BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Sunday, December 5, 2010

Kutoka Udereva teksi hadi msanii na mwandaaji wa filamu


*Anatingisha na filamu za ‘Fake Pregnant’ Where Is Love, na sasa ‘Aunt Suzzy’.

WASANII nchini wataneemeka na kufaidi matunda ya kazi zao za filamu nchini ni pale tu watakapoamua kutoa kazi zilizo na ubora, utashi kwa jamii ikiwemo kufikisha ujumbe wa haraka na mpangilio sahihi wa filamu yenyewe.
Hayo ni maneno yake msanii na mwandaaji wa filamu anayekuja kwa kasi kubwa hapa nchini, Daud Michael, anayetamba na filamu za ‘ Upside Down’, ‘Where Is Love’, ‘Fake Pregnant’ na filamu ambayo tayari iko madukani, iliyojaa mastaa kibao ya ‘Aunt Suzzy’.
Emmed Hamis ‘Ramsey wa bongo’, Ester Flavian,Daud Tairo Michael, na Raulant Anthon ‘makala’
Hivi sasa msanii Daud Michael anamiliki studio yake ya kisasa ijushughulishayo na uandaaji wa filamu mbalimbali hapa nchini inayofahamika kama ‘D Production, iliyopo maskani ya Mabibo Makutano jijini Dar es Salaam.
Daud anasema kuwa mpaka alipofikia ni safari ndefu katika tasnia hiyo ya sanaa kwani aliweza kupita milima na mabonde kama wasemavyo waswahili mpaka kufika hapo alipo na kuwa na kampuni yake hiyo sambamba na kutoa filamu zake ambazo jamii wamezikubali.

No comments:

Post a Comment