BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Saturday, April 14, 2012

Ini Edo ala kiapo.....


Mwigizaji huyo anasema ingawa ndoa yake ni ngumu kwa kuwa mume anaishi Marekani na yeye Nigeria, anajitahidi kwa nguvu zote kuhakikisha haiyumbi.

Siyo rahisi kuimudu ndoa ya aina hii, lakini nimejiwekea mipaka ya kazi na maisha binafsi, unapokuwa muda wa kupiga kazi nafanya hivyo na unapofika wa kuwa na mume wangu, nakwea pipa kumfuata, anasema Edo.

Anaongeza kuwa pamoja na kuwa anatumia nguvu nyingi kuifanya ndoa yake idumu, lakini anashukuru kwa kupata mume muelewa ambaye anapohisi kazidiwa na kazi huwa anamfuata Nigeria kuwa naye pamoja.

Edo ameongeza kuwa ni miaka mitatu sasa tangu afunge ndoa na mwanamume huyo kwa hiyo kilichopo katika mpango ni kutafuta mtoto na kuanzisha familia.

No comments:

Post a Comment