BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Sunday, December 4, 2011

MATANGAZO YA BIASHARA HAYA LIPI.... Ray

NYOTA katika tasnia ya filamu Bongo, Vincent Kigosi (Ray), amesema matangazo ya biashara hayalipi na ndiyo maana hashiriki katika kutengeneza matangazo hayo kwa sababu hayana faida kwake.

Si kama sipati matangazo ya biashara kwa ajili ya kutangaza bidhaa, fedha wanayotoa wahusika ni ndogo sana kiasi cha kukatisha tamaa, siwezi kutumika katika matangazo kwa pesa ndogo wakati nikitengeneza filamu naipata zaidi ya hiyo, alisema Ray.

Kwa wale wanaopenda sifa za kuonekana bila faida waache tu wafanye, lakini mimi msimamo wangu upo kimaslahi zaidi.

Msanii huyo alisema kuwa tatizo la matangazo hayo pamoja na kuwa malipo ni kidogo, lakini hayana ukomo wa muda wa kutumika. 

Mwenye bidhaa husika ana uwezo wa kulitumia hata milele bila kuendelea na malipo mengine, sasa hii si halali kabisa, aliongeza.

Mara nyingi makampuni hunifuata, lakini kila linapofika suala la malipo na ukomo wa tangazo wanakimbia, kuna tangazo ilitakiwa nilifanye, lakini baada kuambiwa kuwa nitalipwa dola 2,500 (Sh 223,864 za Kenya) na litatumika milele bila malipo ya ziada nilikataa.

Msanii huyo alisema kama kuna kampuni inataka kufanya kazi naye anaikaribisha, lakini ikubali kutimiza masharti yake kwa kuwa na mkataba unaoeleweka na si wa kuuza sura.

No comments:

Post a Comment