BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Monday, August 8, 2011

MSANII NYOTA WA FILAMU NIGERIA AFARIKI DUNIA…


MSANII nyota wa filamu nchini Nigeria Sam Loco Efe, amefariki dunia na kwa taarifa zilizotufikia ni kuwa msanii huyo alifariki dunia akiwa katika chumba cha hotel Imo State.
Inasemekana kuwa Sam Loco alifariki akiwa location siku hiyo na mpaka hivi sasa familia yake bado haijatoa taarifa kamili kuhusiana na taarifa za msiba huo na chanzo cha  kufariki kwake.

Msanii huyo ambaye ana umri wa miaka 66 alianza rasmi kuingia katika tasnia hii ya maigizo kupitia tamthiliya mbali mbali ziliyokuwa zikonyeshwa katika vituo mbali mbali vya televisheni nchini humo kuanzia miaka ya 70.
Kwa kifupi tuu  Sam Loco Efe-ni mzaliwa kutoka  Benin City, Edo State lakini alizaliwa Enugu. Hata vivyo alikulia katika maeneo ya Abakakili. Na alijiingiza rasmi katika fani hii baada ya kutazama kazi iliyofanya na wanafunzi wa chuo cha serikali cha Umuahia.
Na aliajiriwa huko Michelin, Ijora, Lagos lakini kwa muda mfupi aliondoka na kujiunga na Dunlop mwaka 1969. Efe alianza rasmi kufanya kazi hii mwaka 1970.

MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHARI PEMA PEPONI

No comments:

Post a Comment