BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Saturday, April 14, 2012

BABA MZAZI WA LULU AFUNGUKA...


BABA mzazi wa Muigizaji wa kike wa filamu nchini maarufu kama Lulu, ambaye anahusishwa na kifo cha marehemu Steven Charles Kanumba, ameibuka na kueleza kushtushwa sana na taarifa za kifo hicho pamoja na habari kuwa bintiye alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na muigizaji huyo nguli na kuwa anahusika na kifo chake. Baba Lulu, ambaye alijitambulisha kwa jina la Michael Edward Kimemeta (49) mzaliwa wa Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro 

BABA mzazi wa Muigizaji wa kike wa filamu nchini maarufu kama Lulu, ambaye anahusishwa na kifo cha marehemu Steven Charles Kanumba, ameibuka na kueleza kushtushwa sana na taarifa za kifo hicho pamoja na habari kuwa bintiye alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na muigizaji huyo nguli na kuwa anahusika na kifo chake.
Baba Lulu, ambaye alijitambulisha kwa jina la Michael Edward Kimemeta (49) mzaliwa wa Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro, kaiambia Globu ya Jamii leo huko Moshi kuwa alimtambua Steven Kanumba kama mwalimu wa mtoto wake Lulu, lakini hakuamini masikio yake baada ya kupata taarifa za kifo hicho, huku bintiye, anayedaiwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na marehemu, anahusika.
Lulu alifikishwa mahakamani juzi Aprili 11, 2012 akikabiliwa na mashtaka ya mauaji ya Marehemu Steven Kanumba, ikiwa ni siku nne baada ya kifo cha msanii huyo.
Alisema kuwa Elizabeth ama Lulu alizaliwa tarehe April 17,1995 katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam, na kwamba alimaliza elimu ya kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya Midway mwaka jana na kwamba hivi sasa ana umri wa miaka 17.
Bw. Kimemeta alisema kuwa ni vyema polisi kuwa makini katika uchunguzi wao kwa kuzingatia kuwa tukio hilo limejenga chuki na uhasama baina ya Lulu na ndugu, jamaa, marafiki na wapenzi wa marehemu Steven Kanumba.
Alisema kuwa kilichomshtusha zaidi ni taarifa za polisi kusema kuwa kulitokea ugomvi kati ya Marehemu Steve Kanumba na Lulu, huku ikitajwa kuwa walikuwa wapenzi.
“Hatukutegemea kama Marehemu Kanumba angeweza kuwa na mahusiano y kimapenzi na binti yetu; kwanza ndiye tuliyekuwa tukimtegemea kwa kiasi kikubwa katika kuendeleza na kukikuza kipaji alichokuwa nacho Elizabeth”, alisema baba mtu.
“Ninaomba Wanasheria na wanaharakati wa haki za kibinadamu kuingilia suala hili na kusaidia katika kupatikana kwa haki dhidi ya shitaka la mauaji linalomkabili binti yangu Elizabeth na pia naomba swala hili lisichukuliwe kishabiki ama kwa hisia bali haki ichukue mkondo wake” alisema.
Alisisitiza kuwa jamii inatakiwa kutambua mazingira ya tukio hilo, ambapo chanzo kinasemekana ni ugomvi uliopelekea tafrani kwa Lulu kutuhumiwa kumsukuma Marehemu Kanumba kwa kile kinachodaiwa kuwa ulikuwa wivu wa kimapenzi na haiyumkini hakukusudia kumuua hivyo yeye anashangaa bintiye kuhusishwa moja kwa moja na mauaji.
“Ushiriki wa mwanangu kuhusu mambo ya sanaa nilikwishapata wasiwasi na mama yake mzazi alikuwa akiwasiliana na Marehemu Kanumba enzi za uhai wake ambaye alikuwa anamhakikishia usalama wa Lulu na kusema kuwa ataendelea kubaki kama mwalimu.. lakini leo nasikia alikuwa ni mpenzi - nilishtushwa” alisema Kimemeta.
Baba Lulu pia ameelezea kusikitishwa kwake kwa kushindwa kuhudhuria mazishi ya marehemu Steven Kanumba kuhofia usalama wake, na kusema mazingira yatakaporuhusu hata sitaki kufika nyumbani kwa marehemu Steven Kanumba na kutoa pole.
Bw. Kimemeta amesema kuwa anaungana na Watanzania wote kutoa pole kwa familia ya Marehemu Steven Kanumba na kutoa mkono wa pole kwa msiba huo mkubwa ambao haukutarajiwa.
Kasema kuwa Kanumba alikuwa bado ni kijana mdogo aliyeonyesha umahiri kwenye sanaa na kwamba amecha pengo kwa familia yake na Tanzania kwa ujumla.
 
HABARI KWA HISANI YA BONGOFLAVALINK.BLOGSPOT.COM

No comments:

Post a Comment