BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Sunday, December 4, 2011

SAJUKI AFUNGUKA KUGAWANYIKA KWA WASANII...

MWIGIZAJI na mwongozaji wa filamu Bongo, Juma Kilowoko Sajuki, amesema watayarishaji wa filamu wamegawanyika katika makundi, ingawa ni vugumu mwingine kulibaini hilo.

Akizungumza na jukwaa hili nyumbani kwake Tabata Bima, jijini Dar es Salaam, msanii huyo ambaye kwa sasa anasumbuliwa na tumbo, anasema kuwa mara nyingi wale ulio karibu nao ndiyo hukuzunguka.

Sisi wasanii tayari tuna makundi japo tunafanya kazi moja, kwa mfano mimi rafiki zangu labda Frank au Dino, basi watakuwa ni hao tu, hata linapotokea jambo kama la msaada wao ndiyo watawajibika, alisema.

Hata kama mtu akiongea na mwingine atasema kuwa huyu jamaa hajichanganyi na watu, lakini ukweli tunajuana kuwa kila mtu na mtu wake. Msanii huyo alisema japo jambo hilo lipo, lakini si rahisi kuyataja makundi hayo. Kutokana na hali hiyo, anawataka wasanii kujilazimisha kujenga umoja wa kweli kuliko ilivyo sasa.

No comments:

Post a Comment