BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Friday, October 28, 2011

WASAMBAZAJI WANAZINGUA ASEMA ROSE...


MTAYARISHAJI na mwigizaji nyota wa filamu wa Bongo, Rose Ndauka, amesema kuwa filamu yake ya Diary imeshindwa kuingia sokoni mapema kwa sababu ya matatizo ya usambazaji.

Badala yake ameamua kuigiza filamu ya Ruben n� Angel wakati akijaribu kumtafuta msambazaji anayefaa.

Filamu ya Diary ilikuwa itoke mapema kabla ya filamu ya Ruben n� Angel, lakini kutokana na matatizo ya usambazaji ameamua kusitisha zoezi hilo. 


Mwanadada huyu ambaye anamiliki kampuni yake inayojulikana kwa jina la Rose Ndauka Entertainment, anatayarisha filamu zake mwenyewe pia na kushiriki filamu nyingine.

�Nilikuwa nimewaahidi wapenzi wa kazi zangu kuwa filamu ya Diary inatoka mwezi huu, na watu walikuwa wanasubiri kwa hamu itoke, lakini ratiba imebadilika badala yake nimetoa filamu nyingine ya Ruben n� Angel,� alisema Ndauka.

Filamu ya Ruben wameshiriki wasanii kama Khaleed Tajiri, Irene James, Ndauka na wasanii wengine filamu hiyo ipo mtaani ikiendelea kuuzwa.


No comments:

Post a Comment