BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Monday, December 6, 2010

GAME 1st QUALITY kuja na MORNING ALARM.

Wakati akiendelea kutesa hivi sasa na Uncle JJ, mkali wa filamu Bongo Steve Kanumba anatarajiwa kuiteka tena tasnia ya filamu Bongo na muvi yake nyingine iliyopewa jina la Morning Alarm. Katika filamu hiyo, Kanumba anashirikiana na 'mchizi' Benny, kijana ambaye anasifika kwa kuigiza filamu za comedy na ujambazi.

Katika muvi hiyo kuna mastaa wengine kibao kama vile Hashim Kambi, Maya, Flora Mvungi, mwanamuziki Patcho Mwamba na wengine wengi Ikiwa ni kazi nyingine makini kutoka chini ya Kampuni ya Game1st Quality, filamu hii inatarajiwa kuliteka soko la muvi itakapoingia mtaani hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment