BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Friday, June 24, 2011

FILAMU YA GLAMOUR (The Reality Behind Dreams) KURUKA ZIFF 26 JUNE 2011.


KAMPUNI mahiri katika masuala ya utengenezaji filamu kwa hapa nchini ya ZG Films Usiku wa tarehe 26 mwezi huu wa sita 2011 kuanzi muda wa saa moja na robo , filamu yake ya Glamour: (The Reality Behind Dreams) itaonyeshwa katika tamasha hili la filamu la ZIFF na kuzinduliwa rasmi na kushuhudiwa na wageni mbalimbali wanaudhuria tamasha hili wakiwa wametoka nchi mbalimbali kutoka sehemu kubwa ya Ulimwengu huu.

ZG Films – Nyumba inayozalisha bidhaa bora za filamu Zanzibar ikiongozwa na mpiga picha mashuhuri na mtengenezaji wa filamu, Javed Jafferji – tayari ameshazindua taarifa kadhaa zinazohusiana na masuala muhimu na matukio ya visiwa vya Zanzibar na Tanzania. Hivi karibuni amezindua Journey to the State House: The Life of Seif Shariff Hamad ikiwa na maana ya Safari ya Ikulu: Maisha ya Seif Shariff Hamad, ambayo itakuwa toleo la mwanzo katika Tamasha la ZIFF 2011(Zanzibar International Film Festival) ambayo imeingia kwa ajili ya tuzo ya filamu bora katika tamasha hilo.

ZG Films ikiwa na lengo la kuangalia athari na ufikaji wa sekta ya filamu Tanzania, ina lengo la kuwafikishia watu kimataifa, kwa kuweka kiwango cha kimataifa katika sekta hiyo hapa Tanzania. Katika kutimiza lengo hili, ZG Films and Media House, wakishirikiana na Zanzibar International Film Festival, inatoa, filamu ya Glamour (The Reality Behind Dreams)
Filamu hii imetayarishwa na Javed Jafferji na kuongozwa na Amitabh Aurora, Glamour: The Reality Behind Dreams ni filamu ya kwanza ya ZG Films and Media House, ni filamu ya Bongo ya Kisasa ikihamasishwa na Swahili Fashion Week – Tukio kubwa Tanzania linalohusiana na uwanamitindo, na kutoa ukweli juu ya sekta ya uwanamitindo, Mhusika mkuu katika filamu hii sio mwengine bali ni Eva Issac (aka “Eva ya Diva”), mmoja kati ya wanamitindo wakubwa Tanzania.

No comments:

Post a Comment