BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Wednesday, September 14, 2011

WASANII WAONYWA KUHUSU MAKUNDI WANAYOFANYA YA KUPONDANA...

MSANII mwenye fani lukuki sokoni, Mshindo Jumanne amebainisha kuwa katika sakata linaloendelea sasa kuhusu maslahi ya wasanii tatizo lipo kwa Wasanii na si kwa Wasambazaji.
Mshindo ambaye pia husambaza filamu ambazo anazitengeneza mwenyewe na baadhi ya filamu za watayarishaji wengine alibainisha hayo kuwa mara nyingi wasanii wanajitenga na kutengeneza makundi ambayo yanapingana yenyewe kwa yenyewe badala ya kuwa na kauli ya pamoja.
Tatizo kubwa ni sisi wenyewe wasanii kwa sababu hatuna umoja ambao unaweza kutuongoza katika kuzalisha filamu zenye ubora huku tukipata maslahi kwa kila mhusika, kwa sasa hali ni mbaya kuliko awali maana unafanya kazi hata hauna uhakika wa kuuza filamu yenyewe.
"Kuna msambazaji mmoja tu mwenyewe nguvu ambaye analalamikiwa lakini watu wanasahau kuwa yeye ni mfanyabiashara na hakuna mtu anayefanya biashara kwa ajili ya mtu mwingine,alisema na kuongeza kuwa wasanii ambao ni nyota ndiyo kikwazo cha ukuaji wa tasnia ya filamu Bongo.
Anasema mara nyingi mtu akiandaa filamu na kuwashirikisha kwa sehemu chache hawataki bali huhitaji kucheza kila filamu kama ni waigizaji wakuu, jambo ambalo yeye anapingana nalo kwani haiwezekani muswada (script) umfuate msanii.

No comments:

Post a Comment