BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Tuesday, December 6, 2011

Ramsey awaasa wasanii wa muvi bongo..


VIPAJI vina nafasi kubwa katika ulimwengu wa sanaa, lakini kuna wakati lazima mhusika atafute elimu kwa ajili ya kulinda na kuendeleza kipaji chake.

Hayo ni maneno ya mwigizaji mahiri wa filamu Bongo, Hashim Kambi Ramsey aliyoyatoa hivi karibuni katika mazungumzo yake na Mwanaspoti.

Wakati naanza kuigiza nilikuwa najua ni kitu cha kujifurahisha tu, nilifanya hivi huku nikiendelea na shughuli nyingine, anasema Ramsey.

Lakini nimebaini uigizaji ni kazi. Inakuhitaji mtu uwe na taaluma hiyo ili uweze kudumu nayo katika kiwango bora.

Kinachosikitisha tu ni kuwa kuna hili tatizo la gharama kuwa kubwa kwa masomo ya filamu.

Akielezea zaidi, anasema kwamba wasanii wanaweza kujiendeleza kwa njia ya mitandao ya filamu, kama anavyofanya yeye.

No comments:

Post a Comment