BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Sunday, September 18, 2011

MSISIMKO WA FILAMU YA CPU UMEFIKA.

 Mmoja kati wasanii waliofika katika usahili wa filamu ya CPU.
ULE msimu wa mapinduzi ya tasnia ya filamu Tanzania unakuja, tunasema kuwa Msisimko wa CPU umefika, na tayari watu kila kona wanasubiri ili waone filamu ya kwanza Tanzania kurekodiwa kwa teknorojia ya kisasa kabisa, kama umepata kusikia habari hizi basi si filamu nyingine ni CPU.
Wasanii wakisubiri kuingia chumba cha usahili.
Timu ya wataalamu kutoka sehemu mbalimbali, wiki hii walikuwa na kazi kubwa kwa ajili ya kufanya usahili wa wasanii wenye sifa na muonekano wa kuigiza filamu ya CPU, timu hiyo tayari imeshawapata wasanii kadhaa na zoezi linaendelea chini ya usimamizi wa kampuni ya Haak Neel Production.
Akiongea na vyombo vya habari meneja masoko wa kampuni hiyo God Mahendeka amsema kuwa
“Wasanii wanaohitajika ni wengi na kuna wasanii ambao tayari wamepita katika usahili na kuanzia sasa timu iliyofanya kazi hiyo itaanza kutangaza majina ya wasanii waliopita katika usahili, na kuhusu vifaa kwa ajili ya urekodiji wa filamu hiyo vipo tayari, watalaamu wanasubiri tu kazi ianze, ” anasema God.
Filamu ya CPU ni filamu ya kwanza ambayo inatarajia kuonyeshwa katika majumba ya sinema Afrika Mashariki, filamu hiyo inashirikisha kampuni mbili kubwa za utayarishaji wa filamu yaani Haak Neel Production na Wegos works ltd, kuanzia sasa kila mara tembelea mtandao huu kupata habari za kusisimua kuhusu filamu ya CPU. USIKOSE!!

Habari hii ni kwa hisani ya filamucenteral.co.tz

No comments:

Post a Comment