BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Saturday, August 20, 2011

SHAMSA APANIA KUMFIKIA OPRAH..


SHAMSA Ford ni msanii wa filamu nchini anayeingia kwa kasi katika tasnia hiyo huku akiwa na malengo ya kufikia mafanikio ya muongozaji maarufu wa vipindi mbalimbali vya televisheni nchini Marekani, Oprah Winfrey.


Shamsa ambaye jina la baba yake linafanana pia na jina la baba wa muigizaji maarufu nchini Marekani, Harrison Ford, ameanza kucheza filamu mwaka 2010 na kuweza kukubalika na watu wengi hasa waongozaji wa filamu ndani na nje ya nchi.



Anasema anatamani kuwa mwanamke wa heshima sana katika ulimwengu huu na baadaye kuwa muigizaji wa kimataifa kama ilivyo kwa Oprah winfrey muongozaji maarufu wa vipindi mbalimbali vya televisheni nchini Marekani.


“Maishani mwangu natamani vitu viwili tu, kuwa mwanamke wa heshima sana katika ulimwengu na muigizaji wa kimataifa. Tukizungumzia Oprah ni mwanamke anayeheshimika sana anauwezo wakufika hapa nchini na kuingia Ikulu kuzungumza na Rais na mawazo yake yakasikilizwa na kutekelezwa leo hii sisi wasanii wa Tanzania hatujaweza kufikia hatua hiyo natamani kuwa wa kwanza,” anasema.



Shamsa anasema, katika kipindi cha muda mfupi ambacho ameanza kuonekana kwenye filamu, ameona mafanikio na kwamba tayari ameanza kupata tenda za kucheza filamu nje ya nchi.

No comments:

Post a Comment