BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Monday, April 16, 2012

RUGE, SHIGONGO, ASHA BARAKA WAKABILIWA NA KASHFA YA KUCHAKACHUA FEDHA ZA MICHANGO MSIBA WA KANUMBA

MAJINA ya watu mashuhuri nchi hii, Erick James Shigongo na Rugemarila ‘Ruge’ Mutahaba- wote wakiwa ni wadau wa tasniya ya Habari yako hatarini kuingia doa.
Kwa nini? Hiyo inatokana na kuwamo kwao kwenye Kamati ya mazishi ya mwigizaji Steven Charles Kanumba, ambayo imeingia kwenye kashfa ya kuchakachua michango ya msiba.
Baadhi ya vyombo vya habari nchini leo vimeripoti kuwa, habari kutoka ndani ya familia ya Kanumba, imeituhumu Kamati hiyo kufanya uchakachuaji wa michango hiyo inayokadiriwa kuwa mamilioni ya fedha, achilia mbali vitu kadhaa, yakiwemo magunia 32 ya mchele.
Kamati ya Mazishi ilikuwa inaundwa  na Mwenyekiti Gabriel Mtitu, Makamu Mwenyekiti, Jacob Steven ‘JB’, Katibu, William Mtitu na Wajumbe Issa Mussa ‘Cloud’ (Mweka Hazina), Kimosa, Vincent Kigosi ‘Ray’, Single Mtambalike ‘Richie’, Dilesh Solanki, Millenne Happiness Magesse, Adele Kanumba (dada wa marehemu), Hartman Mblinyi, Ruge, Ally Choky, Simon Mwakifamba, Eric Shigongo, Steve Nyerere, Mahsein Awadh ‘Dk Cheni’ na Mama Nassor, mmiliki wa nyumba aliyokuwa akiishi Kanumba.
Je, ukweli ni upi. Ni matarajio sasa wahusika wataibuka kujibu tuhuma hizi, hasa ikizingatiwa Kamati iliundwa na watu watu wazito kama Eric Shigongo, mmiliki wa Global Publisher, Ruge Mutahaba, Mkurugenzi wa Clouds Media Group.

Chanzo cha habari hii ni:http://bongostaz.blogspot.com/

No comments:

Post a Comment