BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Tuesday, November 16, 2010

FILAMU YA BEAUTIFULLY KUTOKA TUESDAY ENTERTAINMENT.


KAMPUNI ya Tuesday Entertainment inakuja na filamu inayokwenda kwa jina la Beautifully filamu hii imeshirikisha wasanii wakali kama Charles Magali (Mzee Magali) na mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Bongo fleva Rehema Chalamila (Ray C).

“Ray C mzigo aliopiga katika filamu hii ni simulizi hata mimi sikujua kama mwanadada huyu anauwezo mkubwa namna hii katika uigizaji, ameigiza katika kiwango cha juu sana, na inawezekana akawa tishio zaidi kwa waigizaji wa kike”
Alisema mkurugenzi wa kampuni hiyo Mr. Chuzi.

Filamu imechezwa na Suddy, Asnat, Tony na Mr. Chuzi mwenyewe imerekodiwa Matombo Mkoani Morogoro, filamu hii inayosubiriwa kwa hamu na watazamaji inatarajiwa kutoka mwezi ujao na kusambazwa na kampuni ya Steps Entertanment.

No comments:

Post a Comment