BAADA ya kufanya vizuri katika filamu ya Blue Monday, muandaaji wa filamu hiyo, Abui Ahmed amewataka wapenzi wa filamu nchini kukaa tayari kwa ujio wa filamu mpya itakayokwenda kwa jina la Lost Hope.
Ahmed ambaye pia ni Mkurugenzi wa Abui Production alisema kuwa filamu hiyo iliyobeba ujumbe mzito wa familia na mapenzi kwa ujumla itakuwa sokoni mapema wiki ijayo.
“Filamu hii imebeba ujumbe mzito ambao nina uhakika utaelimisha jamii kwa ujumla na vilevile kumfanya kila mtu ajifunze kwa nafasi yake kutokana na kile kilichopo ndani ya filamu hii”alisema Ahmed.
Aliwataja wasanii walioshiriki katika filamu hiyo ni pamoja na Michael Philipo (Kojack) ,Nila Sultani (Jasmin) ambao ni wahusika wakuu na wengine ni Flora Mvungi,Mainda,Abdala Agosi, Badi pamoja na wengine wengi.
Abui Production imehusika kuandaa filamu mbalimbali zikiwemo Zindiko,Tension of Love na Blue Monday ambayo inafanya vizuri katika soko la filamu nchini.
WAZIRI WA UJENZI MHE. ULEGA AIPA KONGOLE ETDCO KWA UTEKELEZAJI BORA
MIUNDOMBINU YA UMEME
-
*Waziri wa Ujenzi, Mhe. Abdallah Ulega, ameipongeza Kampuni ya ETDCO kwa
umahiri na weledi katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi, ukarabati na
usambazaj...
6 days ago
No comments:
Post a Comment