BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Thursday, November 25, 2010

FILAMU YA OFF SIDE YAWAKUTANISHA MASWAHIBA WAWILI RAY THE GREATEST NA KANUMBA THE GREAT; JE NANI MKALI??



KATIKA tasnia ya filamu hapa nchini majina ya Kanumba na Ray yamekuwa ni majina yaliyozoeleka katika ulingo huu mahili ambao kwa hivi sasa unachukua sura mpya kwa kuweza kushika sana kupitia kazi zao wasanii hawa pia wasanii wengine mbali mbali wanaojihusisha na tasnia hii.

Kitu ambacho watu wengi hujiuliza kwa sasa ni yupi msanii mkali kuzidi mwenzake baina ya wasanii hawa wawili yaani Kanumba pamoja na Ray kigosi kwani wasanii hawa wamekuwa wakifanya vizuri katika fani hii na pia ni maswahiba ambao walianza kazi katika kitovu cha sanaa cha Kaole sanaa group kwa pamoja hivyo ni watu waliopitia njia nyingi hadi kufika hapo walipo ambapo kila mmoja anamiliki kampuni yake binafsi. Kanumba anamiliki kampuni yake inayojulikana kama Kanumba the great film pia Ray nae ana miliki kampuni yake walioshirikiana na johari inayojulikana kama RJ company.

Majibu ya maswali hayo ya wadau wa tasnia hii juu ya ukweli kuwa nani ni mkali yanajibika katika filamu inayotarajiwa kutoka hivi karibuni ambayo ndani yake vichwa hivyo viwili vimeshiriki. Filamu ya OFF SIDE ni moja ya filamu ambayo imeandaliwa chini ya kampuni ya Kanumba na ina vichwa vingine vikali kama Johari, na JB ambao pia ni waasisi wa filamu hapa TZ na wameshafanya kazi kibao kwa pamoja lakini hii ni kali kwa imewakutanisha maswahiba hawa wawili pamoja na mastaa wengine.

Sijui kwa upande wako ni nani mkali? Ila kwangu nasubili nione filamu hiyo ndipo nitoe maoni yangu ila kwa sasa nawakubali wote kwa kazi kali wanazozifanya.

No comments:

Post a Comment