BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Saturday, August 13, 2011

WASANII WA FILAMU WAWALALAMIKIA WASAMBAZAJI...


BAADHI ya wasanii ambao ni wanachama wa shirikisho la filamu nchini TAFF, kutoka mkoa wa Kinondoni, walikutana wiki hii kujadili mqmbo mbali mbali yanayolenga kuimarisha shirikisho hilo.
Miongoni mwa mambo waliyoyatilia mkazo ni kudharauliwa kwa wasanii wachanga na wale wasiokuwa na majina, kusambazwa kwa kazi za wenye majina pekee kukumbatiwa kwa wasanii wachache na kufanyiwa promo kwa video zao, mtandao wa magazeti ambao unaharibu tasnia.

Wasanii walichangia mada kwa kusema, watu ambao walianzisha TAFF na ndio hao hao waliokuja kuivunja na kuanzisha Bongo Movie Club amabo wanasadikiwa hawalitambui shirikisho wala Rais wa shirikisho hilo. Wasanii wengine walitoa kero zao za moja kwa moja kwa kampuni yausambazaji wa filamu Tanzania ya Steps.
Wengine hawakuacha tua shutuma zao kwa wasanii ambao walimeshajijengea jina kwamba wanatumia fedha ili kuuza sura kwenye magazeti.

No comments:

Post a Comment