BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Saturday, October 15, 2011

Aunt Ezekiel asema hajafungiwa...


BAADA ya uvumi wa kufungiwa kwa mwigizaji Aunty Ezekiel kuenea , mwenyewe amefunguka na kusema kuwa huo ni uvumi tu ambao hata yeye amekuwa akiusikia tu bila kujua chanzo chake.

“Sijui nani aliyeanzisha habari hizi, lakini mimi sijafungiwa na sasa ninapozungumza na wewe nipo mzigoni nikiandaa filamu yangu mpya ambayo nitaiingiza sokoni muda si mrefu,” alisema Aunty.

Aunty amesema filamu yake hiyo itaitwa House Boy and House Boy na itakuwa ikielezea maisha ya kila siku ya wafanyakazi wa ndani.

Mwenyekiti wa Bongo Movie, Jacob Steven amesema umoja wao huo haukumfungia kuigiza, bali asingeruhusiw akufanya kazi na msanii yoyote wa umoja huo.

Hata hivyo alisema Aunty ameshajirekebisha kwahiyo anaweza kuendelea na kazi kama kawaida.

Hata hivyo kufungiwa kwa Aunty kuna leta utata kutokana na waigizaji kuwa na vyama mbalimbali ambvyo mpaka sasa hakijukani kipi chenye nguvu ya kuweza kumfungia msanii.

Kipindi cha nyuma kulikuwa na shirikisho la wasanii wa filamu TAFF ambalo inasemekana liliundwa baada ya serikali kuamuru uundwe umoja utakaowawakilisha kwenye shughuli mbalimbali.

Baadae ukaundwa umoja huu uitwao Bongo Movie ambao wasanii wengine wanadai kutoutambua kutokana na mazingira yake nakusema kuwa umeundwa kwaajili ya maslahi ya wasanii wachache.

No comments:

Post a Comment