BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Wednesday, December 8, 2010

Esther Flavian Mwanadada nyota chipukizi kutoka D production

Huyu ni mwanadada chipukizi katika tasnia ya filamu na amezidi kuwa kinara katika filamu tofauti tofauti hasa filamu iliyotoka hivi karibuni kutoka katika kampuni ya D production ijulikanayo kama AUNT SUZZY na nyingine nyingi. Pia Esther ni moja ya Video Queen wa nyimbo mbali mbali kama wimbo wa Sam ujulikanao kama Sina Raha, pia wimbo wa Dullayo uitwao Naumia roho.

Akizungumza na blog hii Esther ametoa mawazo yake kuhusiana na tasnia hii kuwa "ubovu wa filamu unaolalamikiwa hivi sasa na mashabiki wa sanaa hiyo nchini unatokana na tamaa ya waandaji wa ‘filamu’ hizo kutaka kupata ‘fedha ’ za haraka haraka." Aliongeza kwa kusema malalamiko ya mashabiki juu ya kutoeleweka kwa hadithi za filamu za Kibongo wanayopata hivi sasa unatokana na utayarishaji wa kukurupuka unaofanywa na waandaaji kwa lengo la kuingiza mkwaja haraka haraka jambo ambalo linafanya kazi hizo kukosa ubora.. asema Esther.
Kati ya filamu alizocheza kupitia D production ni pamoja na hiyo ya Aunty Suzzy, Fake pregnant, Where is Love na nyingine kibao chini ya mtayarishaji na muigizaji daudi michael..
 

No comments:

Post a Comment