BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Saturday, August 13, 2011

AFRICA MAGIC YAMPA SHAVU MR CHUZI...


MWIGIZAJI na mwenyekiti wa Watengenezaji wa filamu Tanzania Tuesday Kihangala ‘Mr Chuzi’ amesema ameridhishwa na uuzaji wa kazi zake kama ya Millosis, Jasmini na jumba la dhahabu katika kampuni ya Africa Magic inayotumia kuonyesha michezo mbali mbali duniani.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotufikia hivi karibuni tamthiliya ya jumba la dhahabu inatarajiwa kurudiwa kwa mara ya pili na kituo hicho, hivyo hiyo ni nafasi ya kipekee kwa wale wote waliokuwa hawajahawi kuiona ama walikuwa wanavutiwa.

Mr chuzi alionyesha kufurahishwa kwake na mkataba alioingia na kampuni hiyo na hivyo kuahidi kufanya kazi nzuri na zenye ubora zaidi ili kuwapa watazamaji na washabiki wake kile wanachostahili.
Msanii huyu amekuwa mahiri katika kufanya kazi mbali mbali hivyo kuzidi kuijenga tasnia hiyo.


No comments:

Post a Comment