BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Monday, August 8, 2011

JENIFFER MGENDI KUJIKITA ZAID KTK GAME YA FILAMU..


JENNIFER Mgendi ni kati ya waimbaji nyota wa nyimbo za Injili aliyefanikiwa kwa kiasi kikubwa. Nyota huyo anasema matarajio yake nikuwa muongozaji na muandaaji wa filamu ili kueneza injili kwa njia ya uimbaji na uigiza.
Mgendi ambaye amedumu kwa miaka 16 katika gemu la muziki wa Injili, anasema amefanikiwa kwa kiasi na kwamba kazi zake zinakubalika ndani na nje ya nchi.

Anasema, matarajio yake ni kujikita zaidi katika kutayarisha filamu na kwamba amefanikiwa kucheza filai ya Joto la Roho, Pigo la Faraja na Teke la Mama.
“Mafanikio yangu niyakawaida, namshukuru Mungu kwa kuwa naweza kuendesha familia yangu. Malengo yangu kiakili ni kujikita zaidi katika utayarishaji wa filaimu ili niifikishie jamii ujumbe kwa njia ya nyimbo na maigizo,” alisema Mgendi.

No comments:

Post a Comment