BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Tuesday, September 27, 2011

Loveness afunguka kuhus mahusiano...


MUIGIZAJI wa filamu za Bongo, Loveness Watson amebainisha kuwa yeye katika maisha yake hapendi kabisa kuolewa kwani hawezi kuwa huru kama alivyo sasa.
Amesema kulingana na kazi yake ya utayarishaji wa filamu anaamini akiwa mke wa mtu hatapata fursa ya kufanya kazi zake zinamfanya akose muda wa kuwepo sehemu tofauti.
�sipendi kuolewa kabisa kutokana na ndoa za watu ninazoziona, lakini mimi kazi zangu za kushinda sana sehemu ambazo tunarekodi na kurudi muda wa usiku, mume gani atakubali kusubiri mke mwenye kazi nyingi hivyo? "Najikuta nashindwa kujigawa katika ya mume na kazi, sanaa naipenda ipo katika damu,� alisema msanii huyo.
Loveness aliwahi kudaiwa mara nyingi hujifanananisha na Rose Ndauka na hata kutumia jina la mwanadada huyo kwa ajili ya kujipatia sifa, lakini yeye anakataa jambo hilo na kusema kuwa hawezi kufanya hivyo, kwani kazi anazofanya Rose naye anafanya.
Msanii huyo ameigiza filamu kama Sheria Mkononi, Impossible Promise, Fake Love, Penzi la Utata, Blood in the City na Doctor Thomas.

No comments:

Post a Comment