BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Wednesday, September 14, 2011

Wabongo wanammendea Funke Akindele...

INAWEZEKANA wabongo wamo pia. Mamia ya wanaume mabachela wamefumuka kutoka kila kona ya Nigeria na Afrika wakiomba kuwa na uhusiano wa kimapenzi na staa wa Nollywood, Funke Akindele.
Msanii huyo aliliambia gazeti moja maarufu jijini Lagos wiki iliyopita kwamba anahitaji mwanaume wa kumuoa na yuko tayari kwa yoyote atayejitokeza mwenye msimamo na anayeeleweka, ila akatoa angalizo kuwa awe anamuogopa Mungu. Habari hiyo ilichapishwa pia na kwenye ukurasa huu Jumanne iliyopita.
Kwa mujibu wa gazeti hilo, mabachela zaidi ya 200 kutoka nchi mbalimbali za Afrika wamepiga simu, kutuma barua pepe na ujumbe wa simu wakimuwania msanii huyo.
Katika orodha ya wanaume zaidi ya 200 iliyochapishwa kufikia juzi jioni, wengi wametoa namba zao za simu, ahadi na kila mmoja alikuwa akijinadi kwa maneno matamu na kuomba mawasiliano ya binti huyo.

No comments:

Post a Comment