaume zaidi ya 200 iliyochapishwa kufikia juzi jioni, wengi wametoa namba zao za simu, ahadi na kila mmoja alikuwa akijinadi kwa maneno matamu na kuomba mawasiliano ya binti huyo.

Lucy.. kazi za sanaa zamkosesha muda wa kumuhudumia mtoto...


IMEKUWA furaha kwa wasanii wa kike pale wanapofanikiwa kupata mtoto au watoto ambapo wengi wao hupenda kuwahudumia watoto wao kwa asilimia kubwa.
Lengo ni kuweza kumpatia mtoto wake huduma anazostahili na kuweza kuwa karibu naye zaidi ingawa baadhi husema ni njia ya kujigamba kwa wengine.
Lakini kwa Msanii gwiji wa filamu Lucy Komba (31)amekuwa tofauti sana kwani yeye mtoto wake Strom Mbasha (2) anakosa muda mwingi wa kumhudumia kutokana na kutingwa na kazi hivyo mara nyingi anahudumiwa na wasichana wa kazi.
Wiki kati msanii huyo alizungumza kwa kirefu na mwandishi wa habari hii Minael Msuya kuhusu maisha yake nje ya sanaa.

Mwandishi: Wewe ni mama wa mtoto mmoja vipi, unamhudumiaje mtoto wako kabla ya kwenda kazini?
Lucy: Napenda kuwa mkweli siku zote, mimi naamka saa kumi na moja alfajiri hapo najiianda kwenda kazini, mwanangu anakuwa amelala bado. Hivyo sina ninachomuandalia.

Mwandishi: Kwa hiyo mtoto wako anahudumiwa na nani kama wewe unapoamka hufanyi shughuli yoyote tena ukizingatia bado mdogo?
Lucy: Pale nyumbani tuna wasichana wawili wa kazi, mmoja ni maalumu kwa kumhudumia mtoto na mwengine anafanya kazi zingine hivyo mwanangu anahudumiwa zaidi na wasichana wa kazi.
Mwandishi: Hujisikii vibaya mwanao anavyohudumiwa na wasichana hao,

Lucy: Nammis sana mwanangu na ninampenda zaidi hivyo jioni ninaporudi nyumbani na siku za mapumziko namhudumia muda wote, kwani napenda nimhudumie mwanandu wakati wote mwenyewe isipokuwa kazi zinanibana.
Mwandishi: Kwani unafanya shughuli gani zaidi mpaka ukose muda wa kumhudumia mwanao?
Lucy: Kama unavyoniona hapa ofisini, mimi ni Katibu Muhtasi katika Mahakama Kuu ya Tanzania, muda wangu unabana sana hata baadhi ya kazi zangu za sanaa nashindwa kuzimudu.

Mwandishi: Una muda gani na kazi yako hii, vipi kuhusu familia yako inakutegemeaje?
Lucy: Muda mrefu kidogo nilianza hapa tangu mwaka 2003, kwenye familia kwa kweli nahudumia kawaida, mama yangu ndiye anayeitunza familia na kwa sasa bado niko chini ya himaya ya mama yangu siwezi kujigamba kwa chochote.

Mwandishi: Baba wa mtoto unaishi naye au vipi?
Lucy: Siishi na mume hata hivyo sina mpango wa kuishi naye kwa sasa labda baadaye sana.
Mwandishi: Matarajio yako baadaye ni yapi?
Lucy: Matarajio yangu ni kuwa msanii na mtunzi mahiri wa kimataifa ili niweze kuonyesha kipaji change na kuongeza kipato changu zaidi ili familia yangu hasa watoto wangu niweze kuwahudumia na kupata elimu bora.

Mwandishi: Tofauti na sanaa unamatarajio gani mengine?
Lucy: Mh! Mimi naipenda kazi yangu ya uigizaji zaidi hata hii niliyonayo ni kwa sababu tu nimesomea lakini nafikiria kuifanya sanaa kuwa kazi yangu pekee na nitafanya ndani na nje ya nchi. Naamini ndoto yangu itakuwa imetimia kwani hivi sasa sanaa inakuwa kwa kiwango kizuri na ninapenda kuibua vipaji vya wasanii wengi zaidi kama ilivyokuwa kwa wasanii mahiri na wanaokubalika Mzee Chilo, Iren Uwoya, Mkwere na wengine wengi.
Mwandishi: Nikitu gani ambacho usipokifanya kwa siku unaona kama hujafanya kazi siku hiyo?
Lucy: Dah! Nimelipenda swali lako maana umeigusa mboni ya jicho langu, napenda sana kuandika na kufikiria stori mpya kichwani na kuiandaa. Kila siku moja najitahidi niandike japo mistari kadhaa ya stori zangu ili niweze kuandaa filamu zangu na kazi yangu isidumae, nisipofanya hivyo kwangu sioni kama siku  imeisha hii ni kwasababu naipenda kazi ya uigizaji kuliko vitu vingine vyote.
Mwandishi: Maishani mwako unampango wa kumiliki kitu gani ambacho unaona kitakuwa na manufaa kwako?
Lucy: Ninampango wa kumiliki nyumba ya ghorofa moja, tayari nimeanza ujenzi wa nyumba nyangu hiyo maeneo ya Bunju. Wasanii wengi wa bongo wanapenda ufahari wa magari mimi nahitaji kuwa na gari aina ya sports nafikiri litanisaidia kwa shughuli zangu.  
Mwandishi: Je ungependa kuwa na watoto wangapi na mume atakayekuoa awe na vigezo gani?
Lucy: Napenda Mungu akinisaidia niwe na watoto watatu, pia mume wangu asiwe na tabia chafu, anizidi mimi urefu, awe mweupe, mtanashati, mpole na mwenye uwezo wa kutunza familia.   


Saturday, September 10, 2011

'UNPREDICTABLE' coming soon...


Katika hali ya kuonekana kukua kwa fani ya filamu Tanzania wasanii mbali mbali wamekuwa wakifanya jitihada katika kuhakikisha wanatoa kazi mpya mara kwa mara ili kuweza kuliteka soko la filamu Tanzania kikamilifu.
Msanii Vicent kigosi ama Ray ni mmoja wa wasanii hao ambao katika kila hali wanajitahidi kipiga hatua ili kuhakikisha soko hili linabaki katika hali ya kuwapatia faida wanapofanya kazi zao.
Hivi karibu alikuwa chimbo kuandaa filamu yake mpya na kwa mujibu wa blog yake filamu yake iko katika hatua za mwisho na inatarajiwa kutoka hivi karibuni.
Filamu hiyo mpya itakayo toka soon itajulikana kwa jina la UNPREDICTABLE (Chagua la mama).


Thursday, September 8, 2011

MURPHY KU-HOST TUZO ZA OSCAR



Msanii na mchekeshaji kutoka nchini Marekani Eddie Murphy anatarajiwa ku- host event mojawapo kubwa sana ambayo hutokea kila mwaka ya tuzo za filamu ya Oscar 8th Movie Awards inayotarajiwa kufanyika mwezi February.
Event hiyo ambayo itarushwa na zaidi ya televisheni 200 duniani inatarajiwa kufanyika mwezi huo tarehe 26 katika maeneo ya Hollywood’s Kodak theatre nchini humo.

Muphy ambaye alianza kuigiza filamu za vichekesho akiwa na umri a miaka 15, na alipofikia umri wa miaka 19 aliibuka kinara mwenye umri mdogo katika kipindi cha tamthiliya cha televisheni kijulikanacho kama “Saturday Night Live" miaka ya 1980.

Aliingia rasmi katika filamu miaka ya 1982's alipotoka na "48 Hrs." na ilifatiwa na filamu ya "Beverly Hills Cop" na "The Nutty Professor" na "Shrek" franchises. Muvi za Murphy zimempatia kiasi cha zaid ya $7 billion katika mauzo ya box offices duniani, kwa mujibu wa Academy's news release.




HARAMBEE YA MSAIDIE MZEE KIPARA YAANZISHWA


Unamfahamu msanii mkongwe anayekwenda kwa jina la Mzee Kipara, kama ni hivyo basi tunahitaji kumsaidia mzee wetu amekuwa akisumbuliwa miguu kwa muda mrefu sana kwa kifupi Mzee wetu anasumbuliwa na magonjwa mengi ila kwa sasa ni miguu ndio inayomsumbua sana kutoa ni moyo wa wala si utajiri mimi kwa upande wangu nitajitoa kwa hali na mali lakini pia bado tunaomba misaada kutoka kwa wasamalia wema kampuni Global Publisher iliweza kumpa cm ili haweza kutumia kwa njia ya M PESA ili iweze kumsaidia kwa urahisi zaidi namba ni 0753 923454 Asanteni sana

Wednesday, September 7, 2011

MASAWE MTATA APANIA KUFANYA KWELI..

MSANII wa maigizo ya vichekesho ( The Commedy) Rogers  Richard a.k.a. Masawe Mtata amesema atahakikisha anafanya vizuri katika kazi yake ili kipindi cha The commedy kinachorushwa na EATV kiwavutie zaidi watazamaji.
Mtata, ambaye anashika nafasi ya pili katika igizo la komedi linalorushwa na Televisheni ya East Afrika kama wasemavo wapenzi wa kipindi hicho.

“Naipenda sana kazi yangu, hii ni kutokana na harakati mbalimbali nilizopitia katika kuhakikisha kuwa namimi natoka kimaisha.Nitahakikisha nafanya kila mbinu ambayo itaweza kufanya mabadiliko ya hapa na pale lengo likiwa ni kukiboresha kipindi chetu,” anasema.
Mtata anasema, kazi ya kuigiza kwa vichekesho inahitaji ubunifu mkubwa na kwamba wasanii wengi hawatambui ubunifu huo.
“Hili ni tatizo kubwa kwa wasanii kwa kuwa sisi wasanii tunapenda umaarufu wa magari tu bila kutambua kuwa tunatakiwa kuwa wabunifu katika kazi zetu,” anasema.
Aidha Mtata anasema, wasanii wanatakiwa kujiamini katika kila fani ili waweze kufikisha ujumbe kwa jamii kwa njia mbalimbali.
Mtata anasema, mbali na kuwa msanii wa komedi pia ni mwanamuziki na tayari ameandaa albamu yake itakayotambulika kwa jina la ‘Swaga za Kichaga’.
Akitoa ushauri kwa wasanii wenzake, anasema wasanii waboreshe ushirikiano ili waweze kuimarisha Industry ya sanaa.

Sunday, September 4, 2011

KAZI MPYA KUTOKA KWA FADHILI...

 Fadhili Maogola kwnye action na Rose ndauka
 haya ni maandalizi ya mwisho mwisho kutoka kwa D production... hapo ni fadhil akiwa na Hemed ... filamu hiyo inakaribia kuwa sokoni soon na info zaidi utazipata hapa hapa.
Yusuph Mlela, fadhili na wasanii wengine wa filamu