BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Wednesday, May 2, 2012

CLOUD KATIKA HARAKATI ZA UZINDUZI WA TOBA

 Cloud.
MWIGIZAJI na Mtayarishaji wa filamu Swahiliwood Issa Mussa ‘Cloud 112’ yupo katika maandalizi ya kuzindua filamu yake mpya inayokwenda kwa jina la Toba uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Salama uliopo Zanzibar tarehe 18/05/2012 siku ya Ijumaa.
Cloud anakuwa ni msanii wa kwanza kwa mwaka huu kufanya tamasha kwa ajili ya uzinduzi wa filamu yake hiyo ya Toba baada ya utaratibu huo kusimama kwa muda mrefu kidogo, kwani siku hizi filamu zikitengenezwa zinaingizwa sokoni moja kwa moja bila kufanyiwa uzinduzi.
Filamu ya Toba imeshirikisha wasanii nyota kama Suleiman Barafu, chiki, Sandra, Eshe, Bi. Hindu na wasanii wengine wakali katika tasnia ya filamu Swahiliwood hongera kwa Cloud 112 kwa kufanya uzinduzi wa filamu yake

No comments:

Post a Comment